Hii tabia ya serikali inalitia aibu Taifa

Hii tabia ya serikali inalitia aibu Taifa

Yodoki II

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2014
Posts
5,517
Reaction score
4,008
Hii tabıa ya serıkali kukanushu taarıfa kuhusu ukwelı ulio wazı wa mambo yanayotokea kwenye jamii, ni uhunı unaofedhehesha taifa.Hii hali ınawafanya hata wananchi kutokuheshimu serikali.

Mfano,wakatı wa kuhamasisha ujenzı wa laboratorıes mashuleni,serikali iliwaagiza Wakurugenzi wa halmashauri zote kuhakikisha kila mwalimu anakatwa kiası flani cha hela toka kwenye mshahara wake kuchangia ujenzı huo.Utekelezaji ukaanza na taarifa zikaenea zaidi serikali ikilaumiwa kukata mishahara ya walimu, akaibuka Majaliwa Kassım(NW-TAM) akakanusha vikali huku akitokwa na ngita na kupoza koo kwa maji,"Hakuna mwlm atakatwa mshahara wake kwa ajili ya maabara na hakuna mkurugenzi ameamriwa kufanya hvyo"!!"Naomba tena niwatahadhalishe wakurugenzi,hakuna kukata mishahara ya walm kwa ajili ya lab"!Wakati huo zoezi linaendelea!

Juzi juzi tu shule za sekondarı nyingi kutoka halmashauri tofautitofauti zimefungwa kwa kukosa chakula.Baada ya taarifa kuenea na kuwa gumuzo mitaani,akaibuka Ghasia Hawa,"Hakuna tatizo la chakula mashuleni, na serikali inatuma fedha ya chakula kila mwezi", alitoa na takwimu."Kwanza mkuu wa shule haruhusiwi kufunga shule,na tumewaagiza wakurugenzi watuletee maelezo ni kwa nn wakuu wa shule wamezifunga shule?"

Ukweli uko wazi, Waziri anajua chakula hakuna na watu wanajua wana wakuu wa shule na walimu ni sehemu ya jamii tunakaa nao. Kauli za aina hii nyingi na zinakera.

Embu mManzania ,Piga moyo Konde, Tumia kura yako Oktoba, ondoa hawa watu madaktari.
 
Kweli kabisa, wamewafanya waTanganyika wajinga sana. Fukuza hawa watu
 
Huyu Hawa Ghasia hakustahili hata kuwa waziri; hii ndio mizigo ya DHAIFU anayoibeba mpaka mbeleko inataka kuchanika!!
 
nchi hii ni ya kizezeta sana. mtakumbuka wakati wa sherehe za CCM walimu wakuu waliandikiwa barua kuwataka wanafunzi wote waache masomo waende kwenye sherehe. pamoja kwamba barua ile iliscaniwa na kuweka humu jf, bado pinda alisimama bungeni na kukanusha hadi mishipa na mikunyanzi ikamtoka. nchi hii ni ngumu sana.
 
nchi hii ni ya kizezeta sana. mtakumbuka wakati wa sherehe za CCM walimu wakuu waliandikiwa barua kuwataka wanafunzi wote waache masomo waende kwenye sherehe. pamoja kwamba barua ile iliscaniwa na kuweka humu jf, bado pinda alisimama bungeni na kukanusha hadi mishipa na mikunyanzi ikamtoka. nchi hii ni ngumu sana.

Yaani hawa jamaa mimi nimepoteza imani nao kabısa.Mtu anakanusha jambo ambalo lıko wazi kabisa, alafu amekauka vibaya utadhani anasema kweli tupu.Mkuu gani wa shule atakubali kukaa na watoto wasio na chakula??Unaweza manage hao watoto?Si ndo wanachoma moto shule na kumwaga vinyesi ofsi za walimu?Eti jana ndo wameanza kupeleka hela kdogo ili shule zifunguliwe.
 
Hii tabıa ya serıkali kukanushu taarıfa kuhusu ukwelı ulio wazı wa mambo yanayotokea kwenye jamii, ni uhunı unaofedhehesha taifa.Hii hali ınawafanya hata wananchi kutokuheshimu serikali.

Mfano,wakatı wa kuhamasisha ujenzı wa laboratorıes mashuleni,serikali iliwaagiza Wakurugenzi wa halmashauri zote kuhakikisha kila mwalimu anakatwa kiası flani cha hela toka kwenye mshahara wake kuchangia ujenzı huo.Utekelezaji ukaanza na taarifa zikaenea zaidi serikali ikilaumiwa kukata mishahara ya walimu, akaibuka Majaliwa Kassım(NW-TAM) akakanusha vikali huku akitokwa na ngita na kupoza koo kwa maji,"Hakuna mwlm atakatwa mshahara wake kwa ajili ya maabara na hakuna mkurugenzi ameamriwa kufanya hvyo"!!"Naomba tena niwatahadhalishe wakurugenzi,hakuna kukata mishahara ya walm kwa ajili ya lab"!Wakati huo zoezi linaendelea!

Juzi juzi tu shule za sekondarı nyingi kutoka halmashauri tofautitofauti zimefungwa kwa kukosa chakula.Baada ya taarifa kuenea na kuwa gumuzo mitaani,akaibuka Ghasia Hawa,"Hakuna tatizo la chakula mashuleni, na serikali inatuma fedha ya chakula kila mwezi", alitoa na takwimu."Kwanza mkuu wa shule haruhusiwi kufunga shule,na tumewaagiza wakurugenzi watuletee maelezo ni kwa nn wakuu wa shule wamezifunga shule?"

Ukweli uko wazi, Waziri anajua chakula hakuna na watu wanajua wana wakuu wa shule na walimu ni sehemu ya jamii tunakaa nao. Kauli za aina hii nyingi na zinakera.

Embu mManzania ,Piga moyo Konde, Tumia kura yako Oktoba, ondoa hawa watu madaktari.
Easy is to judge the mistakes of others. Difficult is to recognize our own mistakes.
 
Mkuu,tunajitahidi sana na alhamdullulah,tutawatoa pamoja na kujibadilibadili.
Cha msingi tuwe makini ili kuwatambua hata wakijibadili.
Si unajua sasa wanatawi linalotumia nyota badala ya jembe na nyundo?
Yatupasa kuwa makini na imara.
 
Easy is to judge the mistakes of others. Difficult is to recognize our own mistakes.

Those aren't actual mistakes, are intentional and planned to brainfool the mass!Even if are, we must point them a fınger.Should they do the same incase ıt happens for us!
 
kwakweli hii tabia ya serikali kuwabebesha mizigo wengine halafu viongozi wa serikali wanakanusha inakera na inaumiza walio chini yao na pia sisi wananchi tunakuwa wahanga. mfano hili la shule kukosa chakula hadi kufikia kufungwa,halafu waziri anajitokeza kuamuru shule zisifungwe, hapo mwalimu mkuu unamweka kwenye wakati mgumu, atawalisha nini hao wanafunzi kama chakula hakuna? au wanadhani hao wakuu wa shule wanajitungia tu kuwa hakuna chakula mashuleni? Oktoba tuna nafasi ya kufanya maamzi ya busara zaidi
 
Back
Top Bottom