Hii inamuhusu kila mwanaJF, ni muhimu...

Range of deafness
Mild deafness - people who are
hard of hearing may have a little
difficulty following speech in
certain circumstances, especially if
there is a lot of background noise,
but can generally cope if the
environment is favourable.
Moderate deafness - people with
moderate deafness have some
difficulty in following speech in
most settings, but can generally get
a lot of help from wearing a
hearing aid.
Severe deafness - people with
severe deafness hear no speech
without the help of a hearing aid.
Profound deafness - people who
are profoundly deaf hear no
speech, even with the benefit of a
hearing aid( hope mmeamini sasa kuwa kiziwi sio lazma awe hasikii kabisa)
 
Naomba kuchangia kulingana na uwelewa wangu. Hawa walemavu wanamajina ya utambulisho kama vile kiziwi, kipofu, bubu, zeruzeru nk.

Kumwita mtu kwa kutumia kiwakilishi (ki) ni kumfananisha na kitu kama vile, Kisu, kijiko, kiti, kikombe nk. Lugha nzuri ya kutumia kwa hawa ndugu zetu iwe hivi:

1. Kipofu= Asiyeona
2. Kiziwi= Asiyesikia
3. Zeruzeru = Albino
4. Kwa walemavu wa miguu au mikono kuna watu wanawaita vi(ki)wete. Neno sahihi hapa ni mlemavu.
5. Kichaa, mwenda wazimu, chizi huu si ulemavu huu ni ugonjwa that why wanapatiwa matibabu. Hawa wanaitwa wagonjwa wa akili.
Ahsanteni
 
Habari wana jf.
Kumekua na mkanganyiko sana katika lugha tunazotumia wana jf hasa kuhusiana na watu wenye ulemavu. Kwa kutumia taaluma yangu nimeona bora nitoe darasa na yeyote mwenye swali au maoni awe huru kuuliza. Ni ufafanuzi wa majina sahihi ya watu wenye ulemavu
1. Albino
Huyu ni mtu mwenye ulemavu wa ngozi na anatambulika sana kwa muonekano tu. Tafadhali usimuite ZERUZERU, dili, mzungu au majina mengine yanayodhalilisha utu wake. Jina sahihi ni albino au mwenye ulemavu wa ngozi.
2. Kiziwi
Huyu ni mtu mwenye upungufu wa usikivu either hasikii kabisa au ana usikivu kidogo (residual hearing). Hawa wanatambulika hasa kwa kutembea makundi makundi na wanatumia lugha ya alama (nyie mnaita lugha ya ishara au mikono). Ni mara chache sana kumkuta kiziwi anatembea peke ake .Usimuite BUBU au ASIYESIKIA (huyu ni kiburi). Tafadhali muite kiziwi ndo jina lenye heshima kwake.( nahitaji maswali mengi sana kuhusu kundi hili maana nalifahamu kuliko makundi yote hapa).
3. Asiyeona
Usithubutu kumuita KIPOFU maana kipofu ni mjinga wa jambo fulani ndo mana tuna vipofu wa mapenzi nk. Muite asiyeona tu lina heshima na hadhi na hawa wanatambulika sana kwa fimbo nyeupe maalum wanayotumia kutembelea au wanakua na muongozaji.
4. Mwenye ulemavu wa akili
Usimuite taahira, ndondocha, au chizi. Hakupenda kuwa ivo ila jina sahihi ni mwenye ulemavu wa akili na hawa wako makundi tofauti kama wale wenye autisim na mental retardation ni watu wawili tofauti japo wote ni wenye ulemavu wa akili.
N.B. Kuna aina nyingi sana za ulemavu siwezi kuzianisha hapa ila tuwe waangalifu kwa majina tunayotumia kuwaita hawa wenzetu wenye ulemavu manake wenyewe wanasema kila mtu ni mlemavu mtarajiwa so take care. Nakaribisha maswali na maoni

mheshimiwa, wewe unaleta political correctness. usinielewe vibaya lakini
1.kipofu- kiswahili fasaha ni mtu asieona,hamna ubaya wowote kutumia hili jina kwa maana yake halisi.
2.kiziwi-kiswahili fasaha ni mtu asiesikia,hamna ubaya wowote kutumia hili jina inavyotakiwa.
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Naomba kuchangia kulingana na uwelewa wangu. Hawa walemavu wanamajina ya utambulisho kama vile kiziwi, kipofu, bubu, zeruzeru nk.

Kumwita mtu kwa kutumia kiwakilishi (ki) ni kumfananisha na kitu kama vile, Kisu, kijiko, kiti, kikombe nk. Lugha nzuri ya kutumia kwa hawa ndugu zetu iwe hivi:

1. Kipofu= Asiyeona
2. Kiziwi= Asiyesikia
3. Zeruzeru = Albino
4. Kwa walemavu wa miguu au mikono kuna watu wanawaita vi(ki)wete. Neno sahihi hapa ni mlemavu.
5. Kichaa, mwenda wazimu, chizi huu si ulemavu huu ni ugonjwa that why wanapatiwa matibabu. Hawa wanaitwa wagonjwa wa akili.
Ahsanteni

Shukrani kwa mchango wako ila naomba nikupe mpya nyingine.
Tukianza na neno mlemavu. Disability act ilianzia marekani miaka ya nyuma sana na watu wenye ulemavu walikua wanaitwa disabled pipo kumaanisha kuwa mtu anatambuliwa kwa ulemavu ndo mana inaanza adjective disable then inafata people, baadae ikaonekana sio sahihi kumtambua mtu kwa ulemavu wake hivyo wakabadilisha ikawa people with disability manake mtu kwanza disability baadae ndo hapo tz ikaanza kutumia mtu kwanza na utu wake ila kama itahitajika maelezo ya zaidi ndo utasema mwenye ulemavu. So ulemavu sio ishu ila ni sifa ya ziada tu kwa mtu so ni vyema kusema mtu mwenye ulemavu na sio mlemavu/walemavu sawa na kusema mweusi aje badala ya kusema mtu mweusi aje hop umepata kitu hapo.
Lugha ni makubaliano kwa wanajamii husika, Asiyesikia maana yake ni kiburi ndo mana utasikia mama anamsema mtoto kuwa "we mtoto husikii kila siku nakuonya" yafsiri yake ni kuwa huyu mtoto ni kiburi au jeuri hafati maelekeze. Kwa kulitambia hili viziwi kwenye katiba ya chama chao wakaona ni vyema watambulike kwa jina viziwi/deai na ndo mana kuna chama cha viziwi tz na hakuna chama cha wasiosikia au ma bubu.
Jamani sawa kuna ngeli ya ki-vi inayotumika kwa vitu na sio watu lakini lugha ni makubaliano ya watu wenyewe ndo wamechagua waitwe ivo
 
Mtoa mada.
Unaleta kitu inaitwa ubinadamu na sio ufasaha wa lugha.
Hayo maneno yote yapo kama ulivyoyapinga.
Naungana na RRONDO
Usituelewe vibaya.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hiyo Albino ni kizungu kwa kiswahili ni Zeruzeru hata kwenye kamusi TUKI imetafsiriwa jivyo i. e Albino = Zeruzeru.
 
Albino ni kiingereza. Sioni kwanini kingereza uwe sawa lakini zeruzeru liwr kosa. Pili, aina hii mpya inawapumbaza watoto wanaojifunza. Kwa mfano, ukipewa crosswords utafanyaje kama kitu kinachopaswa kuwa na neno moja 'zeruzeru' utaweka 'mtu mwenye ulemavu wa ngozi'. Mimi mdogo wangu mmoja ni marehemu sasa, alikuwa zeruzeru. Aliitwa mazembe.
 
mheshimiwa, wewe unaleta political correctness. usinielewe vibaya lakini
1.kipofu- kiswahili fasaha ni mtu asieona,hamna ubaya wowote kutumia hili jina kwa maana yake halisi.
2.kiziwi-kiswahili fasaha ni mtu asiesikia,hamna ubaya wowote kutumia hili jina inavyotakiwa.

mimi natoa elimu ili msijikute mmeingia kwenye matatizo yasiyo ya msingi. Hebu kutana na prof bagandashwa ni asiyeona yupo pale udsm afu muite we kipofu uone atakavyo react. Au asiyeona yeyote jifanye hujui tu muite kipofu unless awe hajitambui kama wale wanaowekaga vikopo barabarani na kuomba omba
 
mimi natoa elimu ili msijikute mmeingia kwenye matatizo yasiyo ya msingi. Hebu kutana na prof bagandashwa ni asiyeona yupo pale udsm afu muite we kipofu uone atakavyo react. Au asiyeona yeyote jifanye hujui tu muite kipofu unless awe hajitambui kama wale wanaowekaga vikopo barabarani na kuomba omba

au kutana na mr dickson mveyange director wa chama cha viziwi muite bubu ndo utajua nini namaanisha
 
Aisee bagandashwa nilimwandikia makala miaka mingi. Naomba mawasiliano yake. Wakati huo aliishi ubungo kibangu nadhani.
 
Range of deafness
Mild deafness - people who are
hard of hearing may have a little
difficulty following speech in
certain circumstances, especially if
there is a lot of background noise,
but can generally cope if the
environment is favourable.
Moderate deafness - people with
moderate deafness have some
difficulty in following speech in
most settings, but can generally get
a lot of help from wearing a
hearing aid.
Severe deafness - people with
severe deafness hear no speech
without the help of a hearing aid.
Profound deafness - people who
are profoundly deaf hear no
speech, even with the benefit of a
hearing aid( hope mmeamini sasa kuwa kiziwi sio lazma awe hasikii kabisa)

Si kila neno lililoandikwa kwa kiingereza ni sahihi
 
Naomba mnielewe wakuu.
Niko hapa kutoa confusion inayojitokezaga mara nyingi mbele ya macho yangu. Nimeona watu wakipigwa au kufukuzwa wanapotumia majina zeruzeru, kipofu au asiyesikia.
Ukitaka kuthibidisha just do a simple practical, kutana na prof Bagandashwa au Anastaz Amon(huyu yupo kwenye bunge la katiba) wote hawa hawaoni then waite samahanini nyie vipofu kuna ishu nataka kuwaambia. Ukifanikiwa kutoka salama mshukuru Mungu. Au kutana na mr dickson mveyange(exucutive director wa chavita) au kiongozi yeyote wa chama cha viziwi muite bubu au asiyesikia uone kitakachokukuta.
Nimejionea mvurugano mkubwa sana ukijitokeza coz mi nafanya kazi na hawa watu mwaka wa 6 sasa naelewa ndo mana nawatahadharisha juu ya majina yasiyofaa kwa watu wenye ulemavu.
Albino ni neno la kiingereza lakini kwani kuna maneno mangap tunatumia na hayana tatizo. Angalia neno bajeti au tochi kiswahili kiko wap hapo? Lengo la lugha ni kuelewana na jamii husika
 
Mtoa mada.
Unaleta kitu inaitwa ubinadamu na sio ufasaha wa lugha.
Hayo maneno yote yapo kama ulivyoyapinga.
Naungana na RRONDO
Usituelewe vibaya.

mkuu kama yapo kama yalivyo kiufasaha nenda kwenye makongamano ya watu wenye ulemavu then yatumia hayo majina yako then wakikuletea fujo na kukupiga waambie mbona kamusi imeyataja na toa utetezi wako lazma watakuelewa japo kipindi hiko am sure utakua umeshaumia
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom