Naamini Job Ndugai ni mdau hapa JF au ana mtu wake wa karibu anasoma michango hapa na kumpa notes! Mara nyingi anaonekana kufanya maamuzi huko bungeni baada ya mijadala hapa. Ni jambo zuri.
Hata hivyo bunge sasa linatakiwa kipitie tena kanuni zake na kuamua ni wakati gani msiba unagusa bunge au la? Ni pia bunge litoa mwongozo kuhusu ushiriki wa serikali kwenye misiba. Inakuwaje waziri na naibu wake wapige kambi kwenye msiba mmoja huku wizara haina mtu? Ni vigezo gani vinatumiwa na serikali kutoa rambirambi kupitia kodi ya wananchi?
Lakini la muhimu, bunge lijadili kuhusu eneo la kuzika watu mashuhuri. Lazima kuwepo na eneo maalum kwa watu ambao ni wa kitaifa.
Mkuu wakati nakubalina na wewe kuhusu mengine, nadhani hatustahili kuendelea kuzika kwenye makaburi. Tunatakiwa kuanza kuchoma miili na kuhifadhi majivu tu!