Hii ni "siri" nawapa ccm na mgombea wao wa nafasi ya urais Magufuli

Mr pianoman

JF-Expert Member
May 22, 2019
2,552
6,114
Kwanza niwape pole sana ccm kwa spidi mnayo pelekwa na vyama vya upinzani hasa hasa chadema na mgombea wao Tundu Lissu. Tunajua hamku tarajia kama mambo yatakuwa hivi yanavyo onekana siku chache tangu kampeni zianze kwani kwa miaka mitano yote mlikuwa mkijimwambafai wenyewe tu kwenye majukwaa na kufikia hatua ya kusema upinzani nchi umekufa ila leo sizani kama mtatamka hili neno kwani mmejionea wenyewe.

Ushauri wangu kwa CCM nawaomba kuanzia leo muache zile kampeni zenu za kujisifia eti mmejenga sijui barabara, reli, madaraja, mmenunua ndege, na mambo mengine kama hayo ambayo hayagusi maisha ya watu moja kwa moja ila yanagusa vitu.

Kwa miaka mitano yote hizi ndizo zilikuwa kampeni zenu mpaka watu wamesha zichoka kabisa na hawawezi kuwaelewa kabisa kwani ni hoja ambazo hata mimi darasa la saba nikisimama jukwaani nazipangua ipasavyo.

CCM hoja mlizo takiwa kuja nazo hivi sasa ni hoja ambazo zinagusa maisha ya watu kwa asilimia mia moja. Na mambo yenyewe ambayo watu wanataka kuyasikia kutoka kwenu ni kama
Ajira
Uhuru na haki
Huduma za afya ikiwemo bima za afya
Punguzo la kodi
Ulinzi na usalama kwa raia
Ongezeko la bei za bidhaa
Masilahi kwa watumishi wa umma
Ushirikiano mzuri wa kimataifa.
Na mengineyo mengi kama hayo ndio wananchi wanataka kusikia kutoka kwenu CCM.

Jana kwa mara ya kwanza Magufuli akiwa jukwaani anazungumzia ajira za walimu na kutangaza zinatoka muda si mrefu hivi ndivyo vitu ambavyo watu wanataka kusikia sasa na hakika mtawavutia wengi kwani hapa mmewagusa wengi japo mmegusia sekta ya elimu peke yake ila kuna sekta nyingi bado vijana wanateseka mtaani wakisubiri ajira zake.

Sekta kama afya, watu wa kilimo, uhasibu, askari wapya ambao hapa ilikuwa kila mwaka ajira za majeshi zinatoka ila katika awamu hii ya tano imekuwa tofauti kidogo kwani tumeshuhudia vijana wengi wa jkt wakirudishwa nyumbani na kuna tetesi kwamba vijana zaidi ya elfu kumi wa jkt wanaandaliwa kurudi nyumbani muda sio mrefu kwani mpaka nauli ya kurudi nyumbani wamesha saini huko makambini kwao.

Je ni kweli kwamba ajira majeshini hakuna mpaka turudishe vijana hawa wa JKT nyumbani kwa wingi namna hiyo?
Vipi kuhusu wazazi ndugu na jamaa wa hawa vijana si ndio wapiga kura wa leo mnao waomba huko mtaani na Kuwaita wanyonge sasa mbona ndio mnazidi kuwanyonga zaidi vijana wao?

CCM huu ni ushauri wangu mdogo kwenu tu mimi darasa la saba B ufanyieni kazi kwani kilicho baki ni kumwaga ajira za serikali mtaani kidogo mtaeleweka kwa vijana na watu wengine. Acheni kutuimbia hizo ngonjera zenu za KUNUNUA NA KUJENGA tumezichoka.
 
Kwanza niwape pole sana ccm kwa spidi mnayo pelekwa na vyama vya upinzani hasa hasa chadema na mgombea wao Tundu Lissu. Tunajua hamku tarajia kama mambo yatakuwa hivi yanavyo onekana siku chache tangu kampeni zianze kwani kwa miaka mitano yote mlikuwa mkijimwambafai wenyewe tu kwenye majukwaa na kufikia hatua ya kusema upinzani nchi umekufa ila leo sizani kama mtatamka hili neno kwani mmejionea wenyewe.

Ushauri wangu kwa CCM nawaomba kuanzia leo muache zile kampeni zenu za kujisifia eti mmejenga sijui barabara, reli, madaraja, mmenunua ndege, na mambo mengine kama hayo ambayo hayagusi maisha ya watu moja kwa moja ila yanagusa vitu.

Kwa miaka mitano yote hizi ndizo zilikuwa kampeni zenu mpaka watu wamesha zichoka kabisa na hawawezi kuwaelewa kabisa kwani ni hoja ambazo hata mimi darasa la saba nikisimama jukwaani nazipangua ipasavyo.

CCM hoja mlizo takiwa kuja nazo hivi sasa ni hoja ambazo zinagusa maisha ya watu kwa asilimia mia moja. Na mambo yenyewe ambayo watu wanataka kuyasikia kutoka kwenu ni kama
Ajira
Uhuru na haki
Huduma za afya ikiwemo bima za afya
Punguzo la kodi
Ulinzi na usalama kwa raia
Ongezeko la bei za bidhaa
Masilahi kwa watumishi wa umma
Ushirikiano mzuri wa kimataifa.
Na mengineyo mengi kama hayo ndio wananchi wanataka kusikia kutoka kwenu CCM.

Jana kwa mara ya kwanza Magufuli akiwa jukwaani anazungumzia ajira za walimu na kutangaza zinatoka muda si mrefu hivi ndivyo vitu ambavyo watu wanataka kusikia sasa na hakika mtawavutia wengi kwani hapa mmewagusa wengi japo mmegusia sekta ya elimu peke yake ila kuna sekta nyingi bado vijana wanateseka mtaani wakisubiri ajira zake.

Sekta kama afya, watu wa kilimo, uhasibu, askari wapya ambao hapa ilikuwa kila mwaka ajira za majeshi zinatoka ila katika awamu hii ya tano imekuwa tofauti kidogo kwani tumeshuhudia vijana wengi wa jkt wakirudishwa nyumbani na kuna tetesi kwamba vijana zaidi ya elfu kumi wa jkt wanaandaliwa kurudi nyumbani muda sio mrefu kwani mpaka nauli ya kurudi nyumbani wamesha saini huko makambini kwao.

Je ni kweli kwamba ajira majeshini hakuna mpaka turudishe vijana hawa wa JKT nyumbani kwa wingi namna hiyo?
Vipi kuhusu wazazi ndugu na jamaa wa hawa vijana si ndio wapiga kura wa leo mnao waomba huko mtaani na Kuwaita wanyonge sasa mbona ndio mnazidi kuwanyonga zaidi vijana wao?

CCM huu ni ushauri wangu mdogo kwenu tu mimi darasa la saba B ufanyieni kazi kwani kilicho baki ni kumwaga ajira za serikali mtaani kidogo mtaeleweka kwa vijana na watu wengine. Acheni kutuimbia hizo ngonjera zenu za KUNUNUA NA KUJENGA tumezichoka.
Sasa waajiri tuu hata kama hakuna uhitaji au bajeti ya mshahara?
 
Leo ni siku kama ya kumi toka kampeni zianze, kadiri kampeni zinavyoshika kasi ccm wanazidi kupanick, hapa ndio utajua kwanini Magufuli alipiga marufuku siasa ndani ya miaka mitano. Lakini kwa bahati mbaya ni kama kakilemaza chama chake. Natabiri hali ikizidi kuwa ngumu hivi, mauaji na kutekwa wapinzani yataanza kwa kasi tena.
 
Kwa hiyo Serikali iongeze mishahara iache kuwekeza Kwenye miradi itakayo kuja kuwa na tija kubwa kwa Serikali?

Hivi unajua Asilimia 60 ya bajeti yote ya serikali inakwenda kulipa mishahara ya wafanyakazi?

Sasa hapo usipowekeza kwenye miradi mikubwa Ambayo itaiwezesha Serikali kupata fedha nyingi utawezaje kulipa mishahara wafanyakazi?

Kama mishahara kwa sasa ni Asilimia 60 ya Bajeti ya serikali ukiongeza mishahara inamaana Serikali itashindwa hata kununua dawa maosptalini na kupeleka Huduma kwa wananchi umewaza hilo Au ndio ulodilofa wa chadema?
Ametamka leo Mara kule kwamba kwake yeye ni bora kujenga barabara na kununua ndege kuliko kuongeza mishahara. Kichwa Cha John anakijua mwenyewe. Siyo lazima aendelee kuwa rais lkn.
 
Leo ni siku kama ya kumi toka kampeni zianze, kadiri kampeni zinavyoshika kasi ccm wanazidi kupanick, hapa ndio utajua kwanini Magufuli alipiga marufuku siasa ndani ya miaka mitano. Lakini kwa bahati mbaya ni kama kakilemaza chama chake. Natabiri hali ikizidi kuwa ngumu hivi, mauaji na kutekwa wapinzani yataanza kwa kasi tena.
Dunia kwa sasa inatutizama kwa karibu kama vile kuku atizamapo kifaranga chake usichukulie poa
 
Kwa hiyo Serikali iongeze mishahara iache kuwekeza Kwenye miradi itakayo kuja kuwa na tija kubwa kwa Serikali?

Hivi unajua Asilimia 60 ya bajeti yote ya serikali inakwenda kulipa mishahara ya wafanyakazi?

Sasa hapo usipowekeza kwenye miradi mikubwa Ambayo itaiwezesha Serikali kupata fedha nyingi utawezaje kulipa mishahara wafanyakazi?

Kama mishahara kwa sasa ni Asilimia 60 ya Bajeti ya serikali ukiongeza mishahara inamaana Serikali itashindwa hata kununua dawa maosptalini na kupeleka Huduma kwa wananchi umewaza hilo Au ndio ulodilofa wa chadema?
Ulodilofa????

Pimbi kweli wewe,

Kwani Mkapa na Kikwete waliwezaje,huyu rais bora kuliko marais wa awamu zote ashindwe???
 
Kwa hiyo Serikali iongeze mishahara iache kuwekeza Kwenye miradi itakayo kuja kuwa na tija kubwa kwa Serikali?

Hivi unajua Asilimia 60 ya bajeti yote ya serikali inakwenda kulipa mishahara ya wafanyakazi?

Sasa hapo usipowekeza kwenye miradi mikubwa Ambayo itaiwezesha Serikali kupata fedha nyingi utawezaje kulipa mishahara wafanyakazi?

Kama mishahara kwa sasa ni Asilimia 60 ya Bajeti ya serikali ukiongeza mishahara inamaana Serikali itashindwa hata kununua dawa maosptalini na kupeleka Huduma kwa wananchi umewaza hilo Au ndio ulodilofa wa chadema?
Acha upotoshaji wewe. Tafuta bajeti zote uangalie bajeti ya mishahara halafu utafute uwiano. Hivi hukwenda hata vidudu? Buku saba vp wewe?
 
Kwa hiyo Serikali iongeze mishahara iache kuwekeza Kwenye miradi itakayo kuja kuwa na tija kubwa kwa Serikali?

Hivi unajua Asilimia 60 ya bajeti yote ya serikali inakwenda kulipa mishahara ya wafanyakazi?

Sasa hapo usipowekeza kwenye miradi mikubwa Ambayo itaiwezesha Serikali kupata fedha nyingi utawezaje kulipa mishahara wafanyakazi?

Kama mishahara kwa sasa ni Asilimia 60 ya Bajeti ya serikali ukiongeza mishahara inamaana Serikali itashindwa hata kununua dawa maosptalini na kupeleka Huduma kwa wananchi umewaza hilo Au ndio ulodilofa wa chadema?
Kwanza serikali zinazoongeza mishahara hazifanyi miradi ya maendeleo??? Acha ukilaza wako????

Miradi unayosema ndo Uwanja wa ndege wa kimataifa chato au????
 
Kwa hiyo Serikali iongeze mishahara iache kuwekeza Kwenye miradi itakayo kuja kuwa na tija kubwa kwa Serikali?

Hivi unajua Asilimia 60 ya bajeti yote ya serikali inakwenda kulipa mishahara ya wafanyakazi?

Sasa hapo usipowekeza kwenye miradi mikubwa Ambayo itaiwezesha Serikali kupata fedha nyingi utawezaje kulipa mishahara wafanyakazi?

Kama mishahara kwa sasa ni Asilimia 60 ya Bajeti ya serikali ukiongeza mishahara inamaana Serikali itashindwa hata kununua dawa maosptalini na kupeleka Huduma kwa wananchi umewaza hilo Au ndio ulodilofa wa chadema?
Basi sawa
 
Back
Top Bottom