Nas Mapesa
JF-Expert Member
- Jul 31, 2014
- 5,251
- 5,322
Salaam,wana jukwaa kuna jambo linaendelea huku mkoa wa Tanga,ningependa kushare nanyi pengine kuna wanaofahamu kuhusu jambo hili, iko hivi kuna watu wanashirikiana na Nmb kuzunguka mkoa mzima wakijinadi kua ni watoaji mikopo,mikopo hiyo yenye sharti la kua na kitambulisho cha kura tu,kumezuka sintofahamu kwa namna ya ukopaji, wanavyodai ukikopa mil 2 unatakiwa urejeshe Sh 86000 Kila mwezi kwa miezi 12 , hapa ndipo panapochanganya ukipiga hesabu ya haraka utagundua kua mkopeshaji hapati faida zaidi ya hasara sababu marejesho hayafiki hata kiwango ulichokopa,humu kuna wajuvi wa mambo lukuki,mweye ufahamu kama hawa jamaa wameshapita maeneo ya Kwao atupe taarifa na Kama kweli wanatoa mikopo pia atupe taarifa,aina hii ya mikopo sijapata ona popote duniani,kujisajili kwenye Hiyo mikopo ni Sh 20000 kwa Tanga na Sh 40000-80000 kwa wilaya zingine za Tanga.
Note:utapeli umekua mwingi sana siku za karibuni, tuna wasiwasi.
Note:utapeli umekua mwingi sana siku za karibuni, tuna wasiwasi.