Determinantor
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 61,208
- 99,957
Miezi michache Mwigulu Nchemba alijitokeza hapa jukwaani kueleze kile alichokiita ukweli wa jina lake, hongera zake maana inataka ujasiri, katika mjadala ule aliulizwa swali juu ya maoni/mtazamo wake kuhusu zoezi la ukaguzi na yeye alikiri kuwa kwa kweli maadamu watu walisoma na wengine wameshafanya kazi kwa muda mrefu sasa, ni heri ikatafutwa namna ya kuwaacha tu, nakumbuka vyema hili maana nilim-quote kumpogeza na kumchokoza kuwa anatofautiana na Boss wake.
Sasa kwa taarifa za awali nilizonazo ni kwamba kuna Mkoa mmoja ambao uhakiki wa vyeti feki umeshakamata Walimu takribani mia tano na hamsini (550) kwenye Wilaya mbili tu, nikashtuka sana, na kwamba watu hao wako makazini wengine kwa zaidi ya miaka ishirini, sio kwamba hawajaenda vyuo, Lah, wameenda vyuoni wakafundishwa, wakafaulu, wakaja wakafundisha, Wakaguzi Wa Elimu kila mwaka wanakagua maandalio ya na scheme of work na wanafaulisha. Leo hii kuja kuwaondoa hawa wote ni nani ataziba pengo lao?
Kumbuka kila siku kuna Walimu wanaokufa kwa ajali na magonjwa mbali mbali zikiwemo shida lakini pia kuna kundi kubwa tu la walimu wanaostaafu kila uchao sasa hao wote bado haitoshi kuna hili kundo ambalo linaondoshwa kazini, Watoto wetu nani atawafundisha??? Kumbe hili ongezeko la UFAULU wa Wanafuzi limechangiwa na kufundishwa na Walimu wenye vyeti feki??
Ushauri, wakati tunang'oa magugu tuwe tumeandaa mbegu za kupanda!! Vinginevyo tutakua na shamba safi lisilo na magugu wala Mbegu!!! Majanga
Sasa kwa taarifa za awali nilizonazo ni kwamba kuna Mkoa mmoja ambao uhakiki wa vyeti feki umeshakamata Walimu takribani mia tano na hamsini (550) kwenye Wilaya mbili tu, nikashtuka sana, na kwamba watu hao wako makazini wengine kwa zaidi ya miaka ishirini, sio kwamba hawajaenda vyuo, Lah, wameenda vyuoni wakafundishwa, wakafaulu, wakaja wakafundisha, Wakaguzi Wa Elimu kila mwaka wanakagua maandalio ya na scheme of work na wanafaulisha. Leo hii kuja kuwaondoa hawa wote ni nani ataziba pengo lao?
Kumbuka kila siku kuna Walimu wanaokufa kwa ajali na magonjwa mbali mbali zikiwemo shida lakini pia kuna kundi kubwa tu la walimu wanaostaafu kila uchao sasa hao wote bado haitoshi kuna hili kundo ambalo linaondoshwa kazini, Watoto wetu nani atawafundisha??? Kumbe hili ongezeko la UFAULU wa Wanafuzi limechangiwa na kufundishwa na Walimu wenye vyeti feki??
Ushauri, wakati tunang'oa magugu tuwe tumeandaa mbegu za kupanda!! Vinginevyo tutakua na shamba safi lisilo na magugu wala Mbegu!!! Majanga