Mkuu hiyo record ya mechi 15 Man U labda kama kabla ya Arsenal ile..Man u mbona records hizi washazipitia mara nyingi tu
Man untd walisumbua sana enzi wameongoza ligi
Of courseUkiona unazungumzwa sana ujue wanakukubali.
Umeona mbali mkuu.Hivi mnakumbuka wakati ligi inaanza?
Man untd walianza kwa kila aina ya mbwembwe na kujipa majina kama wazee wa 4g na mengineo..
Enzi hizo striker wao Lukaku anafunga balaa, wakaanza kuwatukana kina Morata na wengineo waliowakosa kwenye usajili
Mwisho wa siku wakaanza kula kipondo, watu wanajipigia tuu, mara ghafla lukaku wao akageuka LIKUKU..
Najaribu kuwaza hapa hivi hawa Man untd wangecheza mechi 15 mfulululizo bila kufungwa hata mechi 1 kama Man city hata hii J.F si tungeiona ya moto, tungeweka wapi nyuso zetu kwa mbwembwe zao zile...?