Hivi Hatumuoni Huyu......! au yuko sawa?

huyu jamaa ana nguvu ya ziada.
kumbukeni aliwahi kukiri hadharani kuwa yeye na JK hawajakutana barabarani

inawezekana kabisa anamuogopa na ana sababu kuu na ya msingi ya kumuogopa.

but all in all, hatima ya nchi yetu bado ipo mikononi mwetu sisi wananchi kwa kiasi kikubwa
tutumie vizuri nafasi ya kuchagua kiongozi mwenye sifa na maadili. sio fisadi mmwaga mapesa katika majumba ya ibada.
 
Ni kama serikali na chama chake wanamgwaya!!! Matokeo ya analolifanya yatatupeleka pabaya maana kila siku tunawasikia wakisema MSICHANGANYE SIASA na DINI!!!!! Sasa mtu anapoamua kufanya nyumba za ibada uwanja wake wa kujitambulisha=JANGA
 
Hakuna mtu wa kumzuia Lowassa. Wananchi wanampenda na hela anayo. Hata kama hupendi huna budi kukubaliana na ukweli japo ninaelewa unaumia lakini ndiyo hakuna namna ya kuubadilisha. Huwezi kuukimbia ukweli.
 
Hakuna mtu wa kumzuia Lowassa. Wananchi wanampenda na hela anayo. Hata kama hupendi huna budi kukubaliana na ukweli japo ninaelewa unaumia lakini ndiyo hakuna namna ya kuubadilisha. Huwezi kuukimbia ukweli.
Sina uhakika kama huwa unaelewa mada kabla ya kuchangia.Suala la msingi ni kufuata kanuni na maadili ya msingi ambayo yatasaidia wagombea kutoingia kwenye hali ya kuligawa taifa; na kisha baada ya hapo si uchaguzi upo bwana? sasa ya nini tupige makelele ?
 
CCM ndio waumini wa siasa za udini,hivi ndugu zangu watanzania mambo hayo angefanya zito,mbowe au slaa angeachwa hivi hivi na watanzania achilia mbali chama chake? Tafakali chukua hatua
 
 


Kama una ushahidi tuwekee,ila tujiulize mtu ameiba na tayari anazo pesa na hajachukuliwa hatua.Kaamua kutumia hizo hizo pesa kuimarisha nyumba za ibada badala ya kujijengea majumba ya kifahari nje ya nchi pengine ni moja ya namna yake ya kutubu je unataka kuwashauri viongozi wa nyumba za ibada wazikatae? Kuna majangili na wachawi na wauza madawa ya kulevya na wauza miili nk wanatoa sadaka ndani na nje ya nyumba za ibada bila kujitangaza.Tuwaache watumie hizo pesa watakavyo ilimradi wasivunje sheria.

Huyo mtu sidhani kama ana shida ya Urais maana kama nia ni hiyo angewahonga Nec ya chama chake kwani unauhakika gani kama atapitishwa na chama chake?

Tukirudi kwako je ww ni mkamilifu kiasi gani? Hujawahi kupiga deal? Ulipofanikisha haukutoa sadaka unaposali? Au hukununua zawadi kwa watu wa nyumbani kwako? Tusemeje sasa, tusitembee na hisia na wala tisiwe na hofu zisizo za lazima najua mtangulizi wake hawezi kumpa nafasi nafikiri nimeheshimu ushauri wako wa kutotaja majina ya watu.
 
Nape atoe jibu maana yeye ndiye katangaza kuwa mwanaccm atakayeanza kampeni ya urais mapema atachukuliwa hatua. Sasa mbona EL anaendelea kwa kasi baada ya kumaliza makanisa sasa kaingia kwa machinga na vijana. Muda si mrefu atahamia kwa wakulima na wafanyabiashara. Nape utamuweza EL kweli au ndio zile kelele za barua ndani ya siku 90 wawe wamejitoa mpaka leo kimya kama maiti!
 
 
Hakuna mtu wa kumzuia Lowassa. Wananchi wanampenda na hela anayo. Hata kama hupendi huna budi kukubaliana na ukweli japo ninaelewa unaumia lakini ndiyo hakuna namna ya kuubadilisha. Huwezi kuukimbia ukweli.
Nadhani mda mwingine hata unachosema hukijui. Hebu tetea hoja yako ieleweke we kibaka sio una jamba jamba tu humu. Kakufanyia nini la maana huyo fisadi?
 
Wewe umenena kitu. Jamaa anaweza kuhama chamaaa... Na mimi huko atakakoenda kura yangu itamfuata hukohuko.
 


Fedha yake ndiyo inayowafanya watu wamwogope kwani anaweza kufanya lo lote. Chezea nguvu ya pesa wewe.
 

Ndiyo maana ni mara chache sana huwa ninawaReply watu wanaoniQuote hapa Jukwaani kwasababu ya "pumba" zenu.

Kuchangia kwake ujenzi wa nyumba za ibada analigawa vipi taifa? It seems like you are INSECURE.

Kwanza hii thread yenyewe imejaa nadharia tupu ni kwavile umetukuta sisi waSwahili tunapenda mambo marahisi marahisi lakini kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kuchangia thread ambayo imejaa nadharia tupu (umeshindwa hata kulitaja jina la huyo muhusika umeishia kutuaambia "huyu mtu").

Ni aibu kwa threads za namna hii kuruhusiwa kuwepo hapa kwenye Jukwaa la Siasa. Huyu mtu?! WTF?
 
Asante kuliona hilo...sijui huyu jamaa anaogopewa nini? hakuna chombo cha habari kinachomfichua zaidi ya kummwagia sifa. au ndiyo vibahasha vyenyewe? Msitegemee Mr. Dhaifu akafanya hivyo kwa kuwa yeye ni dhaifu. Msajili mimi humwita Bwana Porojo...ukimsikiliza unakuwa kama unaangalia Origino Comedy vile, sioni uhalisia kwake. Nani mwingine, Katibu Mkuu wetu, Majanga...kana kwamba kaambiwa ukisema tu na mimi nalipua. kimyaaaaaaaaaa! M/Mwenyekiti, yeye ni bwana Mikwara...hana lolote. Labda akimaliza fungate. alishawahi kutishia kuwa atafukuza wote waliongia kwa rushwa....mpaka Yesu atakaporudi. Nani mwingine....Nyerere, amekufa!

Akiisha pata, nawaapia mtalipia mpaka senti ya mwisho ya fedha zote alizowapa! Ninukuu hapa! Kivipi? Mtajua wenyewe, si mlikula, mkashiba? Mtalipia!

Kwa hiyo, hakuna wa kumkemea mtu huyu! Full Stop!
 
navyoamini mimi fisadi huyu hawezi kuwa rais wa nchi yetu labda kama sikuzaliwa mara!ikitokea akawa basi bwana!
 
Nawewe niwalwale mafisadi huwezi kuwalazimisha watu cha kuchangia. Na unachokifanya ndicho vyombo husika havichukui hatua kwakuwa wote ni wanafiki eti wanaogopa kupoteza mwelekeo.
 
navyoamini mimi fisadi huyu hawezi kuwa rais wa nchi yetu labda kama sikuzaliwa mara!ikitokea akawa basi bwana!
kuna siku utakuja kukimbia kivuli chako mwenyewe .nakuambia hizi dini bora zisingekuwepo zimerudisha maendeleo nyuma sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…