Hamed bin Mohammed el Murjebi (
1837 –
14 Juni 1905)
Alijulikana zaidi kwa jina la
Tippu Tip.
Alikuwa mfanyabiashara mashuhuri katika
Afrika ya Mashariki na Kati wakati wa karne ya 19.
HISTORIA YAKE
Babake alikuwa mfanyabiashara Mwarabu Muhammed bin Juma, mamake aliitwa Nyaso. Hamed aliingia katika shughuli za biashara tangu umri wa miaka 12 akafaulu katika
biashara ya misafara kati ya
Zanzibar na
Kongo. Alipanga misafara ya ma
hamali waelfu akipeleka bidhaa kutoka
Bagamoyo kupitia
Tabora hadi
Ujiji kwa
Ziwa Tanganyika na ndani ya
Kongo. Bidhaa alizobeba alitumia kujipatia pembe za ndovu na watumwa; watumwa walisaidia kubeba
pembe za ndovu njia ya kurudi hadi pwani. Hemed alitajirika sana. Athira yake ilipanuka katika Kongo ya Mashariki hadi alitawala eneo kubwa sana.
Hamed akapata jina huko
Ulaya kwa sababu alikutana na wasafiri na wapelelezi Wazungu kama
David Livingstone,
Veney Cameron,
Henry Morton Stanley,
Eduard Schnitzer (Emin Pascha),
Hermann von Wissmann na
Wilhelm Junker ambao mara nyingi walipata misaada muhimu kutoka kwake.
Wabelgiji walipoanza kujenga ukoloni wao Kongo walimkuta kama mtawala wa Kongo ya Mashariki wakapatana naye na kumpa cheo cha gavana ya Mkoa wa Chutes Stanley ("maporomoko ya Stanley", leo
Kisangani) mwaka 1887 alichoshika kwa miaka michache.
Mabadiliko ya ukoloni yaliharibu biashara yake akarudi Zanzibar 1890/91 alipobaki bila misafari mipya hadi kifo chake mwaka 1905.
ASILI YA JINA LA TIPPU TIP
Jina la TIPPU TIP alipewa na kabila la Wazaramo kwasababu ya mlio wa bunduki yake uliokuwa unatoa sauti ya tip tip tip hivyo basi Wazaramo wakisikia tu mlio wa bunduki basi wanakimbia huku wakisema Tippu tip huyo anakuja.
Yeye mwenyewe aliona watumwa ni sehemu tu ya biashara yake akitajirika hasa na biashara ya pembe za ndovu.
Hamed bin Mohammed el Marjebi amejipatia nafasi katika historia ya Afrika ya Mashariki kwa kuandika
tawasifu au kumbukumbu ya maisha yake yeye mwenyewe. Katika lugha ya
Kiswahili ni mfano wa kwanza wa tawasifu.
Pia ni mfano wa pekee wa kumbukumbu ya kimaandishi ya matokeo ya siku zile zisizoandikwa na Mzungu lakini ny mwenyeji. Hakuwa mtu anayemuogopa Mungu
.