Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 844
- 1,604
Akiwa Mkoani Kagera leo Jumanne Oktoba 14, 2025, Mwenyekiti wa Kampeni ya Kitaifa ya Mama Asemewe Bw. Geofrey Kiliba amesema Ushiriki wa Vyama 18 kati ya 19 katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 pamoja na mamilioni ya Watanzania wanaohudhuria mikutano ya kampeni za Vyama mbalimbali vya siasa nchini ni dhihirisho la kufeli kwa nia ovu ya baadhi ya watu waliokuwa wakieneza chuki na hamasa ya kususia uchaguzi.
Kiliba ameyaeleza hayo wakati akitoa tathmini ya Taasisi ya Mama Asemewe kuhusu Kampeni za uchaguzi huo, akisema watu hao waliokuwa wakihamasisha wananchi kususia uchaguzi walifika pia kwenye Taasisi za elimu na Jumuiya zake pamoja na kwa Viongozi wa dini nchini bila ya mafanikio, suala ambalo sasa limedhihirisha ukuu wa Mungu na mapenzi ya Watanzania kwa nchi yao.
"Hawa wahuni wamekataliwa na zaidi ya Taasisi 56, wamekataliwa na Watanzania, wamekataliwa kwetu Wanavyuo, wamekataliwa na wafanyabiashara wadogo, maafisa usafirishaji (Bodaboda na Bajaji) na wamekataliwa na Taasisi makini za kidini zinazotulea.
“Ninaamini kuwa hii vita tutaishinda kwa data na takwimu kwasababu Tanzania yetu ipo chini ya Mikono salama ya Mwenyenzi Mungu,” amesema Bw. Kiliba.
Aidha, Kiliba pia amezungumzia madai ya hivi karibuni ya kulihusisha Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ na siasa za Tanzania pamoja na tukio lijalo la uchaguzi Mkuu wa Tanzania, akisema kuwa Vijana wa Tanzania hawana hofu wala wasiwasi kwani Vyombo hivyo vya ulinzi na usalama vinao uwezo wa kuwadhibiti na kushughulika na watu hao aliwaoita kuwa wahuni wasioitakia mema Tanzania na watu wake.