Hivi kwanini BOT hawatoi tamko kuhusu crypto currency

Mzee_londo

Member
Dec 5, 2018
46
99
Nimepokea ujumbe ufuatao kutoka whatsapp na umenifungua akili sasa ni kwanini serikali kupitia BOT Au Waziri husika wapo kimya

Ujumbe wenyewe

“Habari Mtanzania mwenzangu,

Leo nataka nikutahadharishe na utapeli kuhusu biashara haramu ya Sarafu za kidigitali (cryptocurrencies) ambazo zipo aina nyingi na zifuatazo ni chache tu;
1. Bitcoin
2. Lite coin
3. Ethereum

Nadhani katika majukumu yako ya kila siku ushawahi kukutana na wakaka watanashati au wadada warembo wakakuomba muda wako ili waweze kukushirikisha kukuelezea fursa ya biashara na ukatenga muda wako, kilichofuata ni kushawishiwa kufungua akaunti aidha ya dola za kimarekani 10000$, 5000$, 2000$ au 500$ baada ya maelezo mareefu ya kukushawishi huku ukiahidiwa faida kubwa zenye marejesho kilasiku. Kama bado basi utakutana nao hivi karibuni.

Ndugu zangu huu ni utapeli tena unaenea kwa kasi kama ilivyokuwa DESI au D9, epuka kutapeliwa waingereza wanasema “there is no easy money”. Huu ni utapeli kwasababu zifuatazo:

1. Umiliki wa hizi sarafu za kidigitali, ili kitu chochote kiitwe pesa lazima kiwe na mmliki lakini pesa hizi mmiliki wake hawafahamiki mpaka sasa. Hapa kuna wasiwasi kupotea katika soko bila kujua nini kimetokea ni kama kuteleza tu!
2. Ustahamilivu katika soko, pesa hizi zimekuwa zikipanda thamani kila kukicha na kushuka. Kupanda kwake thamani huwa maradufu hii inaleta wasiwasi kwamba siku zitakuja kushuka vibaya sana.
3. Serikali kupitia benki kuu haitambui hizi sarafu na nimatumaini yangu muda si mrefu watatoa tamko rasmi.
4. Hakuna sheria inayosimamia hii biashara ukitapeliwa huna pa kuanzia
5. Upatu, hii ikimaanisha hakuna kinachofanyika zaidi ya wale waliojiunga kukopeshana wenyewe. Ukijiunga leo unasaini mkataba wa mwaka mmoja ndo uchukue pesa yako.
6. Utakatishaji pesa na ukwepaji kodi, watu wanatumia hii biashara kutakatisha pesa na pia faida inayopatikana kutokana Na hii biashara haikatwi kodi. Epuka kuanguka kwenye mikono ya TAKUKURU
7. Kampuni zinazojihusisha Na hii biashara hapa Tanzania zimekuwa zikibadilisha majina kila mwaka hii sio dalili nzuri

Mwisho nasikitika kwamba watanzania wenzangu takribani 6800 wameweza kuingizwa katika utapeli huu.

Nakutakia kazi njema”

Toa maoni yako
 
Tatizo la Tanzania ni Elimu
Mwenye mamlaka hajui mipaka yake wala majukumu yake
 
Elimu elimu elimu.
Hata alieandika hapo juu bado hafahamu namna modernization decentralized monetary system hizi za Cryptocurrency zinavyofanya Kazi.
Cryptocurrency sio utapeli ni mifumo kama mifumo mingine ya kifedha duniani sema kwenye pesa matapeli ndio na wao wanaishi karibu napo ila crypto ni mfumo wa kifedha unaohitaji ufahamu mpana sana wa masuala ya kifedha ili uuelewe vinginevyo hata ukiwa mtaalamu wa masuala ya kibenki ukiteleza kidogo tu unalizwa na wajanja.
 
Watanzania wengi wana uwezo mdogo sana wa kuchanganua mambo..

Kabla ya kutumia crypto currency unasoma terms and condition,then kwa akili yako unaamua ufanye lipi..

Bitcoin ni sarafu tu ambayo ni exchange method that all..mtu akisema ni utapeli ni lazima aelezee pia utapeli unatoka wapi??

Marekani kuna kampuni kama coinbase ambayo inajihusisha na sarafu hii na inabidi ufanye verification ili uweze kuitumia na pia wapo regulated na Federal reserve ya Marekani..
 
Watanzania wengi wana uwezo mdogo sana wa kuchanganua mambo..

Kabla ya kutumia crypto currency unasoma terms and condition,then kwa akili yako unaamua ufanye lipi..

Bitcoin ni sarafu tu ambayo ni exchange method that all..mtu akisema ni utapeli ni lazima aelezee pia utapeli unatoka wapi??

Marekani kuna kampuni kama coinbase ambayo inajihusisha na sarafu hii na inabidi ufanye verification ili uweze kuitumia na pia wapo regulated na Federal reserve ya Marekani..
Umejibu vizuri mkuu ila wengi hawajui mengi kuhusu Bitcoin.

Bitcoin ni sarafu kama sarafu zingine ikitumika zaidi kwenye "investment" and "transaction" Duniani. Sababu inakubalika kununulia hata magari Duniani. Na hata kubet unaweza kubet via Bitcoin kwa kampuni za ulaya.

Na ndio sarafu pekee Duniani iliyowahi kufikia thamani ya million 50 kwa sarafu moja mwishoni mwa mwaka 2017. Hii ni rekodi ambayo hata dola haijawahi kuifikia.

Bitcoin sio utapeli ni pesa za mtandaoni zilizotengenezwa kwa cryptographic codes na inaaminika ndio future monetary system ijayo.

Huwa nawashangaa watu wasio na uelewa wanakariri kwamba Bitcoin ni utapeli.. How comes? Bitcoin ambayo Bill gate kawekeza hela yake kule iwe utapeli? Wewe unadhani BOT ina expert wa financial advisor zaidi ya Bill Gates? Waliomshauri awekeze hela zake kule?

Mkuu nadhani wengi hawana hii elimu na wanazungumza hisia tu na sio utaalamu. Watuulize sisi expert wa decentralized system.
 
Back
Top Bottom