Hivi huyu Mkumbo ni nani hadi anateuliwa?Alikuwa Muhadhiri,Mwanasiasa, Mtumishi wa Umma au Vyote?

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,701
Tunavyojua Watumishi wa Umma hawapaswi kujihusisha na siasa. Kuna kipindi huyu ndugu alitipitia Misukosuko hadi kutikisa ajira yake kisa kujihusisha na mambo ya CHADEMA. Nadhani alibadilika ndio maana akawa hadi prof. Hadi kesho nilijua Mkumbo ni Mshauri(Consultant) wa ACT wazalendo na kazi hiyo sidhani kama ni siasa bali ni ya kitaalam.

Kuteuliwa kwake na Rais kelele zimezuka kana kwamba amechukuliwa Kiongozi nguli wa Upinzani, Wengine wanalalamika Rais anaua Upinzani, Wengine Mchumia tumbo au Kibaraka wa CCM, Ninaowaelewa moja kwa moja ni wale wanaomlalamikia kwa kusaliti maoni yake juu ya Waadhiri kuteuliwa, Ingawa ninaamini ameisaliti kwa faida ya taifa.

Tunaanzia wapi Kusema Mpinzani huyu ndugu?
Au ameteuliwa akiwa kama nani?
Mpinzani, Mwalimu wa chuo na mtumishi wa Umma, Mwanasiasa machachari, Mshauri wa mambo ya kisiasa?

Ninaomba wajuvi wa haya mambo mnitoe tongotongo tusijekuwa tunapiga kelele kwa vitu ambavyo havipo...
 
Alikuwa Mtumishi wa Umma Mkuu, ajabu alishiriki siasa na hakutumbuliwa kama akina Baregu na Lwaitama. Isije ikawa ni TISS kazini!
Mtumishi wa umma, Muadhiri wengi wao ni washauri wa kitaalamu (Consultants na watafiti, nakosoleka) kwenye taasisi mbalimbali. Ni kosa kutoa ushauri wa kitaalam kwenye taasisi yoyote isiyo ya umma. Maana sio lazima mshauri kuwa mwanasiasa ila anatoa expert consultation kwenye eneo flani mfano utawala kisha anaendelea na shughuli zake...
 
Pro Kitila Mkumbo ni mtumishi wa umma mhadhiri wa Chuo Kijuu cha Dar es salaam.

Tuache kuwa na kudhaniadhania tu kila mtu ni TISS kwasababu ambazo hazina mizania yoyote.

Kwa sasa amechaguliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji tumwache afanye kazi.

Kila mtu na jinsi Mungu alivyompangia safari ya maisha yake kupitia juhudi unazofanya kila siku.

Prof Kitila piga kazi mitandao ina mambo mengi na toka siku ya kwanza ya uteuzi wako niliona mada za ukosoaji.
 
Huyo ni mtumishi wa umma "maalum" wapo wengi sana kwenye vyama vya upinzani mmojawapo ni Mabere Nyaucho Marando mjumbe wa kamati kuu ya Chadema.
Sasa wenye nchi wameamua kumrudisha Profesa Mkumbo kwenye utumishi wa juu baada ya kazi kubwa aliyoifanya akiwa upinzani.
 
Kwanza wanaomkosoa kitila kwa kumshauri rais aisiteue wahadhiri hawafikiri mara 2. Kitila hakuwahi kusema walioteuliwa wakatae hizo teuzi. Yeye alishauri tu rais asiteue na kama umeteuliwa basi huna budi kwenda. na ushauri mtu anaweza kuupokea au la.
 
Mnaolialia mnapoteza muda na ni vyema muda huo mngetumia kufanya mambo mengine ya maana yatakayoongeza thamani ya maisha yenu
 
Mnaolialia mnapoteza muda na ni vyema muda huo mngetumia kufanya mambo mengine ya maana yatakayoongeza thamani ya maisha yenu
hakuna anaelialia wakosoaji wanasema mtu wa upinzani amechukuliwa hivyo kupunguza nguvu kwao wakati jamaa amewahi kuweka wazi kwa capacity yake kazi anayofanya ni kushauri wanasiasa sio siasa.
 
Tunavyojua Watumishi wa Umma hawapaswi kujihusisha na siasa. Kuna kipindi huyu ndugu alitipitia Misukosuko hadi kutikisa ajira yake kisa kujihusisha na mambo ya CHADEMA. Nadhani alibadilika ndio maana akawa hadi prof. Hadi kesho nilijua Mkumbo ni Mshauri(Consultant) wa ACT wazalendo na kazi hiyo sidhani kama ni siasa bali ni ya kitaalam.

Kuteuliwa kwake na Rais kelele zimezuka kana kwamba amechukuliwa Kiongozi nguli wa Upinzani, Wengine wanalalamika Rais anaua Upinzani, Wengine Mchumia tumbo au Kibaraka wa CCM, Ninaowaelewa moja kwa moja ni wale wanaomlalamikia kwa kusaliti maoni yake juu ya Waadhiri kuteuliwa, Ingawa ninaamini ameisaliti kwa faida ya taifa.

Tunaanzia wapi Kusema Mpinzani huyu ndugu?
Au ameteuliwa akiwa kama nani?
Mpinzani, Mwalimu wa chuo na mtumishi wa Umma, Mwanasiasa machachari, Mshauri wa mambo ya kisiasa?

Ninaomba wajuvi wa haya mambo mnitoe tongotongo tusijekuwa tunapiga kelele kwa vitu ambavyo havipo...
By the way, huyu Prof. Mkumbo kabobea katika masuala gani hasa na huko alikoteuliwa kuwa KM ni mambo gani hasa? Maana tunajua kuwa Mawaziri ni viongozi wa kisiasa na si lazima waziri awe na taaluma ya wizara husika, lakini vipi kwa Katibu Mkuu ambaye ndiye mtendaji mkuu wa wizara husika?
 
Watu kazini, task ya kwanza aliopewa imeisha muda wake therefore inafuata task nyingine ili kupoteza lengo. Muda wote watu wako kazini things undercover. 'Utamjuaje kuwa ni mwana wa Mungu!! jibu: kwa maneno yake na matendo'. Anyway wanaojua zaidi watakuja.
 
Mtumishi wa umma, Muadhiri wengi wao ni washauri wa kitaalamu (Consultants na watafiti, nakosoleka) kwenye taasisi mbalimbali. Ni kosa kutoa ushauri wa kitaalam kwenye taasisi yoyote isiyo ya umma. Maana sio lazima mshauri kuwa mwanasiasa ila anatoa expert consultation kwenye eneo flani mfano utawala kisha anaendelea na shughuli zake...
Kumbuka alipendekezwa kugombea urais kupitia ACT akakataa. Je consultant anaweza kupendekezwa?
 
Mtumishi wa umma, Muadhiri wengi wao ni washauri wa kitaalamu (Consultants na watafiti, nakosoleka) kwenye taasisi mbalimbali. Ni kosa kutoa ushauri wa kitaalam kwenye taasisi yoyote isiyo ya umma. Maana sio lazima mshauri kuwa mwanasiasa ila anatoa expert consultation kwenye eneo flani mfano utawala kisha anaendelea na shughuli zake...
Kwa maelezo ya ZITTO akielezea jambo hili alisema kwa nafasi aliyokuwa nayo MKUMBO katika chama alikuwa anashiriki vikao vyote vya chama,sasa mtu kama huyu unasema eti anatoa expert consultation kwenye eneo fulani mfano utawala kisha anaendelea na shughuli zake?
 
Sheria na kanuni za utumishi wa Umma seems zipo selective. Ndo maana watu kama bibi Tulia na former Jaji Mkuu walikuwa Watumishi wa Umma huku wakilipia kadi zao za CCM kwa uficho.

Sasa hivi si siri tena. MaRC, maDC, maDED, maDAS etc ni wanachama watiifu wa CCM na wala hawajifichi tena. Prof. Kitila aachwe tu na tena aendelee kuwa Mshauri wa ACT bila hofu. Precedence imeshawekwa na Mtukufu
 
Back
Top Bottom