Hii ndio "Lack of Coordination" ambayo Katibu Mkuu Kiongozi alikuwa anaizungumzia?

Itoye

JF-Expert Member
Sep 29, 2017
531
1,024
Kheri ya Pasaka.

Hili sakata la Boss wa TPDC limeacha maswali mengi sana ambayo binafsi natamani Mh. Rais alitolee ufafanuzi ili kujenga imani juu ya mfumo wa mipango na maamuzi unaomsaidia katika kutekeleza majukumu yake?

- Sababu zipi alipewa hadi akaridhia kumtengua Boss aliyekuwa akihudumu?

- Kama aliziona zina mashiko na ni nzito, Je! Alijipa muda kujiridhisha juu ya ukweli wake? Je sababu hizo zimepoteza mashiko ndani ya muda usiozidi masaa 24? Au kama bado alikuwa hajajiridhisha kulikua na uharaka gani wa kutoa tangazo lile?

- Jambo hili limewezekana ku - "Undo" lakini naamini kwa muhusika kuna namna limemuathiri, Je! Lingekua ni jambo ambalo madhara yake huwezi kuyabadili au kuyafuta kwa urahisi au ambalo madhara yake ni ya kudumu wangekua tayari kuwajibika? Kama ni ndio basi hata ktk hili natamani kuona watu wakiwajibishwa.

Au tukio hili ndio linadhihirisha ukubwa wa tatizo la kukosekana kwa "network and coordination of information" kama Katibu Mkuu kiongozi alivyosema na Mh. Rais akakazia? Kama hivyo ndivyo basi tuna tatizo kubwa mbele yetu.

RIP JPM.
 
Kukosekana kwa umakini serikalini kunakosababishwa na kukosekana kwa muunganiko (coordination) wa michakato na taarifa ni kifo cha utawala wowote.

Umeuliza swali moja muhimu na sijui kama wasomaji wengine wameona pia, kwamba;

Hivi kwa uzembe (reckless) ya namna hii yangekuwa ni maamuzi ya kugharimu uhai wa mtu, wangeweza kumrudisha duniani mtu huyu kama angekufa?

Hata sasa kwa uzembe na kukosa umakini wa taasisi zinazohusika, zimekwisha haribu reputation ya mtu huyu aliyeteuliwa asubuhi na dunia yote kutangaziwa halafu jioni wanafuta tena kwa mtindo uleule...!!

Hii si sawa kabisa kwa serikali yenye coordination na inayoongozwa na watu wenye akili na maarifa ya kutosha...!!
 
A rest in peace JPM ili iweje?
Ateseke motoni huko, na mwili wake ufukuliwe tuutandike viboko ishirini na Moja kwa madhara ya ukabila, ukanda na mauaji na kudumaza maendeleo ya watu alio tuachia.
Kwenda zako JPM
Mnaojifanya wazalendo wa nchi hii,........

haya nchi mmebakinayo,,,,,,,,,

Tunawaombea
 
A rest in peace JPM ili iweje?
Ateseke motoni huko, na mwili wake ufukuliwe tuutandike viboko ishirini na Moja kwa madhara ya ukabila, ukanda na mauaji na kudumaza maendeleo ya watu alio tuachia.
Kwenda zako JPM
Usipo tubu laana hii itakutafuna wewe na kizazi chako cha kwanza na cha nne..kuwadi na kibaraka wew utakufu kifo kibaya sana tubu
 
Back
Top Bottom