Kwa kiswahili cha mtaani inaweza kueleweka vibaya, lakini hasa ina maana gani ndugu zetu huko Kahama?
Ukisikia aiii! ujue limempata.!Kwani hapa tatizo ni nini? Hujui kuwa neno moja lina maana tofauti katika lugha na sehemu tofauti? Nenda K'njaro uulize maana ya kinu? Hukusikia habari za mto Ngono kule Kagera? Uliwahi kusikia jamaa zetu wa Mahenge wanavyotumia neno kufira wakimaanisha kupenda na si kuharibu mtu? Wewe ungependa shule ya Ufala iitweje na kwanini? Je umetumia mantiki gani kuona ajabu kwenye jina la kawaida tu?