Hivi CCM nyinyi tu ndio mnajua kutawala?

mastersajenti

Senior Member
Dec 4, 2015
165
23
Nimeshangazwa sana na taarifa ya kuvurugika kwa uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Kinondoni. Kwa mujibu wa maelezo ya Mkurugenzi wa manispaa hiyo ni kwamba fujo zilizuka baada ya wajumbe wa CCM kutoka Zanzibar kuja kupiga kura Manispaa ya Kinondoni kumchagua Meya. Hakika jambo hili haliingii akilini kabisa Mzanzibari kuwa Mjumbe wa halmashauri ya Kinondoni kama sio vurugu za CCM katika nchi hii.

Ni vema viongozi wa CCM wakawa wanaheshimu maamuzi ya wananchi na kutii Sheria na kanuni za nchi hii. Sisi sote tuna haki ya kuongoza na kutawala sio CCM pekee. Uchaguzi wa bara uligubingwa na malalamiko, uchaguzi wa Zanzibar mpaka sasa una matatizo makubwa na chaguzi zote in CCM.

Nchi yetu ni ya amani na utulivu. Madiwani wa Kinondoni ndio kisheria wana haki ya kumchagua Meya wao, mbona uchaguzi wa mwaka 2010 wajumbe wa CCM kutoka Zanzibar hawakuja kumchagua Mh. Mwenda?

Kama kura hazitoshi kubalini matokeo.
 
Hili ni jambo la aibu sana kutokea kwa zama hizi na pia chini ya Mkurugenzi msomi mwenye hadhi ya uhandisi. Tufike mahali tuache ushabiki wa kuweka wapambe kwenye siasa. Sifa ya elimu iwe shahada ya chuo kikuu tutoe wajingawajinga hawa
 
CCM ni wapuuzi mno hiyo ni kwa Kinondoni Sumbawanga na Ilala ni ujinga mkubwa
 
Kwani hawakupigwa waliovunja sheria? Mana kama mtu hataki kufuata taratibu atafutwe kokote apigwe tu mana hakuna namna nyingine.

Ndio maana CCM ilifeli kwa muda mrefu kwa ujinga wa kuwalazimisha watu wafanye wanachotaka. Kiongozi asiyependwa na watu ni ngumu mno kuwashawishi watu ili watekeleze majukumu yao. CCM imeshinda zaidi ya halmashauri mia na kitu lakini bado inangangana na zile chache walizoshinda wapinzani.

Wanataka kuficha wizi wao kwa nguvu.

Miradi yenu ya kuuza maeneo ya wazi Imefikia mwisho. Kubalini tu kuliko kuingiza nchi kwenye machafuko. Na ifikie sasa anayevunja amani kwa makusudi asiachwe akaendelea kutanua tu mitaani.
 
Mzanzibari ni mtanzania anuruhusiwa kuishi hata Namtumbo

Inawezekana uko usingizini mkuu. Kama huna laku comment siolazima nibora tu kukaa kimya.

Kwahiyo kwa akiri yako hiyo yaki ccm unaona nisahihi wazanzibar kupiga kura kumchagua mayor kinondoni siyo. Kweli yule mgombea wavipaumbele vya Elimu, Elimi, Elimu angesaidia wengi nchi hii.
 
Kabombe acha upumbavu suala sio Mzanzibari kuishi suala no kupiga kura kama hujaielewa mada sio lazima uchangie
 
Hii sasa ni dharau ya waziwazi ya wanaoitwa watawala wetu. Hii precedence wanayoweka ccm ya kudharau kila mtu na kujiona miungu itatuletea Shida baadae. Hivi watu wafanyeje sasa? mbona in manyanyaso kila upande?
 
Hiki Chama siku kitatoka madarakani nitakesha ninashangilia. Mungu nakuomba nisife mpaka nione CCM imetoka. Amen
 
Back
Top Bottom