Hili jambo linaudhi sana...

Hili jambo linaudhi sana...

Planett

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2014
Posts
10,561
Reaction score
16,339
Ni matumaini yangu kila mtu yuko bukheri wa afya, kama ni mgonjwa au jambo lolote linakusibu basi Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi upate kabiliana na hiyo hali.

Straight to the topic, ebwana leo nimeenda bank (atm) kutoa fedha sasa nimefika pale ndani tayari kuna mtu nikaona nisubiri hadi amalize kilichompeleka nami niingie.

Aisee nimekaa nje kama dk 20 jamaa hatoki nikaona isiwe tabu ngoja nichungulie kama kuna ugumu anapata basi nimsaidie He! ile kucheki jamaa ameshika kikaratasi kirefu (nadhani aliandika passwords) na pale kwenye top ya atm kuna cards kama 15 hivi.

Basi nikajua huyu ni mwalimu ikabidi niwe mpole tuu. Jamani nyie walimu hii tabia haifai kabisa tunapotezeana muda bila sababu za msingi.
 
Mkuu usijali sana hayo ndiyo maisha ya walimu wetu Teezee.Nauli ya kwenda kwa pamoja mjini hawakuwa nayo au ni wale wakopeshaji walikuwa wanachukua chao.Ahsante!
 
Aliyekwambia huyo ni MWALIMU ni Nani? Huyo ni mkopeshaji wa riba kubwa, hapo wadeni wamemwachia ATM Cards kwa riba ya 30%permonth na inatozwa mseleleko. Hiyo ndo hali ya watumishi wengi nchini.
Daa kumbe kuna hiki kitu tz?
 
Ndio,, ukiwa na shida ufahamu unakimbiaga wakti mwengine
Dah, lazima nikubali hii style nilikuwa sijaisikia.

Naelewa mtu anaweza kumuachia mumewe/ mkewe au mtu wa karibu katika familia card na PIN. Hii ya kumuachia mtu baki aliyekukopesha ni mpya kwangu.

Inaonesha ni jinsi gani tuna tatizo. Mishahara haiwatoshi watu kuishi maisha ya kawaida kabisa, pengine haitolewi kwa wakati.

Inatakiwa kuwe na sheria kuzuia haya. Kuwe na vikundi vya jumuiyaza wafanyakazi kupinga maisha haya.
 
Dah, lazima nikubali hii style nilikuwa sijaisikia.

Naelewa mtu anaweza kumuachia mumewe/ mkewe au mtu wa karibu katika familia card na PIN. Hii ya kumuachia mtu baki aliyekukopesha ni mpya kwangu.

Inaonesha ni jinsi gani tuna tatizo. Mishahara haiwatoshi watu kuishi maisha ya kawaida kabisa, pengine haitolewi kwa wakati.

Inatakiwa kuwe na sheria kuzuia haya. Kuwe na vikundi vya jumuiyaza wafanyakazi kupinga maisha haya.
Vyama vya wafanyakazi vipo lkn kwa usawa huu ukiweka UGOKO wao wanaweka JIWE.
 
Nimewakumbuka wagosi wa kaya ... walimu tuna hali ngumu, tutazua kitimutimu .. WALIMU
 
Sijui labda kwingine ila naowafahamu mm huwa hawaachi pin,sijapeleleza pia huwa inasaidia nn sanasana maana ukitaka unamgeuka tu
Kama ni ATM card tu si mtu anaweza kumuachia halafu anaripoti imepotea anapewa nyingine?
 
Dah, lazima nikubali hii style nilikuwa sijaisikia.

Naelewa mtu anaweza kumuachia mumewe/ mkewe au mtu wa karibu katika familia card na PIN. Hii ya kumuachia mtu baki aliyekukopesha ni mpya kwangu.

Inaonesha ni jinsi gani tuna tatizo. Mishahara haiwatoshi watu kuishi maisha ya kawaida kabisa, pengine haitolewi kwa wakati.

Inatakiwa kuwe na sheria kuzuia haya. Kuwe na vikundi vya jumuiyaza wafanyakazi kupinga maisha haya.


Kweli Mkuu,, unakuta una mshahara wa 500,000/= unakopa laki tatu kwa mtu,, dhamana inakuwa kadi ya bank, mshahara ukitoka anakata yake anakurudishia kadi yako

Maisha mengne yanaumiza sana,, basi tu
 
Sasa bila PIN card inamsaidia nini hapo kwenye ATM machine?

Anaachiwa na pin mshahara ukitoka anakata chake na riba,, inakera sana Mkuu hii kitu

Japo kuna Changamoto ya wafanyakazi wengine kutoa hela kupitia mobile money service ,,ukitoka tu anatoa yote anakuambia bado hawajaweka,, unatakiwa ujue kutime ukitoka mnawahiana kwa wale ambao siyo waaminifu,
 
Back
Top Bottom