Inashangaza kuona kuwa heslb walitoa nafasi ya wiki moja tu ya kukata rufaa, lakini wao zinakaribia kumalizikia wiki mbili sasa bado wako kimya kuhusu matokeo ya rufaa za watu. Kama hakuna aliyefanikiwa basi waseme maana muda umekwenda sana.
mbona tushapigwa 3-0 tayari...hamna matokeo ya maana watakayotoa.....yaani heslb wameshindwa kutafuta partners wa kuwapa pesa ili wawape wanafunzi mkopo wanasubir pesa ya serikali tu...nahisi CEO wao amekariri madesa tu lkn sio mbunifu kabisa
Bodi ijaribu kutumia busara na hekima,watoto wa masikini wanataabika vyuoni kwa kukosa hata hela ya kula!vipi watasoma? Hii ni aibu kwa bodi na serikali kwa ujumla nasema hivi kwa sababu mfano suala kama la "transfer" kwa waliosajiliwa chuo kengine na hela kupelekwa chuo kengine,me sidhani kama mchakato wa kuhamisha hiyo pesa kwa kutumia technology iliyopo sasa unaweza chukua hata mwezi!!hii ni aibu ifike mahali wahusika muone aibu,basi hata feedbacks ziwe zunatolewa muda wa majibu husika unapopitilza na si kukaa kimya,watoto wa maskini wanateseka kwa mawazo vyuoni!
Inashangaza kuona kuwa heslb walitoa nafasi ya wiki moja tu ya kukata rufaa, lakini wao zinakaribia kumalizikia wiki mbili sasa bado wako kimya kuhusu matokeo ya rufaa za watu. Kama hakuna aliyefanikiwa basi waseme maana muda umekwenda sana.
Nadhani bado wanasubiri maelekezo toka juu! Hakuna kujiamini wala kujiongeza hata kidogo! Watu wanahofu kufanya maamuzi japo nafasi zao zinawaruhusu kufanya maamuzi! Naona tutasubiri sana! Halafu mwenyewe ngazi ya juu anaona raaaaahaaaaaa!
Nimesoma kichwa cha Habari nikaja mbio nikijua ni ile rufaa ya 15% to 8%, duh kumbe ni rufaa ya watu kuingia kwa huu mtego, anyway hakuna apendaye mikopo ni basi tu watu hawawezi jisomesha