Hivi kumbe uwanja wa Mkwakwani ni wa CCM?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,136
7,905
Dah nimeshtushwa sana nilipokuwa naangalia mechi za ngao ya jamii kuona nembo ya CCM pale uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Sikuwahi kujua ule uwanja unamilikiwa na chama. Kwa hiyo maboresho yote yale ya taa na nyasi yanafanywa na nani?

Jana tena nimeshtuka kumsikia Mkuu wa mkoa wa Morogoro alipokuwa anaongelea kuhamisha mechi ya leo ya Simba na Mtibwa uende uwanja wa Jamhuri akauita "CCM Jamhuri", hili nalo nilikuwa sijui kabisa. Uwanja wa Manungu ni moja ya viwanja vyenye pitch bora kuliko vyote Tanzania.

Nafikiri tunapojadili nini kinakwamisha maendeleo ya michezo nchini, hili nalo la kuangalia.
 
Dah nimeshtushwa sana nilipokuwa naangalia mechi za ngao ya jamii kuona nembo ya CCM pale uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Sikuwahi kujua ule uwanja unamilikiwa na chama. Kwa hiyo maboresho yote yale ya taa na nyasi yanafanywa na nani?

Jana tena nimeshtuka kumsikia Mkuu wa mkoa wa Morogoro alipokuwa anaongelea kuhamisha mechi ya leo ya Simba na Mtibwa uende uwanja wa Jamhuri akauita "CCM Jamhuri", hili nalo nilikuwa sijui kabisa. Uwanja wa Manungu ni moja ya viwanja vyenye pitch bora kuliko vyote Tanzania.

Nafikiri tunapojadili nini kinakwamisha maendeleo ya michezo nchini, hili nalo la kuangalia.
unaposema Manungu ina pitch bora kuliko viwanja vyote tz nakataa
 
nilikunukuu vyema maana ulitumia neno 'kuliko'

Lakini kwa kuwa umesahihisha kwa kusema miongoni mwa top 4 hapa nakubaliana na wewe
Mkuu unaleta ubishani usio na maana. Maneno niliyosema ni haya "Uwanja wa Manungu ni moja ya viwanja vyenye pitch bora kuliko vyote Tanzania". Nikisema "ni moja ya" ina maana hiyo hiyo na kusema "miongoni".
 
Uwanja wa Manungu ni moja ya viwanja vyenye pitch bora kuliko vyote Tanzania

Ushawahi fika MANUNGU wewe
ukiachana na pintch mbovu kama mvua inenyesha wiki moja nyuma hamuwezi kucheza vizuri FULLTOPE na kama ilinyesha ASUBUHI mashabiki pakusimama hakuna mana watasimama kwenye mAdimbwi ya maji
Yaan huo uwanja hata pakukaa hakuna watu wanakalia mawe mabenchi yake hata ya vibanda umoza yana afadhari

Vyoo sasa mpk utoke nje ya uwanja utembee nusu kilomita 1

Ni moja kati ya VIWANJA VYA HOVYO KABISA
 
Ushawahi fika MANUNGU wewe
ukiachana na pintch mbovu kama mvua inenyesha wiki moja nyuma hamuwezi kucheza vizuri FULLTOPE na kama ilinyesha ASUBUHI mashabiki pakusimama hakuna mana watasimama kwenye mAdimbwi ya maji
Yaan huo uwanja hata pakukaa hakuna watu wanakalia mawe mabenchi yake hata ya vibanda umoza yana afadhari

Vyoo sasa mpk utoke nje ya uwanja utembee nusu kilomita 1

Ni moja kati ya VIWANJA VYA HOVYO KABISA
Mambo ya mvua hata kwa Mkapa ni hivyo hivyo tu. Na pia nilikuwa naongelea pitch wala siyo majukwaa au huduma za nje. Halafu hoja ya msingi hapa ni uwanja wa Mkwakwani kuwa chini ya CCM, hayo mengine ni nyongeza tu.
 
Back
Top Bottom