Hii ni kweli ya Magufuli au ni safisha UKAWA na visasi?

Mkuu Swagazetu
Wengi humu hatukuelewi ulipotamka huoni kuundwa Tume kuangalia mienendo ya utendaji mkuu Serikalini. Hivi Polisi,Takukuru, usalama wa Taifa wanafanyakazi gani? Haya mambo yapo to obvious kulikuwa hakuna wa kuyakemea.
 
walewalee, watumishi wa uma walipokea zawadi za millions na kuvunja maadili ya utumishi wa uma na mmewarudisha bungeni. Umepewa takwimu makontena 349 yamepotea bila kukusanywa mapato yatakayowezesha kulipa mishahara ya wafanyakazi wa serikali huduma za jamii na maendeleo, kulipa madeni ya serikali wewe unakuja na headline kama hii...upo sawa wewe? Hapo majuzi tu vijana walikosa mikopo kuanza masomo ya vyuo au hukuwepo nchini? Unaongea vitu gani? Hebu rekebisha hiyo title ya mada yako halafu utulie ushuhudie utendaji wa kazi....eti iundwe tume! Hali mbaya kiuchumi kwasasa tunahitaji kubana matumizi.. Kama vitu viko bayana tume ya nn...
 
mtoa mada ni mpuuzi sana.watu wanachukua maamuzi unaleta siasa!! uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana
 
Rais Magufuli piga kazi. Tuanze kujifunza maadili ya kazi. Tulikuwa ovyo sana. Madudu ya wazi yanatokea halafu watu wanajichekesha chekesha tu, ovyo. Nchi gani inaendeshwA namna ile

Mwisho tukawa na nchi la ajabu ajabu lay watu wa ovyo.

Hata Waafrika tunaweza kuishi kimaadili sio kisanii sanii tu. Piga kazi Dr.

Ebooo,
 
Siku wakija sikia mtu kama kamishna yuko ndani kwa makosa kama hayo kama kakosa ndo heshima kwa kazi itarudi

Mambo ya kijinga jinga yaliyokuwa ya naendelea yalikuwa yana hatarisha usalama wa nchi. Nyoosha hao rais magufuli
 
Eti ukawa. Kwahyo alichangia mafweza mengi halafu jamaa kapigwa chini ndo anafanya madili arudishe hela yake aliyochangia?

Kama ni hivo bad timing. Tulikuwa tunashinda hapa jukwaani kuwapasha kuwa magufuli hatakuwa kama Kikwete.

Nahisi kuna watu bado hawaamini hilo. Subirin tu.
 
Tutasikia mengi ila nasubiri ifike kwa JK ndipo nianze kuamini.

Akifika kwa JK hata EDO hatasalimika usisahau hao ni "two boys" . magufuli a deal na waliopo kwenye uongozi kwa sasa akitaka kufunua ya zamani hata akipewa miaka 50 hatamaliza madudu ni mengi kuanzia escrow ,Richmond mpaka kiwira
 
Sifa unazotoa kwake (ZIWE NA KINAFIKI AU KWELI) ni baada ya kufanya hayo ikiwemo kumfukuza R.BADE ambaye bila kupindapinda ndiye amekufanya uandike...Jiulize Ameonewa?? Si kweli kupote kwa makontena hayo bila kulipiwa ushuru?? Alikuwa wapu wakati yanapotea?? Alimwajibisha nani kama kamishna mkuu baada ya kugundua?? Tatizo lenu CHAGADEMA mnaweka ukanda mbele kuliko kazi..ww na Ben Saanane alosema eti ni chuki hamtofautiani...ww umejificha kwnye ushauri uchwara lkn uko uchi kwa werevu
Mlitaka nchi apewe mzee wa kubeba asbhi na kurudisha jion ili mpige dili zenu...TUNASEMA IMETOSHA NCHI HII SIYO SHAMBA LA BIBI TENA..Mh.JPM PIGA KAZI ONDOA TAKA NA UOZO WOOTE BILA KUWATAZAMA USONI..awe wa kaskazini...kati...kusini...magharibi...ziwa au popote AKIKANYAGA KATIBA (WIZI NA UBADHIRIFU ) FUKUZA..WZALENDO NI WENGI..Na ss tujisikie raha hata tukiwa nchi zingine kuwa tuna nchi ya uadilifu..Take care

Makontena ynaweza kuwa vifaa vya ccm vya uchaguzi hahaaa!
 
hivi unafikir kontena 300 Jk hausiki hapo?

Anahusika kwa sababu ya wingi wa kontena au kwa kuwa anahusik kwa uzembe au ufhifu It does not make sense!
Kama kuna mtu anaweza kunisaidia hili naomba anipe usahihi. JPM alizuru ofisi ya PM jana, leo PM -( hawavumi lakini wamo) akatinga bandarini akaibuka na issue, jioni mtu akatemwa na Dr Mapngo akapew kazi! Haya ni maigizo kama ya muhimbili? sijui yataisha lini.
 
Magufuli mwenyewe tu anajua madudu yote ya nchi hii

hukumsikia wakati wa kampeni nini
 
Unadhani mh Magufuli ameweka makalio ofisini na kusubiri aletewe taarifa? Hujui kama leo mh waziri mkuu alikua bandarini???
Na kakuta uchafu ulio tukuka?

Uchafu hauwezi kutukuka. Ni matumizi mabaya ya lugha. Tusiwafundishe watoto/vijana lugha mbovu.
 
Kamishna kahojiwa na Waziri Mkuu,kuhusu orodha akasema hapo alipo hana labda aipate kwa wasaidizi wake,Waziri Mkuu akamuonesha orodha akakiri ni yenyewe.Akaulizwa mmefanya nini,anasema tunaendelea kufuatilia maana hawajajua ni akina nani wameiba hizo contena.Sasa hii bla bla ni ya nini.Unajua public interest is the interest of the government of the day.Sehemu potential kama TRA huwezi fanya mchezo,huo ni moyo wa nchi.Hayo mambo ya michakato badae,Kmaishna amesimamishwa hajafukuzwa kazi na amaendelea kupata haki zake kama mgfanyakazi mpaka hapo uchunguzi utakapokamilika.Tufikie hatua tuwe serious jamani.

swa kabisa. Nakuunga mkono
 
mwacheni rais afanye kazi.

tume za nini?

Magufuli anafanya ambayo UKAWA tuliyataka.sasa lazima tumpongeze
 
Back
Top Bottom