Hii Mikoa Nani Kailoga?


Ulishaenda vijiji vya Dodoma? Tena hata sio mbali jaribu tu kwenda pale kijiji kilichopo mjini kabisa Kule Ng'ong'ona jirani na chuo kikuu cha dodoma kitivo cha elimu ndo utajua maji ni uhai ama sio na ndo utajua vijiji vyenyeshida viko Lindi na Mtwara tu au la.
 
"ukawa @ work"
sasa hivi ninapoandika kuna watu wamekwama kilometer chache baada ya daraja la Mkapa na watalala hapo kama hawatakwamuliwa.........watu wanaitukana serikali yao sikivu ile mbaya...........alafu wewe unasema @ work Nyambafu......
 

Nilikuwa huko mwaka jana (Vijiji vya Dodoma, Singida na Manyara) sawa tatizo la maji pia ni kubwa, but generally ukiangalia kiwango cha umasikini wagogo hawa wana nafuu maana wana vimbuzi, ving'ombe, wanalima sana mtama n.k Nyumba zao za tembe though full suti ni afadhali kuliko baadhi ya vibanda nilivyoona kusini. Kuna kipindi miaka ya nyuma nilikuwa Lindi, wilaya ya Kilwa Kijiji kimoja mbele ya Nainokwe nilishuhudia tukio la simba akichomoa mtu kutoka kwenye kibanda na kuondoka naye. Baada ya kusikia makelele kulifika sehemu ya tukio na kwa kweli huwezi kusema mtu alikuwa ndani kwani ukuta ni wa majani.
 

Kwani wale wa Pwani ambao wengi wao ni wavuvi hawana uhakika wachakula kwao?? Mbona hata makazi wengine ni nafuu maana kuna vijiji sio vyote hadi nyumba wanajenga kwa tofali za kuchoma sikuiz na Dodoma mmh bora tu nikae kimya ila hali ya vijiji tz ni kote tu shida huko manyara wengi wao hata makazi hawana kutokana na nature yao ya ufugaji ila still hali zao duni
 

Pwani ipi? Mfano kwa wilaya ya Kilwa pia ukianzia vijiji vya pwani vya Marendego, Somanga, Tingi, Njia nne, Mtandango, Mtoni , (Kilwa kivinje mpaka Masoko na Kilwa Kisiwani kuna improvements kubwa), Songomara, Malalani all the way to Jiwe la Mzungu (mpakani na Lindi vijijini), Mkwaya etc tunajua jinsi hali zilivyo. Pia kama umefuatilia tafiti mbalimbali za maeneo haya ya pwani utabaini kwamba wavuvi hawa wamekuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi sana hivyo kushindwa kujikwamua mfano kupungua kwa samaki, wavuvi wakubwa kutoka nje wenye vyombo bora kuliko wao, uvuvi wa meli kubwa kubwa, uvuvi wa mabomu etc
 
habar mkuu?. mi nataka kwenda kuishi mtwara au lindi hasa kijijin ili niweze kujishuhurisha na ufugaji wa kuku wa kienyeji na kilimo kwaajili ya chakula. Nimefanya tafiti ili niweze kuona kijiji kipi niende nikapata majibu:
1. Ng'au
2. mtoni kata ya miteja

kwa uzoefu wako ni wapi patanifaa? au kama una option nyingine naomba msaada wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…