Mwaka 1995 wakati CCM wanapendekeza jina la mgombe urais kupitia chama chao, Hayati Baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere alialikwa katika mkutano ule kwa lengo la kusaidia upitishwaji wa jina lile. Katika hotuba yake Mwalimu aliwaonya wajumbe wa mkutano ule juu ya upitishwaji wa jina ambalo halitakuwa na sifa ya kutatua matatizo kwa watanzania yakiwamo ya rushwa,udini,ukabila na mengineyo aliyoyataja. Mwalimu alitoa picha ya hali ya siasa Tanzania kwa mwaka ule na siku za usoni hasa ndani ya CCM. Aliwaasa wajumbe wa mkutano kwa kuwaambia kwamba wakati wa kupitisha jina usiwe wa mizengwe akiwa na hofu juu ya uelewa wa mambo kwa watanzania waliowengi wakati huo 1995 na mfumo wa vyama vingi kwa chama chake.Nanukuu sehemu ya utabiri wa mwalimu juu ya kinachoendelea hivi sasa nchini mwetu,mwalimu aliwaambia wajumbe wa mkutano ule hivi: MTUTEULIE MGOMBEA ATAEKIDHI MATARAJIO YA WATANZANIA NA ANAEJUA HASWA MATATIZO YAO,WATANZANIA WANATAKA MABADILIKO,WASIPOYAONA NDANI YA CCM WATAYATAFUTA NJE YA CCM.Mwisho wa kunukuu. Ndugu zangu watanzania hakika hiki kinachoendelea hivi sasa ni kuelekea kutimia kwa utabiri wa baba wa taifa. CCM kama kawaida yao wamekuwa wakipuuza mambo mengi na hatimae sasa wanatumia nguvu kuhakikisha wanabaki madarakani,UBWANYENYE WAO NA UMANGIMEZA WAO SASA UNAWAPONZA...WATANZANIA WOTE TUTULIE TUUNGANE PAMOJA...HUU NI WAKATI WA MABADILIKO.