Hili jambo limeniumiza sana

Pole sana lakini msamehe kama unashindwa jilazimishe mana ni mama yako uyo hata iweje uwezi badili hilo...
 
MI NAE ANGEKUFA KAMA ALIVOKUFA BABANGU!

mambo ya mama ni mungu wa pili asee hapana!
MAMA NI MAMA!
MUNGU NI MUNGU !
MAMA ALIUMBWA NA MUNGU KAMA ALIVONIUMBA MIMI!
kama sina maisha kwenye maisha yake,
she wont have in mine!
HIIIIIIIVYO TU YANI!
Ila inauma kweli lakini kama ukishindwa kumsamehe mama yako mzazi nani utakaeweza kumsamehe?
 
Najua umeumizwa Sana lakini yote katika yote msamehe kwakuwa ametamvua kosa lake na ameamua kuja kuomba msamaha
Imeabdikwa' ndugu yako akikosa na kurudi kwako kuomba msamaha saba Mara sabini msamehe 'kajitambua Hugo achilia uuone ukuu wa Mungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbn la kwako dogo sana ilo mkuu...!kuna kuna watu wana case kubwa kuliko hata iyo yako na wanasamehe msamehe tuu uyo mzazi wako..
 
Ila inauma kweli lakini kama ukishindwa kumsamehe mama yako mzazi nani utakaeweza kumsamehe?
MSAMAHA SIO JAMBO RAHISI!
msamaha wa ndani kabisa sio jambo jepesi!
MAMBO YA NIMEKUSAMEHE ILA SITASAHAU ni unafiki tu!
THE REAL MSAMAHA WENGI WETU HATUWEZI!
ILA MAISHA YANATAKA COMPROMISE SANA!
so badala ya kucompromise na mamangu,aseee abaki tu anaishi na yake na mi na yangu!
 
Mkuu biblia haijaacha pahala bila kusawazisha,hiyo mama ni Mungu wa dunia unayojiundia ili kusawazisha kosa inapigwa na fungu la biblia linalosema
Enyi wazazi msiwaudhi watoto wenu wasijekata tamaa,
Huyo mzazi kaudhi,tena sana,kuna aina ya wazazi hawafai kuitwa wazazi man matendo yao hayalingani na daraka la uzazi,
Nnachoweza kumshauri huyu ndugu,aache kuliwazia na kuumia huu ya hili maana hata afanye nini haibadili kitu,kwa hiyo dawa ya hili ipo ndani yake ,yaani aamue kulipikea na kutoumia na asonge mbele,
La zaidi na kubwa aitimize amri ya kusamehe,na kutoweka kisasi na kuendelea kumuheshimu mama na kumuimbea msamaha kwa Mungu maana maneno alotamka yalikuwa ni kumshika Mungu makosa au kumkosoa Mungu jambo ambalo ni kosa sana,
Samehe sahau na muone mama kwa jicho la upendo si uadui then move on,trust me ukionesha upendo kwake ni adhabu itayomtesa sana sana,
Haibadiliki ndo mzazi huyo
Tafuta gape bila papara uwe na kwako full stop,ila usikurupuke maana unaweza ongeza tatizo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi sikutendewa vizuri na baba ikapelekea kudharaulika na kutukanwa na ndugu zangu hata wakanibagua na kunitenga kabisa,nikabaki nashikamana na mama,mama alipofariki nikabaki km sina ndugu,maisha yangu ya kimaskini na nna watoto mama yao kazingua,
Unajua nilichofanya
Nilichukua watoto wangu,nikajaa ujasiri wa kuwa sina ndugu ni Mimi na vimapacha vyangu nikasonga mbele kwa hasira za kupigana na maisha,nikaondoa kinyongo na walonitenga,nikamuachia Mungu halafu nikafanya kazi sanaaaa,trust me kilichotokea kwangu ni muujiza wa kusimulia na kumshukuru Mungu,mambo viceversa,Nina kazi nimejenga,watoto walosusiwa wapo form five sasa na maisha angalau yapo murua,sasa naonekana mtu na walonipuuza wapo hoi,
Acheni Mungu aitwe Mungu,watu tunapitia magumu sana,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana dadangu, Mungu akupe nguvu ili uelewe umuhimu wa mama na kurudisha roho yako na kumsamehe na kumtendea wema sana. Sisi imani yetu inasema "Pepo ipo chini ya nyayo za mama.'' Sisi wengine mama zetu wameshatangulia mbele za haki, tunatamani wangekuwa hai kula matunda yetu sasa hivi wakati tuna uwezo lakini Mungu amewapenda zaidi ndo maana kawachukua. Hivyo basi, tuliza roho yako, jirudi, Nenda kwa mama yako, mkumbatie, mpe hugs na mwambie mama nimekusamehe na wewe ndio ufunguo wa pepo yangu, yaliyopita yamepita, nakupenda mama na nitakutunza maishani mwangu kote na ufanye hivyo kikwelikweli kwakuwa hakuna kama mama. Pole sana na utubie haraka sana kwakuwa hujui lini mamako atakufa huenda akafa kabla ya kutubia kwako na utakuja juta mbeleni pindi hali uliyonayo itakapokutoka kwakuwa huwezi kuwa hivyo maishani mwako kote.

 
Pole sana.

Unapitia wakati mgumu sana, kama kuna uwezekano nenda kakae mbali na Mama ili upunguze mawazo ila jitahidi usimchukie Mama.

Mengine mwachie Mungu.
 
Baba yangu hakunitunza kabisa hata kidogo. Alimwacha mamangu nikiwa na miezi 3 akaenda kuoa mwanamke mwingine wa kutoka kwao. Tokea hapo hakututunza sisi sote. Alizaa kule watoto watano. Yeye alifariki kabla mimi sijaanza kazi. Na baada ya kuwa very successful person still sikuwasusa wale wadogo zangu kwa makosa ya dingi na hata kama yeye angekuwepo ningemtunza pia. Nimewasomesha baadhi ya watoto wa babangu hadi university na nimewajengea nyumba kwenye kiwanja cha baba yetu kama family house ingawa mimi siitumii nimejenga kwaajili yao. Tusamehe ili tupate baraka tele za Allah, yeye anaona yaliyo dhahiri na sirini na anajua jinsi ya kulipa kwa makadirio yake, tufanye hivyo ili tupate radhi zake.
 
Pole na hongera sana na Mungu akubariki. Nataka nikushauri uwasaidie nduguzo pia japo hawakukupenda lakini napata kigugumizi kwakuwa dunia hii ni hadaa. Watoto niliosomesha hadi chuo kikuu leo hii wananitukana na kunikana na kuvunja udugu nami na mke wangu aliyewalea kuonekana mwanga na mchawi kwao. Mungu ni mwema sana.
 
Mungu ni mkuu ongera sana
 
Shukrani Sana kwa ushauri mzuri
 
Reactions: BAK
Ongera kwa moyo wa kipekee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…