Hii tabia dada zetu mmeitoa wapi siku hizi?

Hii tabia dada zetu mmeitoa wapi siku hizi?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
63,059
Reaction score
126,648
Kilichopelekea niandike kichwa hicho cha habari ni tabia Iliyojitokeza kwa shemeji yenu Mrs. Gentamycine ambapo amekuwa na katabia kapya ambako sikajui nani kamfundisha ambapo kila anapokuwa tu safarini kikazi zaidi ya wiki moja au wiki mbili akirudi tu lazima anipime Damu.

Kujua kama eti nina maambukizi ya VVU/UKIMWI. Hali hii sasa naona inaelekea kunishinda kwani matobo ya sindano katika mikono yangu na mikononi sasa yamezidi na kila mara nasikia maumivu hadi imefika muda sasa naomba Dua kwa Mungu asiwe anapata safari za kikazi kwani najua akisafiri tu akirudi mziki ni ule ule wa kuchanjwa kunipima HIV/UKIMWI

Naombeni msaada wenu jamani nifanyeje au nimfanyeje huyu shemeji yenu.

Nawasilisha
 
na yeye anakubali kupima au anakupima mwenyewe tu? Ukiona mtu akimshuku saaana mwenzake kuwa ni mwizi ujue na yeye ana element za wizi.
 
pole kwa matatizo yako kaka.au hakuamini mpaka afanye hivyo? ila kufanya hvo ana hakiki kama hajaingiliwa na virus katika njia yake so jaribu kumuweka na kumu hakikishia kua unampenda na unamlinda muda wote,si unajua tena mwanamke akpenda anapenda kweli!
 
na yeye anakubali kupima au anakupima mwenyewe tu? Ukiona mtu akimshuku saaana mwenzake kuwa ni mwizi ujue na yeye ana element za wizi.

Mmmmmmh Hilo Nalo Neno Mkuu Ngoja Nianze Kumfanyia UDUKUZI au Kumu Edward Snowden Kwani Napata Hisia Ya Ulichokisema.
 
pole kwa matatizo yako kaka.au hakuamini mpaka afanye hivyo? ila kufanya hvo ana hakiki hajaingiliwa na virus katika njia yake so jaribu kumuweka na kumu hakikishia kuna unampenda na unamlinda muda wote,si unajua tena mwanamke akpenda anapenda kweli!

Sasa Huko Kunipenda Ndiyo Kila Siku Anidunge Misindano? au Ndiyo Ule Msemo Kuwa " AKUFUKUZAE HAKUAMBII TOKA? ". Nateseka Jamani.
 
Sasa Huko Kunipenda Ndiyo Kila Siku Anidunge Misindano? au Ndiyo Ule Msemo Kuwa " AKUFUKUZAE HAKUAMBII TOKA? ". Nateseka Jamani.

kwan ww unadhan inaweza ikawa hyo,pengine lakn sdhan kama hakupend asnge fanya hvo kama hakuna upendo mpatie elimu huyo shem atakuua brother!
 
.....Muache aendelee kukutoboa toboa maana inaonekana kila akienda safari, hicho anachokifanya yeye ndo anahisi na wewe unafanya hivyo hivyo. Ongea nae vizuri mwambie we huna haja ya kumpima ila awe anakumbuka kutumia Kondomu huko anapoenda.

Ila pole Mkuu!!.
 
.....Muache aendelee kukutoboa toboa maana inaonekana kila akienda safari, hicho anachokifanya yeye ndo anahisi na wewe unafanya hivyo hivyo. Ongea nae vizuri mwambie we huna haja ya kumpima ila awe anakumbuka kutumia Kondomu huko anapoenda.

Ila pole Mkuu!!.

Akhsante Mkuu Ila Kwa Hali Hii Itanibidi Niombe Msaada UN au Kwa Wana HUMAN RIGHTS WATCH Kwani Mwili Una Matobo Ya Kupilatowiwa.
 
Kuna sababu anaitafuta,ili ukigoma tu umekwisha.unajua sisi mabosi tunawapangia michepuko wetu safari nyingi ili tukawagegedee mbali unajua wanaume wengine wanoko sana.
 
Hivi kumbe Dna inaona virus walioingia kwenye damu kwa wiki tu tangu waingie??? btw story yako nzuri sijui inatufundisha nn?
 
Huyo dada kicheche balaaa hapo anakupima kinafki ili usjue anafanya akiwa huko semina. Na ndio maaana anapewa seminar mara kwa mara......ukiona mkeo Anapewa sana semina ushtuke kijana
 
Kuna sababu anaitafuta,ili ukigoma tu umekwisha.unajua sisi mabosi tunawapangia michepuko wetu safari nyingi ili tukawagegedee mbali unajua wanaume wengine wanoko sana.

Mkuu Unanipa Machungu. Kumbe Ni Hivi! Na Shemeji Yenu Ni Mzuri Hakuna Mfano Si Miss Chagga Wala Tyta Hakuna Anayetia Mguu.
 
Back
Top Bottom