Mzee Es,
Kwa nini umethubutu kumtukana Mkapa lakini? Yeye ni Rais mstaafu, na kwa hali hiyo sio sawa hata kidogo kumtukana.
Mzee Malecela kazi kubwa aliyofanya CCM ni kusimamia chaguzi sehemu zilizoonekana ngumu (kama kwa Cheyo). Amebobea kwenye fani ya wizi wa kura.
Mzee Malecela alishawahi kuwaambia vijana wa CCM: mwana upinzani akikupiga kofi moja, wewe mrudishie mawili. Yaani ni mhamasishaji wa mapambano ya wenyewe kwa wenyewe. Hatari sana.
Anyway, unaweza kumpenda, lakini wacha kabisa kumtukana Mkapa. Tuko wengi ambao tuna macho na tumeona na kutambua jinsi Mzee Mkapa alivyojenga uchumi wa Tanzania. Amewapiku sana Musa (Mtumishi wa Mungu) na Mzee Ruksa.
Kuhusu kijiwe kinachowafaa akina sisi, nashauri tuhamie hapa na tupajenge sisi wenyewe. Tusisubiri mtu mwingine apapashe moto.
Tunasubiri kwa shauku michango mingi na yenye faida kwa taifa toka kwako.
Augustine Moshi