Hii mitandao ya simu tunasalimika?

Hii mitandao ya simu tunasalimika?

Mwanaume

Senior Member
Joined
Oct 11, 2009
Posts
133
Reaction score
25
Jamaa yangu mwenye simu ya airtyel 078... simu yake tarehe 16/8/2016 iliingiliwa na wahalifu wakitumia particulars za usajili walizozipata kwa njia ya kihalifu.

Wakaitumia simu hiyo kwa uhalifu kwa kutaka kuibiwa watu. Haijulikana walifanikiwa kwa kiasi gani. Lakini siku mbili baadaye watu wa customer care walipigiwa simu, pamoja na kushindwa kuzuia mhalifu kuendelea kutumia line hiyo kwa madai kwamba imetumika namba isiyokuwa ya mwenyewe, wakashauri key contacts wajulishwe uwepo wa tukio hilo na wakaelekeza suluhu ya kudumu jamaa aende airtel shop na kitambulisho kwa ajili ya kurekebisha tatizo.

Mwezi mmoja baadaye, jamaa akaenda airtel shop kama alivyoelekezwa na wakajaribu kumhudumia. Lakini tangu alipohudumiwa jamaa hajarecover mawasiliano ya simu yake licha ya kuwasiliana zaidi ya mara nne na watu wa customercare wakiahidi kurekebisha tatizo.

Wakati line inaswapiwa tarehe 16/9/2017, mhalifu alikuwa akiendelea kupokea na kujibu simu wa conbtacts wake pamoja na kufanya some transactions.

Issue ni hii, kama mitandao inazembea kuhandle suala sensitive kwa usalama na mali kiasi hiki, je wadau tuko salama kiasi gani?

Wakatabahu
 
Ninachojua mimi, customer care wengi wa hii mitandao hawana uelewa mpana wa kazi hiyo, cha kusikitikia zaidi, kwenye issue sensitive hawana hata wenye taaluma kwaajili ya ku-handle kesi ambazo ni more technical.
 
Ni hatari sana. Ndio maana nchi za wenzetu na baadhi ya makampuni hata hapa nyumbani kuna kitengo cha Cybersecurity, hiki kitengo ni muhimu sana haswa katika matatizo kama hayo (hacking).
Jamaa ashukuru ya kwamba hiyo namba yake wametumia kwa njia hizo, maana ingeweza kuwa mbaya zaidi ingekuwa ya kwamba imetumika kwenye uhalifu ambapo mtu au watu walipoteza maisha. Unaweza kujikuta kwenye matatizo ambayo hukutegemea. Mpaka ijulikane haukuhusika utakuwa umeshapumzika Segerea hata mwaka mzima Kama sio miwili.

Ila na sisi Watanzania tumezoea sana kuburuzwa na haya makampuni. Huyo mhanga ilitakiwa atafute "mwanasheria msomi" na kupata ushauri wa kisheria nini kifanyike. Nina hakika ana shauri la msingi akifungua kesi dhidi ya hao service provider.
 
Back
Top Bottom