Katika kuelekea uchaguzi mdogo wa jimbo la igunga unaotegemea kufanyika hivi karibuni, kumepelekea kuwepo mikakati mbalimbali inayofanywa na vyama mbalimbali vya siasa katika kuhakikisha kuwa jimbo hili linachukuliwa na kuwa chini ya chama husika.
Kutokana na hulka hiyo CCM imejikuta ikipanga mikakati mbalimbali ya kuhakikisha jimbo hili haliendi kwa wapinzani,na vyama vya upinzani vikiongozwa na CUF na CDM wakijaribu kuling'oa jimbo hili kutoka kwa chama tawala. hivi karibuni nimepata taharifa kuwa kuna mkakati wa chama cha CDM kuleta vijana mia nane (800) ili kusaidia kampeni zinazotarajia kuanza hivi punde ambapo mpaka jana vijana takribani mia tatu walikuwa tayari wameshaingia maeneo mbalimbali ya jimbo hili.
Lakini chenye kutia shaka na doa kubwa ni mkakati halisi wa utendaji kazi wa vijana hao ambao kila mmoja anapokea posho ya shilingi elfu thelasini (30,000) kwa siku, mkakati wao kwa namna nilivyopata kuufahamu kupitia baadhi ya wapasha habari hii ni kuwa haupo kidemokrasia wala hauna nia ya kufuata falsafa ya utii wa sheria na utawala bora kwani mkakati huo unajumuisha kushusha bendera za ccm wakati wa usiku,kuchochea makundi rika wakilengwa vijana katika kuhamasisha vurugu kipindi cha kampeni kwa matumizi ya mabango yenye maneno ya kashfa na matusi ambayo yanaandaliwa hivi sasa, mikakati hii na mingineyo kama hii ni doa katika igunga.
Napenda kutoa angalizo kuwa siasa si uadui wala vurugu, tutumie mikakati inayofuata utaratibu wa kisheria na demokrasia katika mchakato huu wa kutupatia wanaigunga kiongozi bora tumtakae...!
Kutokana na hulka hiyo CCM imejikuta ikipanga mikakati mbalimbali ya kuhakikisha jimbo hili haliendi kwa wapinzani,na vyama vya upinzani vikiongozwa na CUF na CDM wakijaribu kuling'oa jimbo hili kutoka kwa chama tawala. hivi karibuni nimepata taharifa kuwa kuna mkakati wa chama cha CDM kuleta vijana mia nane (800) ili kusaidia kampeni zinazotarajia kuanza hivi punde ambapo mpaka jana vijana takribani mia tatu walikuwa tayari wameshaingia maeneo mbalimbali ya jimbo hili.
Lakini chenye kutia shaka na doa kubwa ni mkakati halisi wa utendaji kazi wa vijana hao ambao kila mmoja anapokea posho ya shilingi elfu thelasini (30,000) kwa siku, mkakati wao kwa namna nilivyopata kuufahamu kupitia baadhi ya wapasha habari hii ni kuwa haupo kidemokrasia wala hauna nia ya kufuata falsafa ya utii wa sheria na utawala bora kwani mkakati huo unajumuisha kushusha bendera za ccm wakati wa usiku,kuchochea makundi rika wakilengwa vijana katika kuhamasisha vurugu kipindi cha kampeni kwa matumizi ya mabango yenye maneno ya kashfa na matusi ambayo yanaandaliwa hivi sasa, mikakati hii na mingineyo kama hii ni doa katika igunga.
Napenda kutoa angalizo kuwa siasa si uadui wala vurugu, tutumie mikakati inayofuata utaratibu wa kisheria na demokrasia katika mchakato huu wa kutupatia wanaigunga kiongozi bora tumtakae...!