StudentTeacher
JF-Expert Member
- Jan 30, 2019
- 3,679
- 3,719
Katika mambo ambayo yanamfanya mtu aheshimike kipekee kabisa mahali popote ni uwezo wake wa kujizuia(Self-control). Kuzuia tamaa za mwili wake na kuchuja fikra zake kabla hajatamka kwa kinywa chake.
Hii ni pamoja na kujizuia kutembea na mke wa mtu,kutukana au kukashifu,Boss kutembea na wafanyakazi wake,Kudhuru mwili,kuiba,kuua,kuwa na wivu mbaya,kudhalilisha utu wa wengine na mambo mengine ya hovyo.
Kipimo cha haraka cha kujua uwezo wa mtu wa kujizuia(Self-control) ni ulimi wake. Yaani maneno yatokayo kinywani mwake hasa anapokuwa kwenye mazingira au katikati ya watu aliozoeana nao au kukasirishwa n.k!. Hii ni Kwa wote wanaume kwa wanawake!.
Ukiona mtu akikasirishwa kidogo tu anatukana au kukashifu ujue kuna walakini kwenye uwezo wake wa kujizuia(self-control).
Uwezo wa kujizuia sio jambo la asili. Kwa kawaida,miili yetu huwa inataka ipate inachotamani instantly(papo hapo). Kimsingi tamaa za mwili hazipo tayari kuzuiwa(zipo straight one way forward).
Uwezo wa kujizuia unajengwa Kwa program maalumu za kiroho na kisaikolojia.
Kufikia level ya "akupigaye shavu la kulia halafu unamgeuzia na la kushoto" sio jambo linalokuja hivi hivi tu.
Mwenye character hii ana mvuto wa kipekee sana. Mfano mzuri ni Yesu Kristo. Alikuwa na uwezo mkubwa wa kujizuia,na kuchuja nini cha kufanya na nini cha kutofanya,nini cha kusema na nini cha kutokusema. Ndio maana alikuwa anafuatwa na makundi ya watu popote anapokwenda bila mabango wala maspika ya matangazo. Watu wengi sana walivutiwa na sifa hii njema aliyokuwa nayo.
Kama kuna mtu kaoa au kaolewa na mtu mwenye self- control niseme dhahiri kwamba mtu huyo amepata raha halisi ya dunia hii. Ama hakika anakula mema ya nchi haswaaa!.
Nihitimishe kwa kusema,Self-control ni sumaku ya kuwavuta watu wema wakujie maishani mwako. Kwa sababu wanakuamini.
Mtu asiye na self-control ni hatari na anaweza kufanya Jambo lolote baya muda wowote. Mfano mzuri,huwezi kumkabidhi binti yako mbichi kabisa kwa mwalimu wa kiume ambaye unajua fika kabisa kinywa chake kimejaa maneno yenye vinasaba vya ngonongono tu,eti amfundishe bintiyo tuition. Kwa sababu unaiona hatari ya bintiyo kuharibiwa.
Maisha ni kupanga na kuchagua. Unapopanga na kuchagua jambo pia panga na chagua kubeba matokeo yake.
Naomba kuwasilisha,
Muwe na siku njema.
Sent from my 2201116TG using JamiiForums mobile app
Hii ni pamoja na kujizuia kutembea na mke wa mtu,kutukana au kukashifu,Boss kutembea na wafanyakazi wake,Kudhuru mwili,kuiba,kuua,kuwa na wivu mbaya,kudhalilisha utu wa wengine na mambo mengine ya hovyo.
Kipimo cha haraka cha kujua uwezo wa mtu wa kujizuia(Self-control) ni ulimi wake. Yaani maneno yatokayo kinywani mwake hasa anapokuwa kwenye mazingira au katikati ya watu aliozoeana nao au kukasirishwa n.k!. Hii ni Kwa wote wanaume kwa wanawake!.
Ukiona mtu akikasirishwa kidogo tu anatukana au kukashifu ujue kuna walakini kwenye uwezo wake wa kujizuia(self-control).
Uwezo wa kujizuia sio jambo la asili. Kwa kawaida,miili yetu huwa inataka ipate inachotamani instantly(papo hapo). Kimsingi tamaa za mwili hazipo tayari kuzuiwa(zipo straight one way forward).
Uwezo wa kujizuia unajengwa Kwa program maalumu za kiroho na kisaikolojia.
Kufikia level ya "akupigaye shavu la kulia halafu unamgeuzia na la kushoto" sio jambo linalokuja hivi hivi tu.
Mwenye character hii ana mvuto wa kipekee sana. Mfano mzuri ni Yesu Kristo. Alikuwa na uwezo mkubwa wa kujizuia,na kuchuja nini cha kufanya na nini cha kutofanya,nini cha kusema na nini cha kutokusema. Ndio maana alikuwa anafuatwa na makundi ya watu popote anapokwenda bila mabango wala maspika ya matangazo. Watu wengi sana walivutiwa na sifa hii njema aliyokuwa nayo.
Kama kuna mtu kaoa au kaolewa na mtu mwenye self- control niseme dhahiri kwamba mtu huyo amepata raha halisi ya dunia hii. Ama hakika anakula mema ya nchi haswaaa!.
Nihitimishe kwa kusema,Self-control ni sumaku ya kuwavuta watu wema wakujie maishani mwako. Kwa sababu wanakuamini.
Mtu asiye na self-control ni hatari na anaweza kufanya Jambo lolote baya muda wowote. Mfano mzuri,huwezi kumkabidhi binti yako mbichi kabisa kwa mwalimu wa kiume ambaye unajua fika kabisa kinywa chake kimejaa maneno yenye vinasaba vya ngonongono tu,eti amfundishe bintiyo tuition. Kwa sababu unaiona hatari ya bintiyo kuharibiwa.
Maisha ni kupanga na kuchagua. Unapopanga na kuchagua jambo pia panga na chagua kubeba matokeo yake.
Naomba kuwasilisha,
Muwe na siku njema.
Sent from my 2201116TG using JamiiForums mobile app