Hivi kifo kina siri gani

Hivi kifo kina siri gani

Hakuna mwenye majibu timilifu kuhusu siri ya kifo.
Hii ni kwa sababu hatuna uwezo wa hiari wa kwenda upande wa pili na kurudi na majibu kamili. Vivyo hivyo kwa wafu.
Siri yao ni nzito sana. MANAKE wanajua kama moto upo huko au haupo.
 
Nani alikudaganya kwamba kuna malaika/kiumbe mtoa roho anaitwa ISRAEL?
Kwa kifupi hakuna malaika huyo!
Malaika wa kifo yupo na anajulikana kwa jina la Azrael, Samael,Salieri katika uyahudi.

Wapo wengi Kila mtu na kazi yake
 
Mbona kifo hakina siri yoyote. Bible tyr imeainisha mtu aapokufa anapande mbili mbele yake, kama alikuwa na matendo mema basi anaenda Paradiso kama anamatendo Mabaya hapo hapo baada ya kufa ni Motoni kuchomwa moto.
 
Nikisikiaga mambo ya kufa kufa nakonda sana nataman nisizeeke nisife sijui nikimbilie wapi
Acha kuwa na ugonjwa wa panic attack wewe kinacho kusumbuwa na kijua hahahahahah aha ila pole saana ndugu yangu kuwa una tumia karafuu na kupenda kusikiliza bahari zile ambazo zina kuwa wasiwasi na kufanya moyo wako kwenda mbio na kuhisi kuwa utakufa sasa hivi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kifo hakina Siri, mwili ukizeeka na kuchoka roho inaondoka, na ndio kifo. Inaenda kuanzisha maisha mengine, hakuna cha mbinguni wala motoni.
 
Oya emu huo ufala wako uwaambie madogo zako wa kijijini huko, haujui humu tumo watu wazima umri wa baba ako??

Unatuita makusudi utufunge kamba shingoni?
 
Kuna mtoto wa ndugu yetu(miaka 5) alikuwa anasoma chekechea katika shule inayomilikiwa na taasisi ya Roman catholic alifarika mwaka jana mwezi wa 9,tulimzika salama. Siku tatu baadae aliyekuwa mwalimu wake alikuwa anafungua mlango wa ofisini kwake akamkuta yule mtoto amekaa anafungua kurasa za baadhi ya daftari zilizokuwa mezani. Yule mwalimu alirudi nje haraka na kukimbia kwenda kwa padre kumweleza alichokiona kule ofisini,padri akamsindikiza mwalimu ili kwenda kujionea mwenyewe alichosimuliwa. Kwa bahati mbaya hawakumkuta yule dogo tena pale ofisini lakini cha kushangaza lile daftari alilokuwa anapekua lilikuwa ni la kwake(marehemu) kwasababu wale watoto baada ya kumaliza masomo darasani daftari walikuwa wanaacha shuleni.

Binafsi huwa najiuliza sana juu ya kifo cha yule dogo na mwisho wa siku naishiaga kujisemea Mungu ndyo mpangaji wa vyote.
 
wavaa kobaz wanajifanyaga wajuzi kuhusu kifo, wanavyokichambua dah yan utahisi uwaga kuna utalii uko wanaenda na kurudi. Siri ya kifo aijuaye ni marehemu,
 
Acha kuwa na ugonjwa wa panic attack wewe kinacho kusumbuwa na kijua hahahahahah aha ila pole saana ndugu yangu kuwa una tumia karafuu na kupenda kusikiliza bahari zile ambazo zina kuwa wasiwasi na kufanya moyo wako kwenda mbio na kuhisi kuwa utakufa sasa hivi

Sent using Jamii Forums mobile app

Acha tu ndugu
 
Watu wengi wanajiuliza je kuna maisha baada ya kifo
Na mimi pia najiulizaga swala hilo pia
Lakini mkasa huu nahisi utatusaidia sote kujua kitu fulani

Mwaka 2013 kuna mama mmoja kijijini kwetu alikutwa ameanguka shambani kwake watu fulani wakamuogota na kumpeleka hospitalini
Lakini kwa bahati nzuri na mbaya mama huyo alipona lakini alipooza kabisa mikono na miguu
Baada ya mwezi kazaa mama huyo alikufa
Na kumbuka ilikuwa juma pili ndo alifariki mama huyo na Juma tatu akazikwa
Sasa kuna siku mimi na mke wa brother yangu tulikuwa tunakwenda shambani
Tulivyo kuwa Karibu na shambani la mama yule mama marehemu maana tulikuwa tuna pita shambani kwake kwenda shambani kwetu
Tukaanza kuhisi nyama za mwili kusinyaa na mwili kuwa baridi pamoja na nywele kukokotwa wote tukahisi labda ni baridi ya asubuhi lakini tulivyo kuwa tuna Songea tukawa tuna sikia harufu kali na mbaya
Tulivyo angalia pembeni tulimuona mama yule ambaye alizikwa juma tatu yupo karibu na mti alafu alikuwa kama analia hivi
Tulikimbia mbio uku tukilalamika kwa bahati nzuri kulikuwa kuna pita akina baba wa wili hivi walisikia kelele zetu Wakaja mbio kule ambako tulikuwa wajatuliza nini tatizo tukawapa mkasa wote walishangaa

Mwaka 2016 kuna kijana mmoja ambaye alikuwa ana toka south Afrika uko alikuja kutibiwa kiasili kijijini kwetu lakini kwa kwa bahati mbaya kijana yule hakupona alifariki

Baada ya kupita wiki mbili kuna siku nilikuwa zangu tu nimelala mchana nikaota kijana huyo ana kuja kuniambia kuwa ni mwambie Mke wake achukuwe mtoto wao na pesa ambazo ziko ndani ya pochi lake kwenye suruali jeusi dollars 800 wakimbie sehemu ile ambayo wakaa
Mimi niliamuka uku nikiwa na maswali mengi kichwani juu ya ndoto hiyo kama ni kweli au ni ndoto tu ya kama ndoto zingine
Nilipotezea lakini moyo wangu ukawa unaniambie nenda nenda
Kabla ya kwenda nilimpa habari hizo mama yangu akanishauri kuwa niende kumpa habari hizo mke wa marehemu
Nilikwenda kumpa habari hizo uku moyo wangu ukiwa na maswali mengi nikifikiri nitaonekana Muongo
Nilikwenda kumpa taarifa hizo alinibishia lakini alivyo kwenda kucheki akakuta kweli pesa hizo zipo alishangaa saana

Je kifo kina siri gani? ]
Huyo mama aliekufa then mkamuona shambani kwake anatoa harufu mbaya sana halafu analia kwa uchungu.

Inaonekana hakua mtu mwema katika maisha yake hapa duniani, na amekufa katika hali ya dhambi bila kutubu hiyo ni dalili yakua yupo mahali pabaya anateseka.
 
Dah ww una maneni makali
Pole sana sikuwa na maana ya kukuumiza ila hata mimi kwa umri wangu huu naona mda unazidi kukaribia
Wengi wametangulia wakiwa bado wadogo Sana yaani marafiki zangu kibao
Ila hakuna namna ipo siku na mimi ntaondoka tu

Kumbuka baada ya miaka 110 hakuna hata mtu mmoja alie hai sasa atakuwepo
 
Pole sana sikuwa na maana ya kukuumiza ila hata mimi kwa umri wangu huu naona mda unazidi kukaribia
Wengi wametangulia wakiwa bado wadogo Sana yaani marafiki zangu kibao
Ila hakuna namna ipo siku na mimi ntaondoka tu

Kumbuka baada ya miaka 110 hakuna hata mtu mmoja alie hai sasa atakuwepo

Inatosha bhna eboo
 
Back
Top Bottom