Hii ndio Silaha Kuu ya CHADEMA!.

Hii ndio Silaha Kuu ya CHADEMA!.

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,198
Reaction score
7,536
Kimsingi mshikamano na ushirikiano wa hali ya juu "Team work" ndio nguzo muhimu zaidi ya zote kwa taasisi yeyote ile au watu wenye lengo moja na wanao pambana kuliendea lengo hilo.Ni kwa mshikamano na ushirikiano tu, watu wanaweza kulinyanyua jiwe kubwa ambalo kimsingi kama akijaribu kunyanyua mtu mmoja mmoja (mmoja baaada ya mwengine), wote wataishia kutenguka migongo na jiwe li pale pale.Ni kwa ushirikiano na mshikamano tu; Nyuki wanaweza kutengeneza asali ya kuwatosha kwa matumizi yao na nyingine nyingi ya ziada kwa matumizi ya viumbe wengine.

Hata hivyo ni lazima umoja na mshikamano huo utawaliwe na dhamira njema, upendo , njia na maono sahihi juu ya kule wanakotaka kwenda, kinyume chake itakuwa ngumu kufanikiwa.
 
Asante sana Mkuu kwa uchambuzi mwanana , labda niongezee tu tena kidogo sana kwamba kwa ushirikiano huu na kwa mshikamano huu wa CDM , basi njia yao ya kuingia Ikulu ni nyeupe kabisa.
 
Jambo la muhimu zaidi ni CHADEMA kujipambanua kwamba kiko kwa malsahi ya wana nchi kuhakikisha rasilimali za nchi hii kwanza nikwamanufaa ya wananchi, na kama ndiyo hivyo basi ili Chama hiki kiweze kufanikiwa kupambana na propaganda za chama tawala kinabidi kupata sapoti kubwa kutoka kwa wanachiwenye mapenzi mema na nchi hii. kwani iwe chama tawala au cha upinzani bila wananchi kukisapoti hakifiki popote.
Kwa jinsi ilivyo basi wananchi tunajukumu kubwa sana la kutoa sapoti kwa chama ili kiweze kufikia malengo
 
Ni kweli, inawapasa kushikama zaidi kadri siku ziendevyo, ili kuweza kufikia lengo.
 
Hivi CHADEMA ndiyo wameishawishi serikali ya CCM suala la katiba?
 
kwani iwe chama tawala au cha upinzani bila wananchi kukisapoti hakifiki popote.
Kwa jinsi ilivyo basi wananchi tunajukumu kubwa sana la kutoa sapoti kwa chama ili kiweze kufikia malengo
Mkuu uko sawa ila wakati mwengine wananchi wanataka kusapoti chama fulani kulingana na mwelekeo wake , ila kama ni chama cha upinzani wanaogopa kukisapoti wazi wazi kwa kuogopa kuhujumiwa.Unakuta mtu labda ni mjasiriamali; halafu akionekana anaunga mkono upinzani wanamuambia "ngoja utaona!" halafu wanaweza kumuhujumu (kumfilisi n.k.) Njia nyingine ni hii ya kuwabambika watu kesi.Sasa hali hii huwaogopesha wananchi wengi kutofautiana na chama tawala.Lakini chama chenyewe kinapoonesha mshikamano na ushirikiano, woga wa kuhujumiwa hupungua hata kwa wananchi wa kawaida wanaotaka kukiunga mkono chama kwa kuwa wanajua msaada utakapohitajika, basi, utapatikana.
 
Mkuu Betlehem hayo uliyoyasema ndiyo yaliyokufanya wewe kuhamia cdm? maana hatujasahau makovo uliyoyasababisha kipindi cha nyuma?


Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu na hii ndiyo ilikuwa nguzo kuu ya Tanu kipindi cha ukoloni na sasa nguzo hii iko cdn na sio ccm tena.......
 
Mkuu Betlehem,

Thanx for your nice analysis; ni kweli "Umoja ni nguvu na utengano ni Udhaifu"
Magambaz wanatumia kila mbinu ili watutenge, lakini wameshindwa kwa jina la YESU.
 
Hivi Chadema ndiyo wameishawishi serikali ya CCM suala la katiba?
CHADEMA haijaishawishi ila JK mwenyekiti wa CCM aliiteka nyara kwa kimbelembele chake. Shukrani kubwa kwa JK maana ilikuwa ni ilani ya uchaguzi na ameitekeleza vizuri so far.
 
Baada ya dhiki faraja, ilikuweza kujikomboa lazima kuna kuumia sana na kusdhalilika. Kwani hata mafisadi wasipenda kuona wanaondolewa katika nafasi hizo. Hivyo ukombozi ni vita kubwa tu, lakini nakubaliana na wewe Viongozi wakionesha umoja wa shati basi inakuwa ni picha ya muongozo mzuri kwa wananchi
 
Hivi Chadema ndiyo wameishawishi serikali ya CCM suala la katiba?

Si bora hata wangeishawishi , CHADEMA wameiburuza ( wameilazimisha ) serikali ya CCM kuingia kwenye mchakato wa katiba !
 
Hivi Chadema ndiyo wameishawishi serikali ya CCM suala la katiba?

Wimbo wa katiba mpya haukuanza jana Mkuu. Wimbo huo umeanza hata Kabla CHADEMA haijazaliwa. Ukitaka kujua muziki huu ulianza lini muulize Mchungaji Mtikila na kesi yake ya Mgombea Binafsi pale Mahakama kuu ndo utajua Wimbo wa Katiba Mpya umeanza lini. Au mtafute Njelu Kasaka na washirika wake Kina Dr. Ngunangwa na kundi lao lililoitwa G55 wakati wa utawala wa Mwinyi. Hii katiba mpya ni tukio kujibu kilio kina zaidi ya miaka 20.
 
Ushawishi mkubwa wa katiba mpya ni msukumo mkubwa wawananchi na si swala la JK na serikali yake, kama unaweza kukumbuka majibu ya Kombani na mwanasheria mkuu wa serikali. kwamba watu wanaongea kama Bata. lakini leo wao ndiyo wamekuwa kama wamepoteza muelekeo
 
Mkuu uko sawa ila wakati mwengine wananchi wanataka kusapoti chama fulani kulingana na mwelekeo wake , ila kama ni chama cha upinzani wanaogopa kukisapoti wazi wazi kwa kuogopa kuhujumiwa.Unakuta mtu labda ni mjasiriamali; halafu akionekana anaunga mkono upinzani wanamuambia "ngoja utaona!" halafu wanaweza kumuhujumu (kumfilisi n.k.) Njia nyingine ni hii ya kuwabambika watu kesi.Sasa hali hii huwaogopesha wananchi wengi kutofautiana na chama tawala.Lakini chama chenyewe kinapoonesha mshikamano na ushirikiano, woga wa kuhujumiwa hupungua hata kwa wananchi wa kawaida wanaotaka kukiunga mkono chama kwa kuwa wanajua msaada utakapohitajika, basi, utapatikana.

Dah ! Mkuu betlehem asante sana , maelezo yako yananifanya nijisikie huru sana kusupport cdm , Ninakunywa chai kavu lakini najihisi kama nina maandazi mengi sana !
 
Hivi Chadema ndiyo wameishawishi serikali ya CCM suala la katiba?
Imendikwa na Elias Msuya na Freddy Azzah.12April 2011.(Vijana Forum)
Wanasiasa wapinga muswada wa kurekebisha katiba


WAKATI serikali ikijiandaa kuwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Katiba bungeni wiki ijayo, wanasiasa na wasomi wameupinga wakisema utawa bana wananchi.Hata hivyo, wawakilishi wa CCM na UDP walionja joto la jiwe na kulazimika kukatisha hotuba zao, baada ya kuzomewa na washiriki wa Kongamano la kujadili Muswada wa Marekebisho ya Katiba lililofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam jana.

Mwakilishi CCM azomewa
Hata hivyo, hali ya hewa katika kongamano hilo ilichafuka baada ya Mwakilishi wa CCM, Prince Bagenda kupanda jukwaani na kuanza kutoa maoni ya chama chake ambapo washiriki wa kongamano hilo walianza kumzomea kila alipoendelea kuzungumza.Bagenda alikiri kwamba hoja ya Katiba haikuwa ya CCM, lakini akasema CCM ilikubali kwa kuwa Serikali huongozwa kwa maoni ya wananchi. Hata hivyo, Bagenda aliwakera watu aliposema suala la katiba haliji hivi hivi tu, bali wananchi wanapaswa kudai. "Msifikiri kila kitu mnapewa tu, lazima mdai," alisema Bagenda huku akizomewa na washiriki wa kongamano hilo. Baadaye alishindwa kuendelea kutokana na kuzomewa licha ya Msimamizi wa kongamano hilo, Dk Kitila Mkumbo, kujaribu kuwatuliza watu bila mafanikio.

.Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ambaye alishiriki katika kongamano hilo, alisema chama chake hakioni nia njema ya serikali katika kuunda katiba mpya, hivyo wataipinga bungeni na nje ya bunge. Chama hicho kimeapa kutumia maandamano kwa kile wanachokiita nguvu ya umma kuupinga muswada huo kama utapitishwa na Bunge kuwa sheria.

Ritz ; una swali jengine?

 
Kimsingi mshikamano na ushirikiano wa hali ya juu "Team work" ndio nguzo muhimu zaidi ya zote kwa taasisi yeyote ile au watu wenye lengo moja na wanao pambana kuliendea lengo hilo.Ni kwa mshikamano na ushirikiano tu, watu wanaweza kulinyanyua jiwe kubwa ambalo kimsingi kama akijaribu kunyanyua mtu mmoja mmoja (mmoja baaada ya mwengine), wote wataishia kutenguka migongo na jiwe li pale pale.Ni kwa ushirikiano na mshikamano tu; Nyuki wanaweza kutengeneza asali ya kuwatosha kwa matumizi yao na nyingine nyingi ya ziada kwa matumizi ya viumbe wengine.

Mwaka 2010, CHADEMA , walishikamana na kushirikiana kweli kweli katika uchaguzi mkuu, hatimae matunda ya kazi yao yalionekana.Walifanikiwa kupata viti vingi vya ubunge kwa kiwango ambacho hakikutarajiwa.


Wabunge wa CHADEMA walishikamana ndani ya Bunge na Kuweza kuiwajibisha serikali vilivyo bungeni.Mara ya kwanza ni kipindi walivyomshinikiza Waziri mkuu El Kujiuzulu na mawaziri wengine wawili, na mara ya pili; Ni mwaka 2012 walivyoishinikiza serikali hata Rais akawajibika kupanga upya baraza la mawaziri.

CHADEMA, Kwa ushirikiano mkubwa wameendensha M4C ambayo imeonekana kuwa na mafanikio makubwa.Miongoni mwa mafanikio hayo ni kuwafanya wananchi kujitambua na hata sasa unaona CCM nayo imeenza kuzunguka hadi katika vitongoji kuwafikia wananchi (Ni jambo zuri mno) kwa kuwa washajua kuwa sasa wananchi wanajitambua sana kutokana na elimu waliyoipata kama matunda ya M4c.


Kwa kuwa CCM, wametambua silaha hii ya Mshikamano na ushirikiano ambayo imekuwa inawasaidia CHADEMA;basi wameamua kufanya kila mbinu ili kuvuruga ushirikiano na mshikamano huo.Wamekuwa wakitengeneza mizengwe kwa kuweka mapandikizi ndani ya CHADEMA, kama akina Mtela Mwampamba na timu yake .Hata hivyo kwa kutumia silaha hii hii ya Ushirikiano na mshikamano; CHADEMA wamefanikiwa kuvuka hiki kihunzi.


Kwa mshikamano wa CHADEMA, wameweza kuweka wanasheria wa kuwasimamia wanachama na viongozi wao wanaohujumiwa kisiasa na kesi zote wameonekana kuzisimamia vyema.Rejea kesi ya Lema Arusha, Kesi ya Rwakatare, Kuna yule jamaa wa Kilolo aliesweka ndani Kwa kumrekodi mkuu wa wilaya, Kuna kiongozi wa Chadema, Mtwara alikamatwa kwa kuhusiswa na vurugu za gesi na wakati hakuwepo mtwara na kesi nyengine nyingi.


CHADEMA kwa ushirikiano wao na mshikamano wao; Wameishawishi serikali ya CCM kukubali mchakato wa katiba mpya; mchakato ambao hapo awali ulipingwa na CCM.Ni kwa mshikamano na ushirikiano CHADEMA wamefanya tena vizuri na sasa mchakato unaendelea.

Hii ni mifano michache tu katika mingi.Kwa hakika Mshikamano na Ushirikiano, ni silaha imara kuliko mkuki wa chuma cha pua.Hii ndio silaha ya CHADEMA iliyowafikisha hapa walipo.Hii ndio silaha itakayo wapeleka CHADEMA hatua nyengine mbele.Maadui wa CHADEMA wataweka nguvu nyingi kuhakikisha wanaiharibu silaha hii kwa ajili ya usalama wao.Ni vyema CHADEMA wakawa na tahadhari ya ziada kuilinda silaha hii.

Hakika 100 % hata yule mpenda pembe za ndovu hilo hana uwezo wa kulipinga hilo
 
Uzuri wa CHADEMA ni viongozi wasioteteleka, wana vision na wanajuwa nini wanachokipigania. Vyama vingine ni kwa ajili ya kuganga njaa. Vinaibuka kipindi cha uchaguzi kisha mwisho wa siku kinatangaza kujitoa na kura zake wapewe magamba! CCm wanahaha huku na kule kuwafungulia kesi zisizokuwa na kichwa wala miguu viongozi wa CDM ili washindwe kutekeleza majukumu yao-Lakini kwa sababu CDM ina Mungu, mwisho wa siku mafisadi wana aibika! Peooopleeeees Poooweeeeer!
 
Pia la kuongeza ni kwamba CHADEMA wamekuwa wakifanya tafiti na kusema ukweli kwa kila jambo wanalolileta mbele ya wananchi au hata bungeni,ndo maana serikali na CCM imeshindwa namna ya kuwashitaki.CHADEMA imeweza kuwapa wananchi tumaini jipya la kupata haki na utawala wa sheria.Keep up viongozi wa CHADEMA,may GOD bless u all!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!:car:
 
Back
Top Bottom