jakackseru
Senior Member
- Mar 15, 2014
- 132
- 27
Kuna binti tulipendana kwa kipindi kirefu mpaka hapo kulipotoke sababu ya kutufanya tuishi pamoja japo sio mimba. Tumeishi wote huu mwaka wanne, siku hizi kimezuka tabia kila tunapopishana kauli hata kama ni kwenye simu basi anaondoka na kwenda kwa shangazi yake.
Akiwa huko nakuwa sijui mpaka ninaporudi nyumbani ndipo nakuta hayupo na simu yangu haipokelewi tena, ingawa ni sehemu ya karibu ambayo ni gari moja na nauli ni mia nne tu. Lakini huyo shangazi yake humpokea na kukaa naye hata wiki pasipo kunitaarifu na wala kuuliza kulikoni huko alipotoka.
Nimeivumilia hii tabia lakini inazidi kadri siku zinavyokwenda. Siku moja nikaamua kumtolea uvivu japo ni mtu mzima. Nikamuuliza kwamba, Je, huwa anajitafakari kwa hayo anayoyafanya? Alichonijibu siwezi kukiaandika humu.
Wadau naombeni ushauri wenu je hivi ndivyo tunavyotakiwa kuishi na mabinti wa siku hizi?
Akiwa huko nakuwa sijui mpaka ninaporudi nyumbani ndipo nakuta hayupo na simu yangu haipokelewi tena, ingawa ni sehemu ya karibu ambayo ni gari moja na nauli ni mia nne tu. Lakini huyo shangazi yake humpokea na kukaa naye hata wiki pasipo kunitaarifu na wala kuuliza kulikoni huko alipotoka.
Nimeivumilia hii tabia lakini inazidi kadri siku zinavyokwenda. Siku moja nikaamua kumtolea uvivu japo ni mtu mzima. Nikamuuliza kwamba, Je, huwa anajitafakari kwa hayo anayoyafanya? Alichonijibu siwezi kukiaandika humu.
Wadau naombeni ushauri wenu je hivi ndivyo tunavyotakiwa kuishi na mabinti wa siku hizi?