Hii naomba iwafikie bodi ya mikopo(HESLB)

Hii naomba iwafikie bodi ya mikopo(HESLB)

ElimuMdau

New Member
Joined
Nov 16, 2016
Posts
1
Reaction score
3
Naandika makala hii kuelezea kilio chetu kwa wanafunzi tuliokosa mikopo hususan chuo cha Dar es Salaam Maritime Instutute (DMI). Taasisi hii ambayo inatoa kozi ya Bachelor in Marine Engineering and Bachelor in Marine Transportation, katika mwaka huu imepokea jumla ya wanafunzi 70. Cha kusikitisha katika wanafunzi hao 70 ni wanafunzi wawili tu ndio wamepatiwa loan allocation na bodi ya mkopo na ndio majina yao yamefika chuo.

Swali la kujiuliza, jee ni kweli wanafunzi wawili tu katika chuo kizima ndio wenye sifa? Je, wanafunzi wengine wote waliobaki wakishindwa kujisomesha maana yake ni kwamba kwa mwaka huu DMI itashindwa kusomesha wanafunzi wapya?Malecturer waliokuwepo kusomesha wanafunzi wa Bachelor kwa mwaka huu watakua na kazi gani?

Ushauri:

Naomba bodi ya mikopo ifikirie upya na kwa umakini je hii ni haki chuo kizima kwa mwaka huu kuwapa mikopo wanafunzi wawili tu? Tunaomba bodi ya mikopo, viongozi wa serikali na wadau wa elimu watusaidie kututatulia tatizo hili. Wengi wetu ni maskini na hatuna uwezo wa kujisomesha bila ya mkopo.

Ahsanteni naomba kuwasilisha!
 
Kweli elimu ya bongo hapana, tujiweke wazi tu kuwa Tanzania hatuhitaji tena wasomi hapa kilimo kwanza.
 
Naandika makala hii kuelezea kilio chetu kwa wanafunzi tuliokosa mikopo hususan chuo cha Dar es Salaam Maritime Instutute (DMI). Taasisi hii ambayo inatoa kozi ya Bachelor in Marine Engineering and Bachelor in Marine Transportation, katika mwaka huu imepokea jumla ya wanafunzi 70. Cha kusikitisha katika wanafunzi hao 70 ni wanafunzi wawili tu ndio wamepatiwa loan allocation na bodi ya mkopo na ndio majina yao yamefika chuo.

Swali la kujiuliza, jee ni kweli wanafunzi wawili tu katika chuo kizima ndio wenye sifa? Je, wanafunzi wengine wote waliobaki wakishindwa kujisomesha maana yake ni kwamba kwa mwaka huu DMI itashindwa kusomesha wanafunzi wapya?Malecturer waliokuwepo kusomesha wanafunzi wa Bachelor kwa mwaka huu watakua na kazi gani?

Ushauri:

Naomba bodi ya mikopo ifikirie upya na kwa umakini je hii ni haki chuo kizima kwa mwaka huu kuwapa mikopo wanafunzi wawili tu? Tunaomba bodi ya mikopo, viongozi wa serikali na wadau wa elimu watusaidie kututatulia tatizo hili. Wengi wetu ni maskini na hatuna uwezo wa kujisomesha bila ya mkopo.

Ahsanteni naomba kuwasilisha!
Bora nyie wawili wamepata ila huku kwetu darasa zima hatuna tumelipa direct fee daily tunampiga sound accountant wa chuo kwamba tutapewa mkopo sasa itafika kipindi itawekwa deadline tutafukuzwa chuo
 
Acheni kulia lia. Serikali itasomesha inapoweza, na sio wanafunzi wote.
 
Mbona mm nilijisomesha kimasikini. Nyie mnapenda starehe ya kunywa pombe, cm kubwa maisha bora wakati bado wanafunzi!!!!!!!
 
Mtukufu amegundua wasomi ni wasumbuf sana. wanahoji kila kitu sasa namna pekee ya kuwapunguza ni kuwanyima mikopo
 
Mbona mm nilijisomesha kimasikini. Nyie mnapenda starehe ya kunywa pombe, cm kubwa maisha bora wakati bado wanafunzi!!!!!!!
Wape uzoefu wewe umewezaje kumudu kujisomesha.Sio kila anayelia anapenda
 
jamani ivi kuna batch nyingine? Mara nasikia majina 25 elfu yamekamilika mara bado elfu 3 ivi ukweli ni upi katika hili....msaada kwa anaejua chochote
 
DMI haina issue siku hizi ..daaah poleni sana
 
Mkipata kamuda msikilizage kale ka wimbo ka ndio mzee na sio mzee ka prof j.
 
Back
Top Bottom