Mu-sir
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 3,621
- 1,629
Wakuu nina ndugu yangu ambaye alipata udahili katika chuo kikuu cha TUMAINI campus ya Iringa na anachukua (BaEd). Tangu amejiunga hadi sasa hawajapata mkopo na katika kufuatilia bila mafanikio wakaamua kugoma leo lakini kabla hawajaanza mgomo wao wakakaa kikao na mkuu wa chuo ili kumhoji na alipoona maswali yamezidi aliwajibu kwa hasira kuwa "mkitaka mwende popote, kozi yenyewe haijasajiliwa halafu mnakuja juu" sasa je, hivi serikali inawezaje kuruhusu chuo kufundisha masomo ambayo hayajasajiliwa TCU? Hi nchi inaongozwa na watu gani? Au ni mazuzu? Nawasilisha.