Jamani kuna wanaume ambao wanaoa then wanaenda kuweka kambi kwa wazazi wa mke yaani ukweni, hivi utakuwa na sauti kweli ya kuongea juu ya mkeo? c utakuwa kazi yako we kucheka tu kama ***** na wanaume mnalichukuliaje hili? tabia hii inakera bwana.
Jamani kuna wanaume ambao wanaoa then wanaenda kuweka kambi kwa wazazi wa mke yaani ukweni, hivi utakuwa na sauti kweli ya kuongea juu ya mkeo? c utakuwa kazi yako we kucheka tu kama ***** na wanaume mnalichukuliaje hili? tabia hii inakera bwana.
vipi wa lwalo yuko ukweni nini? LOL
Kikwetu hiyo 'hairuhusiwi ' kabisa ni uvunjifu mkubwa wa mila na desturi, unavunja heshima ya jamii yenu na ya kwkao kama mwanaume so unadharaulika mazima. Hata kulala kule bila sababu maalum hairuhusiwi kabisa
sasa huyo nahisi sio mwanaume kamili...ana matatizo gani? hana nyumba? kazi?
Kaizer, we acha tu tuna kaka yetu isee tena wa pekee, ana kazi mnzuri tu ila sijuhi nini kimempata wadada tumekaa kupanga kila mbinu ya kumchomoa atleast wakapange ila braza kang'ang'ana ukweni ndio kwanza anamwambia mkewe dada zangu wasumbufu kweli! mwanamke nae hataki hata kutusikia, na kabla hajamuoa alikuwa amepanga nyumba mnzima sinza ila alivyo muoa tuu kahamishia vilago ukweni, inauma sana kwa kweli
vipi wa lwalo yuko ukweni nini? LOL
Kikwetu hiyo 'hairuhusiwi ' kabisa ni uvunjifu mkubwa wa mila na desturi, unavunja heshima ya jamii yenu na ya kwkao kama mwanaume so unadharaulika mazima. Hata kulala kule bila sababu maalum hairuhusiwi kabisa
sasa huyo nahisi sio mwanaume kamili...ana matatizo gani? hana nyumba? kazi?
Kaizer, we acha tu tuna kaka yetu isee tena wa pekee, ana kazi mnzuri tu ila sijuhi nini kimempata wadada tumekaa kupanga kila mbinu ya kumchomoa atleast wakapange ila braza kang'ang'ana ukweni ndio kwanza anamwambia mkewe dada zangu wasumbufu kweli! mwanamke nae hataki hata kutusikia, na kabla hajamuoa alikuwa amepanga nyumba mnzima sinza ila alivyo muoa tuu kahamishia vilago ukweni, inauma sana kwa kweli
kwa hiyo ukakasirika kikwelikweliiiii....hahahahahahaJamani naomba niwashirikishe hii story ni ya kweli na imetokea. Mimi ni mchaga na nimeoa mchaga na wote tunaishi Dar mke wangu yeye wazazi wake wana hali nzuri kule moshi na wana nyumba nzuri sana kule kijijini wakati mimi kule kwangu kuna kibanda cha matope tuu. Tangu tulipooana ndugu za mke wanakaa kwangu mpaka leo wa kike na wa kiume. Pia wakwe zangu huwa wananitembelea na wanakaa kwangu wakija Dar. Sasa kuna mwaka Fulani kulitokea msiba moshi nikasafiri na mke wangu kwenda kuzika baada ya mazishi nikawa nimeamua kwenda kulala moshi mjini, tulipomuaga mama mkwe akatuambia hapana laleni tuu hapa nyumbani mbona kuna room ambazo hazina watu? Basi tukaamua kupaki gari letu nje tukaingia ndani mapema tukalala maanatulikuwa tumechoka kwa safari. Shemeji yangu aliporudi akakuta gari nje alimuuliza mama yake, hawa mbona wameacha gari hapa wammeenda wapi? Mama mkwe akamjibu kuwa wamechoka wamelala. Jambo hilo lilimchukiza sana shemeji yangu na nilipoamka asubuhi kumuga kuwa nasafiri kurudi Dar alinitizama kwa ghadhabu sana na kuniuliza . Hivi nani alikuruhusu kupaki gari hapa nyumbani na kama usingelikuta asubuhi hii ungemuuliza nani?. Swali hili lilinikera sana na nikamjibu si ningekuuliza wewe ambaye ndiye mwenyeji wangu?. Akaniambia kuanzia leo sitaki uwe unalala hapa nyumbani. Kauli hii iliniudhi sana na kwa sababu mke wangu ambaye ni dada yake alikuwepo na alikuwa anasikia maneno hayo, mimi nilimjibu sawa wala hutakaa unione tena hapa na huyu dada yako ambaye ndiye aliyenileta hapa ana hiari yake kuondoka na mimi for good au kubaki hapa for good. Mama watoto aliamua kuingia kwenye gari analia njia nzima mpaka Dar. Basi tulipofika dar nilimwambia mama watoto afanye utaratibu wa kuwaondoa wadogogo zake wa kike ambao walikuwa wanakaa kwetu na pia watoto wawili wa kaka zake wengine waliokuwa wanakaa kwetu wakiwa wanasoma wafanyiwe utaratibu wa kuhama pale maana sikuona sababu ya kuendelea kuwasaidia tena. Uamuzi huo haukuweza kutekelezeka kwa sababu kila nilipomtaka mke wangu awaeleze ndugu zake uamuzi wangu huo alikuwa analia tuu na kudai kuwa namuonea na nia yangu ni kumtesa kwa masimango ili afe na kwamba yeye hatofanya hivyo ila mimi niendelee tu kumtesa mpaka afe na tutakutana kwa mungu siku ya judgement ndipo itakapojulikana kama ni haki mtu kumuua mwenza wake kwa kosa ambalo siyo lake. Niliamua kubadilisha msimamo wangu na mpaka leo naishi na ndugu wa mke wangu na watoto wa kaka zake ili yeye afurahi tuu na sii vinginevyo. Niliamua kwenda kujenga haraka mahali pa kuwa nafikia na mpaka leo huwa nikienda ukweni huwa nasalimia nikiwa nimesimama wala sikai.
My take: mila za kiafrika ni kandamizi sana hakuna mahali ambapo zinampa favour kijana wa kiume ukweni hata kidogo. Hivyo wale ambao hawajaoa wafikirie mara mbili kabla ya kufanya maamuzi.
Fulani kulitokea msiba moshi nikasafiri na mke wangu kwenda kuzika baada ya mazishi nikawa nimeamua kwenda kulala moshi mjini, tulipomuaga mama mkwe akatuambia hapana laleni tuu hapa nyumbani mbona kuna room ambazo hazina watu? Basi tukaamua kupaki gari letu nje tukaingia ndani mapema tukalala maanatulikuwa tumechoka kwa safari. Shemeji yangu aliporudi akakuta gari nje alimuuliza mama yake, hawa mbona wameacha gari hapa wammeenda wapi? Mama mkwe akamjibu kuwa wamechoka wamelala. Jambo hilo lilimchukiza sana shemeji yangu na nilipoamka asubuhi kumuga kuwa nasafiri kurudi Dar alinitizama kwa ghadhabu sana na kuniuliza . Hivi nani alikuruhusu kupaki gari hapa nyumbani na kama usingelikuta asubuhi hii ungemuuliza nani?. Swali hili lilinikera sana na nikamjibu si ningekuuliza wewe ambaye ndiye mwenyeji wangu?. Akaniambia kuanzia leo sitaki uwe unalala hapa nyumbani. Kauli hii iliniudhi sana na kwa sababu mke wangu ambaye ni dada yake alikuwepo na alikuwa anasikia maneno hayo, mimi nilimjibu sawa wala hutakaa unione tena hapa na huyu dada yako ambaye ndiye aliyenileta hapa ana hiari yake kuondoka na mimi for good au kubaki hapa for good.