Until_The_End
JF-Expert Member
- Nov 21, 2020
- 1,708
- 2,687
Sisi wakatoliki tunasema tunapokea watu wa aina zote kama tunavyopokea na kusali na wazinzi, wezi wa kura n.kNini msimamo wake kuhusu mabwabwa kuwa sehemu ya ukatoliki?
Hapo ndio tutaanza kumpima uwezo wake kiimani. Akianza danadana ya kuupigia debe upinde tutampelekea moto wa mashambulizi mpaka ateme bungo.
Umevaaje?
🤣🤣🤣. Leo XIV ndo huyu sasa. Nyuma yake kuna akina Leo 13 kabla na kwa mujibu wa Wikipedia ni hawa hapa na miaka waliokuwa Mapapa kwenye mabano.Kwann hua wanawabadil majina?! Hao akina leo XVi ni kina nani?!
MmetishaWalau na sisi Mathematicians tumetoa Papa😁 katika historia ya kanisa
Mbona hata huyu wakwetu Protase Rugambwa aliteuliwa siku hiyo hiyo, angechaguliwa leo tungesema aliandaliwa kuwa Papa?Kwa mda alioyeteuliwa kuwa Kadnali ni kama aliandaliwa kuwa Papa, September 30, 2023 ni juzi hapo.
Uraia wake wa asili ni mmarekani.Kwa hio kumbe sio muamerika?
China wananifurahisha maana Rais lazima awe engineer na engineer ni mwanamahesabu mwenzetuWalau na sisi Mathematicians tumetoa Papa😁 katika historia ya kanisa
Hili limeshangaza! Kumbe naye asingekuwa Ngozi nyeusi angeula.Mbona hata huyu wakwetu Protase Rugambwa aliteuliwa siku hiyo hiyo, angechaguliwa leo tungesema aliandaliwa kuwa Papa?
Kwani wewe si mlokole?😂Walokole na masalia ya bibi Ellen G whites wanadai marekani ni taifa la kipepo sasa papa katoka huko ni moto juu ya moto maninaa
Amewahi kutembelea Tanzania mara kadhaa, kiswahili anakiongea vizur sanaHUYU NDIYE PAPA MPYA.
Robert Francis Prevost, aliyezaliwa tarehe 14 Septemba 1955 mjini Chicago, Marekani, ni Papa mpya wa Kanisa Katoliki, Anachukua jina la Papa Leo wa XIV. Kuchaguliwa kwake mnamo Mei 8, 2025, kunamfanya kuwa Mmarekani wa kwanza kushika wadhifa huu katika historia ya miaka 2,000 ya Kanisa Katoliki .
ELIMU NA MAISHA YAKE YA AWALI
Prevost amehitimu Shahada ya Sayansi katika Hisabati kutoka Chuo Kikuu cha Villanova mwaka 1977. Baadaye, akafanikiwa kujiunga na Shirika la Mtakatifu Augustino (OSA) mwaka huo huo, na akaweka nadhiri zake za milele mnamo Agosti 1981. Amepta Shahada ya Uzamili katika Theolojia kutoka Catholic Theological Union mjini Chicago, na kisha Shahada ya Uzamili na Shahada ya Uzamivu katika Sheria ya Kanisa kutoka Chuo Kikuu cha Kipapa cha Mtakatifu Thomas Aquinas (Angelicum) mjini Roma .
HUDUMA YA KICHUNGAJI NA UONGOZI
Baada ya kupewa daraja la upadre mwaka 1982, Prevost ametumika Peru mwaka 1985 kama mmisionari. Ametumikia katika maeneo mbalimbali ya Peru, ikiwa ni pamoja na Chulucanas na Trujillo, ambako amehudumu kama paroko, mkurugenzi wa malezi, mwalimu wa sheria za kanisa, na jaji wa mahakama ya kanisa.
Soma Pia: Kanisa Katoliki lapata Papa mpya wa 267, ni Robert Francis Prevost kutoka Marekani, ataitwa Papa Leo XIV
Mnamo mwaka 1999, alichaguliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Shirika la Augustino huko Chicago, na mwaka 2001 alichaguliwa kuwa mkuu mkuu wa shirika hilo duniani, nafasi aliyoitumikia hadi mwaka 2013 .
Mwaka 2014, Papa Francis alimteua kuwa msimamizi wa kitume wa Dayosisi ya Chiclayo nchini Peru, na mwaka uliofuata akawa askofu wa dayosisi hiyo. Katika kipindi chake huko, amehudumu pia kama makamu wa rais wa Baraza la Maaskofu wa Peru kuanzia mwaka 2018 hadi 2023 .
NAFASI ZA JUU VATICAN NA UCHAGUZI WA UPAPA.
Mnamo Januari 2023, Prevost aliteuliwa na Papa Francis kuwa mkuu wa Idara ya Maaskofu (Dicastery for Bishops) na rais wa Tume ya Kipapa kwa ajili ya Amerika ya Kusini. Katika nafasi hii, amekuwa na jukumu la kuidhinisha uteuzi wa maaskofu duniani kote, jambo lililompa ushawishi mkubwa ndani ya Kanisa Katoliki .
Katika hatua nyingine Aliteuliwa kuwa kardinali mnamo Septemba 30, 2023, na baada ya kifo cha Papa Francis mnamo Aprili 21, 2025, amechaguliwa kuwa Papa katika mzunguko wa nne wa upigaji kura wa mkutano wa makardinali (conclave) uliofanyika Mei 8, 2025 .
MAISHA BINAFSI NA MTAZAMO WA KICHUNGAJI
Prevost ana uraia wa Marekani na Peru, na Anajulikana kwa mtazamo wake wa wastani na uongozi wa kidiplomasia, akifanana na mtangulizi wake, Papa Francis, katika msisitizo wa huduma kwa maskini na mageuzi ndani ya Kanisa .
Kuchaguliwa kwake kama Papa Leo wa XIV kunatarajiwa kuendeleza mwelekeo wa mageuzi na ushirikishwaji ulioanzishwa na Papa Francis, huku akikabili changamoto za kifedha na kiroho ndani y
Mimi sina USHIRIKA na walokoleKwani wewe si mlokole?😂
Basi wewe ni mfuasi wa martin Luther.Mimi sina USHIRIKA na walokole
Yesu Kristo Akbar.....Takbiir
Mimi ni ndg wa mudy na bibi faizaBasi wewe ni mfuasi wa martin Luther.
Watu wanadhani kuwa mtu akiwa wa Dini ni kulaza,kumbe kinyume chake,!Sasa unasemea papa? Ukiona mtu anaitwa askofu jua ana PhD (hapo sijaongelewa makadinali ambao ndio wanakua mapapa).
NB: Achilia mbali askofu au kadinali, ukiona mtu kapata upadri jua kichwani kuna elimu ya maana sio hizi za kuungaunga!
Yaani,wanaanza aisee Anza na Dr,pro duuh utafikiri kalazimishwa Kusoma!Lakini hutasikia Dr.Papa Leo
Njoo kwa huyu aliepewa za kuunga unga.
Mheshimiwa …Daktari, Mama…