Hii imekaaje wakuu

Kakole

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
2,094
1,743
Akili ya midume kabla ya kuoa,

Mke asipomjali na kumpenda mama yangu kwakweli itabidi tu tuachane, yaani mama yangu alivyonihangaikia kwakweli sitaki mtu wa kumnyanyasa kabisa, ikitokea nikaoa mwanamke asiyempenda na kumjali mama yangu basi hata mimi hawezi kunipenda na kunijali pia, mama ndio kila kitu bwana, ameuza mpaka mkaa ili tu niweze kwenda shule.

Baada ya kuoa sasa halafu bahati mbaya kaoa mke asiyemjali mama yake.

aaaah! huyu mama bwana ni msumbufu sana, yeye anapaswa kuishi na huyu mke wangu kwa akili la sivyo mimi sintaweza kujenga familia, yeye anapaswa kumuelewa huyu mke wangu kuwa akili zake ziko resi sana, aaah! yaani mama amekuwa kikwanzo katika ndoa yetu, yaani mama hajaliwi tena hapo, kila kizuri ni kwa mke tu mama hakumbukwi tena, kanga mpya haijui mpaka ccm wampe baada ya miaka mitano.

Wakuu tuwajali sana mama zetu kwa hali na mali tusijisahau, wadada pia mnapoolewa jitahidi sana kuwajali hawa wamama, wengine wamebaki wajane kwa hiyo mume alobakia wa kumjali na kumhudumia ni mume wako hivyo muwe na huruma sana.

Nawasilisha.
 
Mweee ninavompenda mama yangu mimi jamani Mungu mwenyewe anajua .... kashindia hadi maji ili tu nisome mimi jamani Ila jikosee mtukane au mfanyie kitu kitachomuhuzunisha ohooo ntakutengua taya... Mama aheshimiwe
 
NIMPENDENANI amefanikiwa sana ktk hili na kwa kweli ni.mfano wa kuigwa na wanawake wengune.

Ni kazi rahisi sana kuishi na mama mkwe if only wewe ni mwanamke mwenye sifa za kike otherwise huwezi.

Kuishi na mama sioni taabu kwani.kama una uwezo wa kumtunza na hahitaji vitu vingi, ma wanaume nao tuwe na akili unashindwaje kubalance kati ya mama na mkeo??.

Kosa kubwa tunalofanya ni kulinganisha kati ya mama na mkeo yupi bora, this is the greatest mistakes we do, a mother and a wife are incomperable entities, mama anaupendo wake tofauti na mke, na.mke ana nafasi yake na upendo wake pia
 
Dah huwa nawazaganikiolewa na mwanamme asimpend na kumjari mama yangu itakuwaje wakati mie namjali mama yale? Sipati picha
 
Dah huwa nawazaganikiolewa na mwanamme asimpend na kumjari mama yangu itakuwaje wakati mie namjali mama yale? Sipati picha
Omba Mungu akujalie sawasawa na hitaji la moyo wako.
 
Mweee ninavompenda mama yangu mimi jamani Mungu mwenyewe anajua .... kashindia hadi maji ili tu nisome mimi jamani Ila jikosee mtukane au mfanyie kitu kitachomuhuzunisha ohooo ntakutengua taya... Mama aheshimiwe
Endelea kumpenda na kumheshimu nawe utaishi miaka mingi.
 
NIMPENDENANI amefanikiwa sana ktk hili na kwa kweli ni.mfano wa kuigwa na wanawake wengune.

Ni kazi rahisi sana kuishi na mama mkwe if only wewe ni mwanamke mwenye sifa za kike otherwise huwezi.

Kuishi na mama sioni taabu kwani.kama una uwezo wa kumtunza na hahitaji vitu vingi, ma wanaume nao tuwe na akili unashindwaje kubalance kati ya mama na mkeo??.

Kosa kubwa tunalofanya ni kulinganisha kati ya mama na mkeo yupi bora, this is the greatest mistakes we do, a mother and a wife are incomperable entities, mama anaupendo wake tofauti na mke, na.mke ana nafasi yake na upendo wake pia
Kwanza hakuna kama mama,na huwezi kumpenda Mama yako mzazi ukashindwa kumpenda mama wa mwenzio,na kama unaweza kumstahmilia mama yako mzazi na huenda akawa na vitimbi kuliko mama mkwe,hata mama mkwe awe mkorofi vipi
wewe ukimuonyesha ukarimu wallah atabadilika na nafsi yake itamsuta....
 
Akili ya midume kabla ya kuoa,

Mke asipomjali na kumpenda mama yangu kwakweli itabidi tu tuachane, yaani mama yangu alivyonihangaikia kwakweli sitaki mtu wa kumnyanyasa kabisa, ikitokea nikaoa mwanamke asiyempenda na kumjali mama yangu basi hata mimi hawezi kunipenda na kunijali pia, mama ndio kila kitu bwana, ameuza mpaka mkaa ili tu niweze kwenda shule.

Baada ya kuoa sasa halafu bahati mbaya kaoa mke asiyemjali mama yake.

aaaah! huyu mama bwana ni msumbufu sana, yeye anapaswa kuishi na huyu mke wangu kwa akili la sivyo mimi sintaweza kujenga familia, yeye anapaswa kumuelewa huyu mke wangu kuwa akili zake ziko resi sana, aaah! yaani mama amekuwa kikwanzo katika ndoa yetu, yaani mama hajaliwi tena hapo, kila kizuri ni kwa mke tu mama hakumbukwi tena, kanga mpya haijui mpaka ccm wampe baada ya miaka mitano.

Wakuu tuwajali sana mama zetu kwa hali na mali tusijisahau, wadada pia mnapoolewa jitahidi sana kuwajali hawa wamama, wengine wamebaki wajane kwa hiyo mume alobakia wa kumjali na kumhudumia ni mume wako hivyo muwe na huruma sana.

Nawasilisha.
"Sio vyema kumdharau mama mzazi kutokana na matamshi ya mke"
 
kwa jinsi mama yangu alivyo mkorofi, ana kelele ( teh teh), muongeaji (na bado ninampenda) ni expirience tosha kuishi na mama wa mwenzangu vizuri hata akiwa na maneno kias gani, ( ikiwa nitajaaliwa kumpata).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom