Hii ndo michepuko ya ndoa...

Hii ndo michepuko ya ndoa...

Kasie

Platinum Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
22,801
Reaction score
43,177
Habari zenu wanandoa wote wa MMU,

Michepuko katika ndoa ni noma, kaa katika mstari wa ndoa yako, baadhi ya michepuko yenyewe inatokea hivi;

Funguo ambae ni mume wa Kufuli yuko nyumbani kwake na mkewe, funguo akiwa anaoga bafuni kufuli anamuaga mumewe kuwa anatoka na gari maramoja kuwahi sokoni na atarudi muda si mrefu. Mara kufuli anarudi ndani na kumwambia mumewe gari imekataa kuwaka naomba namba ya simu ya fundi gari nimpigie aje atengeneze maramoja niwahi sokoni. Mumewe huku akiwa bafuni anamjibu mkewe, nakuja namba ziko kwenye simu (bila mkewe kusikia vizuri anajiambia aah simu yake si hii hapa wacha niangalie namba nimpigie fundi aje kuliko amnsubiri hadi mumewe atoke bafuni) Kiroho safi anaenda kwenye inbox ya simu ya mumewe na kuanza kutafuta fundi, anaanza kusoma..... fundi ujenzi, fundi mashine, fundi nguo, fundi gari.. aahaaa hii hapa (kufuli anajiambia mwenyewe na kupiga simu) Simu inaita na inapokelewa na mschana anayeanza kuongea kimahaba kwa sauti iliyolegea (hallo mpenz, mambo nafurahi umenipigia nasikia raha sana hasa kwa kuninunulia simu ya touch screen na tv flat screen, nakupenda sana mpenz) Kufuli akashindwa kuvumilia kusikiliza na kuhamaki wewe ndo fundi gari?? wewe ni nani? looh!! yule mschana nae anahamaki na kupayuka mama yangu kisha anakata simu. Zogo linalozuka baada ya hapo wanalimaliza wanandoa wenyewe.

Kufuli jumapili hii kamuaga mumewe anaenda kwenye kichen party kisha huyo anaishia anakokujua, kufika mida ya saa tatu usiku mumewe anaamua kumpigia mkewe na simu inaita tuu haipokelewi, mara anaamua kumpigia shosti wa mkewe ambae alimwambia wataenda wote kwenye kichen party. Shosti ake Kufuli anapokea simu (akiwa nyumbani kwake) anapokea simu na kumsalimia shemeji yake vizuri kisha anaulizwa vipi huko kwenye kichen party mnatoka saa ngapi? maana saa tatu saa hizi na nampigia kufuli simu hapokei mwambie arudi si lazima akae hadi mwisho. Shosti mtu bila kufikiri anauliza kichen party? kichen party gani? Anapopata maelezo kutoka kwe shemejie (akili inamjia sasa bi shosti aue soo la kufuli kwa mumewe na kujibalaguza) aaah shemeji ni kweli tuko hapa kwenye kichan party ya rafiki yetu eeheheeee huku anakigugumizi na kujichekesha, mara inasikika sauti ya mtoto wa bishosti akiita mama nataka kulala chumbani kwako leo...... funguo anaghafirika na kujua tayari kaibiwa huku na huku nae bishosti anakata simu na kuacha zogo limalizwe na wanandoa wenyewe.

Japo michepuko siku hizi iko mingi sana, ya aina nyingi nyingi na ni hatari kwa ndoa, mwanadoa tulizana na mkeo/mumeo, maranyingi mmoja anapochepuka hutumia kinga kwa mara4 hadi 5 za mwanzo baadae hujenga uaminifu na kuanza kuchubwika kavu kavu ambapo ndo maambukizi hutokea, JILINDE, MLINDE NA MWENZIO ACHA MICHEPUKO.

Kama ulishawahi kukutana na habari hii basi mtaarifu ambae hajaijua na ndo mara ya kwanza pata habari na chukua tahadhari.
Kama unamchepuko uache maramoja na kama huna usijaribu kuchepuka.
 
Kuchanika kwa jamvi si mwisho wa maongezi. Mradi asirudi na miwaya na asinipitishie usoni tu, acha awachape nao huko anipunguzie shughuli ya usiku.

Kulinganisha na tamaduni zetu hizi za mitala na mafiga matatu, uaminifu bado tuna njia ndefu sana, until the cow comes home.
 
Kuchanika kwa jamvi si mwisho wa maongezi. Mradi asirudi na miwaya na asinipitishie usoni tu, acha awachape nao huko anipunguzie shughuli ya usiku.

Kulinganisha na tamaduni zetu hizi za mitala na mafiga matatu, uaminifu bado tuna njia ndefu sana, until the cow comes home.

Duuuh kwa hiyo wewe unaikubali michepuko sio? aiseee!! hatari lakini salama. Mie kila nikifikiria kuishi kwa matumaini nasikia ki.si.mi kimesinyaaaaaa japo siku hizi hakuna kukonda na kutoka madonda ila mmmhhh nikifikiri tuu nakosa pozi la kuachama miguu.
 
Mh yangu macho maana siku hzi tumebakia kupewa taarifa tu,hakuna kuomba ruhusa wala nini,mungu na atuepushe na haya yooote!
 
Kasinde
===> hapa ni kumuomba mungu tu,nafikiri ukiamini kila kitu kinawezekana maana ngono/mapenzi hayana makombo!
 
Last edited by a moderator:
Message sent, mi kwa uelewa wangu kama wana ndoa tutakuwa na hofu ya Mungu tutashinda michepuko, bila hofu ya Mungu ni ngumu kushinda
 
Message sent, mi kwa uelewa wangu kama wana ndoa tutakuwa na hofu ya Mungu tutashinda michepuko, bila hofu ya Mungu ni ngumu kushinda

ni kweli usemamcho hali inatisha, hizi ARV's zisingekuwepo watu wangekuwa na hofu ila kwa sababu sikuhizi watu wanakuwa safii kama nyororo na wakaka wanaweka siksi paki kumbe tayari kaukwaa. Michepuko ni majanga, kwa wanaozipenda familia zao wanatulia hawachepuki.
 
Kasinde
===> hapa ni kumuomba mungu tu,nafikiri ukiamini kila kitu kinawezekana maana ngono/mapenzi hayana makombo!

sala ni muhimu hasa kwa watoto wanaozaliwa siku hizi mioyo ya watu imebadilika, si wanawake si wanaume si wazee wala si vijana wote wanakwenda mutasamutasa, penye watu 10 binadamu ni mmoja.
 
Mh yangu macho maana siku hzi tumebakia kupewa taarifa tu,hakuna kuomba ruhusa wala nini,mungu na atuepushe na haya yooote!

Tatizo watu wanaingia kwenye ndoa wote wakiwa sugu, hawajali tena ni kujijali wenyewe na kusema wanakula bata hadi kuku aone wivu kumbe wanajimaliza. Mungu aepushe kwa kweli.
 
ni kweli usemamcho hali inatisha, hizi ARV's zisingekuwepo watu wangekuwa na hofu ila kwa sababu sikuhizi watu wanakuwa safii kama nyororo na wakaka wanaweka siksi paki kumbe tayari kaukwaa. Michepuko ni majanga, kwa wanaozipenda familia zao wanatulia hawachepuki.

Mwenzangu! acha tu Mungu atusaidie maana wewe kama wewe unaweza jitunza vp mwenzio?????
 
Tatizo watu wanaingia kwenye ndoa wote wakiwa sugu, hawajali tena ni kujijali wenyewe na kusema wanakula bata hadi kuku aone wivu kumbe wanajimaliza. Mungu aepushe kwa kweli.

huu usugu ni upi unaouongelea??
 
huu usugu ni upi unaouongelea??

kwamba kwenye ndoa wanaume wanacheat na mwanaume nae anaingia kwenye ndoa akiwa na mawazo kuwa mkewe anaweza kuibiwa na mabwana wengine pale anaposema anaenda kazini au saluni au kichen party ndo huo usugu wa mawazo yanayowapelekea wanandoa hao kuchepuka nje.
 
kwamba kwenye ndoa wanaume wanacheat na mwanaume nae anaingia kwenye ndoa akiwa na mawazo kuwa mkewe anaweza kuibiwa na mabwana wengine pale anaposema anaenda kazini au saluni au kichen party ndo huo usugu wa mawazo yanayowapelekea wanandoa hao kuchepuka nje.
unamaanisha kulipiza kisasi
 
Sometimes unawaza unaona bora usioe..ila upweke unakuwa kikwazo, na maadili, watoto wazaliwe katika ndoa kama wewe ulivyozaliwa na kulelewa kwenye familia moja yenye baba mmoja na mama mmoja!

A big challenge..Lord help us!
 
kwamba kwenye ndoa wanaume wanacheat na mwanaume nae anaingia kwenye ndoa akiwa na mawazo kuwa mkewe anaweza kuibiwa na mabwana wengine pale anaposema anaenda kazini au saluni au kichen party ndo huo usugu wa mawazo yanayowapelekea wanandoa hao kuchepuka nje.

Kamwe usijenge dhana kwamba kwa kuwa mwenzako anatoka nje ya ndoa na wewe utoke...huko ni kujipalia makaa kichwani. Mungu alimpa kila mtu roho yake na siku ya hukumu kila mtu atahukumiwa kwa matendo yake mwenyewe. Mwenzako akichepuka piga magoti endelea kumuita Mungu...hakika ataitika
 
Back
Top Bottom