errymars
Member
- Dec 17, 2019
- 27
- 210
Kiernan Jarryd Forbes, ‘AKA’ alizaliwa Cape Town nchini Afrika Kusini Januari 28, 1988 na alijiingiza katika anga ya muziki mwaka 2002 alipoanzisha kundi la Hip-Hop lililoitwa Entity pamoja na wasanii wenzake, Vice Versa na Greyhound.
Kutokana na ubora wa mashairi yao, waliteuliwa kuwania Tuzo ya KORA kipengele cha cha Hip-Hop Bora Afrika kabla ya kusambaratika mwaka wa 2006 na baadaye AKA aliendelea kufanya kazi kwa kujitegemea ‘solo artist’ na kutoa kwa albamu yake ya kwanza ‘Alter Ego’ mwaka wa 2011.
Albamu nyingine tatu zilifuata ikiwemo ya siku za karibuni ya 2018 iitwayo ‘Touch My Blood’ na katika maisha yake AKA alikuwa na uhusiano na mtayarishaji wa muziki Ntombezinhle Jiyane, maarufu kama DJ Zinhle mwenye umri wa miaka 39.
Walifanikiwa kumpata binti anayeitwa Kairo Olwethu Forbes mwaka 2015 na wenzi hao walitengana mwaka huohuo kabla ya kurudiana tena mwaka 2018 na kutengana tena mwaka 2019 na jambo la kusikitisha ni kwamba AKA alipata mpenzi mpya aitwaye Nelli Tembe, wakachumbiana Februari 2021 lakini Nelli alianguka kwenye kibaraza na kufariki, Aprili 2021.
Kutokana na ubora wa mashairi yao, waliteuliwa kuwania Tuzo ya KORA kipengele cha cha Hip-Hop Bora Afrika kabla ya kusambaratika mwaka wa 2006 na baadaye AKA aliendelea kufanya kazi kwa kujitegemea ‘solo artist’ na kutoa kwa albamu yake ya kwanza ‘Alter Ego’ mwaka wa 2011.
Albamu nyingine tatu zilifuata ikiwemo ya siku za karibuni ya 2018 iitwayo ‘Touch My Blood’ na katika maisha yake AKA alikuwa na uhusiano na mtayarishaji wa muziki Ntombezinhle Jiyane, maarufu kama DJ Zinhle mwenye umri wa miaka 39.
Walifanikiwa kumpata binti anayeitwa Kairo Olwethu Forbes mwaka 2015 na wenzi hao walitengana mwaka huohuo kabla ya kurudiana tena mwaka 2018 na kutengana tena mwaka 2019 na jambo la kusikitisha ni kwamba AKA alipata mpenzi mpya aitwaye Nelli Tembe, wakachumbiana Februari 2021 lakini Nelli alianguka kwenye kibaraza na kufariki, Aprili 2021.