Hivi bado watu wanaungama

Hivi bado watu wanaungama

Huyu jamaa alikuwa anaungama kwa Magufuli juzi!
9087655443.jpg
 
Baada ya kujua ni kuwateka watu kisaikologia sijawahi tena. Utampigiaje mwanaume magoti na kumwambia makosa yako? Ungama kwenye moyo wako na Mungu wako
Mkuu hauhofii kugeuka nguzo ya chumvi kama Ruth.
 
Kuungama kuna nguvu na baraka nyingi.
Nina ushahidi Mimi binafsi. Kaungame uone raha na Amani yake.
 
Unaweza kuungama hata mbele ya kanisa zima au umaiti wa watu. Cha msingi upo tayari kupokea fedheha na uadui kutoka kwenye huo umati kwa kukiri makosa yako kwa Mungu.
 
Kuungama kuna nguvu na baraka nyingi.
Nina ushahidi Mimi binafsi. Kaungame uone raha na Amani yake.
Tusiwe tunajazana ujinga jamani mambo kama haya kama unayaamini tafadhali usishawishi wengine kaa nalo moyoni ili uende mbinguni mzee baba
 
1 YOH. :2:1
Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,

1 YOH. :2:2
naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.
 
Tusiwe tunajazana ujinga jamani mambo kama haya kama unayaamini tafadhali usishawishi wengine kaa nalo moyoni ili uende mbinguni mzee baba

Kama wewe ni mkatoliki lazma uungame tena kwa padre. Hiyo ndio karama ya kutubu na kunyenyekea.
Kama hutaki basiii
 
Kuungama ni kwenda mwambia padre madhamb yako yote kwa maana ya kwamba hapo unamwambia Mungu...
Duuh unamwambia Padre mishemishe zako? Hawahawa mapadre walevi na wazinzi? Kesho nitamuuliza Padre X.....maana ni mzee wa gambe na anawatoto watatu wote amewapa majina ya Marais.......
 
Yohana 20:21-23

Basi Yesu akawaambia tens, Amani iwe kwenu; kama baba alivyonituma Mimi, Mimi nami nawapeleka ninyi." Naye akiisha kusema hayo, akavuvia, akawaambia, "pokeeni Roho Mtakatifu wowote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wowote mtakaowafungia dhambi , wamefungwa."
Kuungama dhambi kwa padri ni sawa tu.

Tatizo ni pale ukidhani kuwa bila kwenda kwa Padri huwezi kusamehewa dhambi.
Hilo ni tatizo.

Tuwakane sawa hapo tu.
 
Back
Top Bottom