Historia fupi ya deni la Stirling Civil Engineering Ltd

Historia fupi ya deni la Stirling Civil Engineering Ltd

Kipenzi Changu

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
58,079
Reaction score
134,472
Ukifuatilia muhtasari wa hii hadithi ya Bilioni 90 (87) unachukia sana....

Tulipovunja mkataba wa kandarasi yao ya ujenzi wa barabara ya Wazo Hill hadi Bagamoyo (kibabe), Stirling Civil Engineering Ltd, wakatupeleka mahakamani.>>>> (TUKASEMA HATUTISHWI)

Tarehe 10 Desemba, 2009 - Mahakama ya Usuluhishi ya Paris ikaamuru tuwalipe fidia ya hasara tuliyowasababishia kwa kiburi chetu, ya dola za Marekani milioni 25 (Takribani Shilingi Bilioni 40 wakati huo) >>>> TUKAGOMA!

Serikali yetu ikakata Rufaa, tarehe 10 Juni 2010 hukumu ya rufaa ikasomwa, tukapigwa chini. Tukaamuriwa kuilipa kampuni hiyo fedha hizo vinginevyo kila mwaka mmoja utakaohesabiwa tutalipa na riba ya asilimia 8. >>>>TUKADHARAU!

Kutokana na ucheleweshaji wa malipo, deni hilo limeongezeka hadi dola za Marekani milioni 38.7 kufikia tarehe 30 Juni, 2017. Hii ni sawa na takribani shilingi Bilioni 90 za Tanzania. >>>> TUKAENDELEA KUGOMA!

Mwezi Julai 2017, kampuni inayotudai imekamata ndege yetu, 'Bombadier Dash Q400' - sharti la kurudishiwa ndege yetu (isipigwe mnada) ni sisi kulipa hizo shilingi bilioni 90. >>>> NDIYO TUMEKUMBUKA KUWAPIGIA MAGOTI!

[Tayari Waziri Mahiga amewaomba Stirling Construction tuwalipe Bilioni 30 (kama advance payment) waachie ndege yetu wakati mazungumzo mengine ya namna ya kumalizia deni lililobaki yakiendelea. Halafu kuna watu bila aibu wanasema Lissu ndiye sababu ya ndege yetu kukamatwa. Hivi Lissu anahusikaje hapa?]

Ninajiuliza hivi akili zetu tumemgawia mwekezaji gani?

Yani tunakwenda kuwalipa watu Bilioni 90, za bure [kwa uzembe wa mtu mmoja aliyevunja mkataba kwa kukurupuka.!]

Bilioni 90 ni sawa na Magari 3,000 ya Wagonjwa (Ambulances) na yangeliweza kugawiwa kila kata ya Tanzania.

Bilioni 90 ni sawa na matrekta 1,500 ya kisasa na tungeliweza kuyagawa kwa nusu ya kata za Tanzania na kwa miaka mitano idadi ya Makumi Elfu ya wakulima wangefaidika.

Bilioni 90 ni pesa nyingi sana, mno! Lakini zinakwenda kupotea hivi hivi, na wanaoohusika na kiburi kilichopelekea hasara hii siyo tu kwamba wamekataa kujiuzulu au kuomba radhi! Bali wanatumia nguvu kubwa zaidi kutaka umma uamini kuwa wao ni "watakatifu" na "hawafanyi makosa makubwa kama haya."

Tungekuwa na watu wenye utu wangelitoka hadharani, wangekiri makosa yao, wakajiuzulu na kuomba wasishtakiwe. Kinyume chake, waliotutia hasara hii ndo wako mstari wa mbele kuwatisha waliofichua KASHFA hii.
 
Mkuu hizo Billini 90 ni jela nyingi sana kiasi cha kuwezesha kupatikana Kwa huduma ya Maji japo Kwa mkoa Pendwa wa Dar! Inasikitisha Watu wanahangaika Maji Ni shida jamani ! Sijui nianze mchakato wa kutafuta appointment ya kwenda kumuona anko Magu ili kumweleza shida ya Maji iliyopo? Maana Watu wamefuatilia hadi Kwa Waziri imeshikana, halafu chakushangaza maeneo mengine Watu wako mita chache toka Bomba kubwa la Maji ya Ruvu lakini hawapati Maji wananunua Kwa bei kubwa sana! Tena Hawa Dawasco Dawa Yao ni kuwajengea hoja kuwa huenda wako nyuma ya Hawa wauza Maji siyo bure!
 
Hata zile hela zilizotumika ktk kuandaa mapendekezo ya katika mpya na zile zikizotumika ktk bunge la katiba bora zingetumika ktk kutoa huduma za Maji lakini badala Yake wamezitafuna bure hadi leo hakuna cha maana kinachoendelea lakini Mungu yupo na anaona hakika walipohusika na ule udhalimu Mungu atajua namna ya kuwashuhulikia !
 
Deni usababishe wewe lawama unipe mimi
Nadhani huyu amevunja rekodi na kuwa binadamu wa kwanza tokea kuumbwa kwa Tanganyika na Tanzania kuzalisha hasara kubwa kiasi hicho kwa kiburi chake. Hili haliwezi kupita hivi hivi, kama sio 2021 basi majaliwa 2026 lazima tutabadili kipengele fulani katika katiba ili mtu fulani akaone kule segerea kukoje.
Kama mjanja angeanza kuboresha miundo mbinu ya Segerea au Ukonga maana yatakuja kuwa makazi yake ya kudumu. 90 bilioni ziende hivi hivi kijinga? Halafu unakashfu watu! Ngoja siku wale walioitwa wapumbavu wakawa ndio wenye kuangalia hatima yake na kupata majibu kwa nini majani ya mchicha ni mboga na sio ya bangi
 
Ukifuatilia muhtasari wa hii hadithi ya Bilioni 90 (87) unachukia sana....

Tulipovunja mkataba wa kandarasi yao ya ujenzi wa barabara ya Wazo Hill hadi Bagamoyo (kibabe), Stirling Civil Engineering Ltd, wakatupeleka mahakamani.>>>> (TUKASEMA HATUTISHWI)

Tarehe 10 Desemba, 2009 - Mahakama ya Usuluhishi ya Paris ikaamuru tuwalipe fidia ya hasara tuliyowasababishia kwa kiburi chetu, ya dola za Marekani milioni 25 (Takribani Shilingi Bilioni 40 wakati huo) >>>> TUKAGOMA!

Serikali yetu ikakata Rufaa, tarehe 10 Juni 2010 hukumu ya rufaa ikasomwa, tukapigwa chini. Tukaamuriwa kuilipa kampuni hiyo fedha hizo vinginevyo kila mwaka mmoja utakaohesabiwa tutalipa na riba ya asilimia 8. >>>>TUKADHARAU!

Kutokana na ucheleweshaji wa malipo, deni hilo limeongezeka hadi dola za Marekani milioni 38.7 kufikia tarehe 30 Juni, 2017. Hii ni sawa na takribani shilingi Bilioni 90 za Tanzania. >>>> TUKAENDELEA KUGOMA!

Mwezi Julai 2017, kampuni inayotudai imekamata ndege yetu, 'Bombadier Dash Q400' - sharti la kurudishiwa ndege yetu (isipigwe mnada) ni sisi kulipa hizo shilingi bilioni 90. >>>> NDIYO TUMEKUMBUKA KUWAPIGIA MAGOTI!

[Tayari Waziri Mahiga amewaomba Stirling Construction tuwalipe Bilioni 30 (kama advance payment) waachie ndege yetu wakati mazungumzo mengine ya namna ya kumalizia deni lililobaki yakiendelea. Halafu kuna watu bila aibu wanasema Lissu ndiye sababu ya ndege yetu kukamatwa. Hivi Lissu anahusikaje hapa?]

Ninajiuliza hivi akili zetu tumemgawia mwekezaji gani?

Yani tunakwenda kuwalipa watu Bilioni 90, za bure [kwa uzembe wa mtu mmoja aliyevunja mkataba kwa kukurupuka.!]

Bilioni 90 ni sawa na Magari 3,000 ya Wagonjwa (Ambulances) na yangeliweza kugawiwa kila kata ya Tanzania.

Bilioni 90 ni sawa na matrekta 1,500 ya kisasa na tungeliweza kuyagawa kwa nusu ya kata za Tanzania na kwa miaka mitano idadi ya Makumi Elfu ya wakulima wangefaidika.

Bilioni 90 ni pesa nyingi sana, mno! Lakini zinakwenda kupotea hivi hivi, na wanaoohusika na kiburi kilichopelekea hasara hii siyo tu kwamba wamekataa kujiuzulu au kuomba radhi! Bali wanatumia nguvu kubwa zaidi kutaka umma uamini kuwa wao ni "watakatifu" na "hawafanyi makosa makubwa kama haya."

Tungekuwa na watu wenye utu wangelitoka hadharani, wangekiri makosa yao, wakajiuzulu na kuomba wasishtakiwe. Kinyume chake, waliotutia hasara hii ndo wako mstari wa mbele kuwatisha waliofichua KASHFA hii.
Hii hadithi inatufundisha kwamba " KIBURI SI MAUNGWANA""...Tumlipe mzungu asepe....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna kitu apoo hiyo historia hainaa mashiko ya ainaa yoyotee tupige mdomo tuu anae mpinga Magufuri ni kibaraka wa wakoloni mamboleo ndiyo anayo yaleta lissu sasa ivii tafuta Mada nyingine haunaa takwimu za unacho semaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Samahan mkuu tusaidie takwimu ambazo mwenzako hajaziweka..

Thanx in advance.

Sent from my Nokia ya Tochi using JamiiForums Mobile app
 
Back
Top Bottom