HESLB Kuna hili limeumiza kwakweli

HESLB Kuna hili limeumiza kwakweli

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,762
Reaction score
4,975
Kwanza Kabisa namshukuru Mola kwa uzima pia nawasalimu nyote.
Nimejaribu kufuatilia loan repayment yangu heslb nilichokiona naomba niwajulishe na wenzangu ili kama ulikuwa hufahamu uanze kufahamu na kuchukua hatua usije ukashangaa huku unaumia.

Heslb kuna makato ya ziada waliyoyaweka ambayo haya hasa ndiyo pigo kuu kwa watoto wa wakulima walioomba mkopo.

Kuna additional charges ambamo ndani yake kuna Administrational fee,penalty(10% na kuna Value retention fee.

Hayo mambo ndiyo ambayo yatawaduwaza. Nilifikia hatua ya kutaka kupata loan repayment statement yangu baada ya kuona salary yaku kuwa kama ina kirusi.

Nimeshangazwa sana na badiliko la makato kutoka 42560 mpaka 75200.
Nilichokiona ni riba kubwa inayofikia Milioni mbili na point kadhaa
Nakumbuka kipindi nahitimu pale udsm mwaka 2010 tuliambiwa kuwa wataanza kutukata marejesho ya mkopo baada ya miaka miwili na Mimi niliajiriwa mwaka 2011 mwezi wa kwanza na mwaka 2012 Disemba walianz kunikata marejesho yao kwa utaratibu wa 42560 @ mwezi.

Ila ghafla mwaka huu naona makato yamefikia 75200. Nilichokiona kingine ni kuwa nimepigwa penalty kutokana na kuchelewa kuanza kurejesha.

My take dawa ya deni ni kulipa ila kwa mtindo huu tunaumizana sana ukizingatia taarifa tulitoa mapema kwa waajiri wetu tuanze kukatwa lakini halo ndiyo hiyo.

Rai yangu nawasihi kama unafahamu ulikopeshwa na bodi ya mikopo ya elimu ya juu fuatilia mapema uanze kulipa deni na hii ni kwa wale ambao wapo kwenye ajira na hawakatwi marejesho hayo huko mbele wakikunasa utaimba na additional charges.
 
Kwanza Kabisa namshukuru Mola kwa uzima pia nawasalimu nyote.
Nimejaribu kufuatilia loan repayment yangu heslb nilichokiona naomba niwajulishe na wenzangu ili kama ulikuwa hufahamu uanze kufahamu na kuchukua hatua usije ukashangaa huku unaumia.

Heslb kuna makato ya ziada waliyoyaweka ambayo haya hasa ndiyo pigo kuu kwa watoto wa wakulima walioomba mkopo.

Kuna additional charges ambamo ndani yake kuna Administrational fee,penalty(10% na kuna Value retention fee.

Hayo mambo ndiyo ambayo yatawaduwaza. Nilifikia hatua ya kutaka kupata loan repayment statement yangu baada ya kuona salary yaku kuwa kama ina kirusi.

Nimeshangazwa sana na badiliko la makato kutoka 42560 mpaka 75200.
Nilichokiona ni riba kubwa inayofikia Milioni mbili na point kadhaa
Nakumbuka kipindi nahitimu pale udsm mwaka 2010 tuliambiwa kuwa wataanza kutukata marejesho ya mkopo baada ya miaka miwili na Mimi niliajiriwa mwaka 2011 mwezi wa kwanza na mwaka 2012 Disemba walianz kunikata marejesho yao kwa utaratibu wa 42560 @ mwezi.

Ila ghafla mwaka huu naona makato yamefikia 75200. Nilichokiona kingine ni kuwa nimepigwa penalty kutokana na kuchelewa kuanza kurejesha.

My take dawa ya deni ni kulipa ila kwa mtindo huu tunaumizana sana ukizingatia taarifa tulitoa mapema kwa waajiri wetu tuanze kukatwa lakini halo ndiyo hiyo.

Rai yangu nawasihi kama unafahamu ulikopeshwa na bodi ya mikopo ya elimu ya juu fuatilia mapema uanze kulipa deni na hii ni kwa wale ambao wapo kwenye ajira na hawakatwi marejesho hayo huko mbele wakikunasa utaimba na additional charges.
Mkuu,
Soma hii kitu kwa faida yako na wengine:

UREJESHAJI WA MIKOPO ELIMU YA JUU
UTARATIBU KWA WAAJIRI NA WAAJIRIWA KATIKA UREJESHAJI WA

MIKOPO YA ELIMU YA JUU


Swali: Mwajiri anapaswa kufanya nini baada ya kuajiri wahitimu wapya?

· Kwa mujibu wa sheria Na. 9 ya mwaka 2004 ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (kama ilivyorekebishwa), mwajiri anapaswa aijulishe Bodi kwa maandishi kuhusu waajiriwa wapya ambao ni wahitimu wa vyuo vya elimu ya juu ndani ya siku ishirini na nane (28) tangu tarehe ambayo wahitimu hao wameajiriwa.


Swali: Nini kitafuata baada ya kuwasilisha HESLB orodha ya wahitimu walioajiriwa?

· Baada ya kupokea taarifa kutoka kwa waajiri, Bodi itabainisha wafanyakazi walionufaika na mikopo ya elimu ya juu.


Swali: Mwajiri ana wajibu gani baada ya kupokea orodha ya wadaiwa wa mikopo kutoka HESLB?

· Anapaswa kuhakikisha kuwa makato ya kila mwezi kutoka kwenye mishahara ya wadaiwa wa mikopo yanawasilishwa Bodi kama ilivyoelekezwa ndani ya siku kumi na tano (15) baada ya kila mwisho wa mwezi.


Swali: Nini kitatokea endapo mwajiri ataacha kukata mshahara wa mfanyakazi baada ya kuelezwa na HESLB kwamba mfanyakazi huyo ni mdaiwa wa mkopo?

· Iwapo mwajiri atashindwa kukata ama kukata mshahara wa mdaiwa wa mkopo na kushindwa kuwasilisha makato hayo Bodi ndani ya muda uliopangwa, atatozwa asilimia kumi (10%) ya kiasi cha deni lililopaswa kulipwa kwa kila mwezi ambao makato hayatawasilishwa.


Swali: Ni lini mnufaika wa mkopo anapaswa kuanza kurejesha mkopo wake?

· Mkopo huanza kulipwa unapomalizika mwaka mmoja wa neema baada ya kuhitimu masomo ya elimu ya juu au baada ya kusitisha masomo kwa sababu yoyote ile.


Swali: Je, ajira ya mdaiwa wa mkopo ni jambo linalozingaliwa katika urejeshaji wa mikopo?

· Wadaiwa wanapaswa waanze kurejesha mikopo muda unapofika bila kujali iwapo wameajiriwa ama la.


Swali: Ni asilimia ngapi hutozwa kama tozo la kutunza Thamani ya fedha kwa kila mdaiwa wa mkopo?

  • Madeni yote ya mikopo hutozwa asilimia sita (6%) kama tozo la kutunza Thamani ya Fedha (VRF) kwa mwaka.

Swali: Kwa nini HESLB inatoza tozo la kutunza Thamani ya Fedha (VRF) kwenye mikopo inayorejeshwa?

· Mikopo inatozwa tozo la kutunza Thamani ya Fedha ili kutunza thamani ya fedha dhidi ya mfumuko wa bei ambao unapaswa kuwa na thamani sawa wakati mkopo utakapotolewa kwa wanafunzi wengine wenye uhitaji katika siku zijazo.


Swali: Ni hatua zipi za kisheria zitachukuliwa kwa wadaiwa ambao hawatarejesha mikopo yao?

· Mdaiwa yeyote ambaye, bila sababu za msingi atashindwa kulipa mkopo atachukuliwa hatua za kisheria. Aidha, mambo yafuatayo yatafanyika:
(a) Atapata adhabu ya kulipa asilimia kumi (10%) ya mkopo wake wote.
(b) Taarifa zake zitawasilishwa kwenye taasisi zinazosimamia taarifa za

wakopaji wanaotaka kukopa kutoka taasisi za fedha zinazotoa mikopo,

ambapo watazuiliwa kukopa kutoka kwenye Taasisi za Fedha.
(c) Atazuiliwa kupata ufadhili wa Serikali kwa ajili ya masomo ya Uzamili au

Uzamivu katika chuo chochote cha Elimu ya Juu ndani na nje ya nchi.
(d) Maelezo yao yatawasilishwa Wizara ya Mambo ya Ndani, Idara ya

Uhamiaji ambapo hawatapewa kibali kwa ajili ya kusafiri nje ya nchi


Swali: Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali(CAG) na kampuni zingine binafsi za ukaguzi wana wajibu gani katika urejeshaji wa mikopo?

· Jukumu la Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG) na makampuni mengine binafsi ya Ukaguzi ni kuhakikisha waajiri wanatekeleza kwa kuwasilisha wahitimu Bodi ya mikopo na makato ya fedha kutoka kwa wadaiwa yanawasilishwa kama ilivyoelekezwa.


Swali: Mnufaika wa mkopo anapaswa kufanya nini ili kulipa deni lake?

· Mara baada ya kuhitimu masomo au kusitisha masomo yake kwa sababu yoyote ile, mnufaika anapaswa aitaarifu Bodi kwa maandishi mahali alipo na hali ya ajira yake ili kukubalina na Bodi juu ya ulipaji wa mkopo wake.


Swali: Makato huwasilishwaje HESLB?

· Kwa wanufaika waajiriwa, hukatwa asilimia nane (8%) ya mshahara wa kila mwezi.

· Mnufaika anaweza kulipa kiwango cha chini cha shilingi 100,000/= kila mwezi kupitia Akaunti zifuatazo:
i. Benki ya Posta Tanzania CCA0240000032
ii. NMB Bank Akaunti 2011100205
iii. Benki ya CRDB Akaunti 01J1028467503

-------------------------
 
Mkuu,
Soma hii kitu kwa faida yako na wengine:

UREJESHAJI WA MIKOPO ELIMU YA JUU
UTARATIBU KWA WAAJIRI NA WAAJIRIWA KATIKA UREJESHAJI WA

MIKOPO YA ELIMU YA JUU


Swali: Mwajiri anapaswa kufanya nini baada ya kuajiri wahitimu wapya?

· Kwa mujibu wa sheria Na. 9 ya mwaka 2004 ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (kama ilivyorekebishwa), mwajiri anapaswa aijulishe Bodi kwa maandishi kuhusu waajiriwa wapya ambao ni wahitimu wa vyuo vya elimu ya juu ndani ya siku ishirini na nane (28) tangu tarehe ambayo wahitimu hao wameajiriwa.


Swali: Nini kitafuata baada ya kuwasilisha HESLB orodha ya wahitimu walioajiriwa?

· Baada ya kupokea taarifa kutoka kwa waajiri, Bodi itabainisha wafanyakazi walionufaika na mikopo ya elimu ya juu.


Swali: Mwajiri ana wajibu gani baada ya kupokea orodha ya wadaiwa wa mikopo kutoka HESLB?

· Anapaswa kuhakikisha kuwa makato ya kila mwezi kutoka kwenye mishahara ya wadaiwa wa mikopo yanawasilishwa Bodi kama ilivyoelekezwa ndani ya siku kumi na tano (15) baada ya kila mwisho wa mwezi.


Swali: Nini kitatokea endapo mwajiri ataacha kukata mshahara wa mfanyakazi baada ya kuelezwa na HESLB kwamba mfanyakazi huyo ni mdaiwa wa mkopo?

· Iwapo mwajiri atashindwa kukata ama kukata mshahara wa mdaiwa wa mkopo na kushindwa kuwasilisha makato hayo Bodi ndani ya muda uliopangwa, atatozwa asilimia kumi (10%) ya kiasi cha deni lililopaswa kulipwa kwa kila mwezi ambao makato hayatawasilishwa.


Swali: Ni lini mnufaika wa mkopo anapaswa kuanza kurejesha mkopo wake?

· Mkopo huanza kulipwa unapomalizika mwaka mmoja wa neema baada ya kuhitimu masomo ya elimu ya juu au baada ya kusitisha masomo kwa sababu yoyote ile.


Swali: Je, ajira ya mdaiwa wa mkopo ni jambo linalozingaliwa katika urejeshaji wa mikopo?

· Wadaiwa wanapaswa waanze kurejesha mikopo muda unapofika bila kujali iwapo wameajiriwa ama la.


Swali: Ni asilimia ngapi hutozwa kama tozo la kutunza Thamani ya fedha kwa kila mdaiwa wa mkopo?

  • Madeni yote ya mikopo hutozwa asilimia sita (6%) kama tozo la kutunza Thamani ya Fedha (VRF) kwa mwaka.

Swali: Kwa nini HESLB inatoza tozo la kutunza Thamani ya Fedha (VRF) kwenye mikopo inayorejeshwa?

· Mikopo inatozwa tozo la kutunza Thamani ya Fedha ili kutunza thamani ya fedha dhidi ya mfumuko wa bei ambao unapaswa kuwa na thamani sawa wakati mkopo utakapotolewa kwa wanafunzi wengine wenye uhitaji katika siku zijazo.


Swali: Ni hatua zipi za kisheria zitachukuliwa kwa wadaiwa ambao hawatarejesha mikopo yao?

· Mdaiwa yeyote ambaye, bila sababu za msingi atashindwa kulipa mkopo atachukuliwa hatua za kisheria. Aidha, mambo yafuatayo yatafanyika:
(a) Atapata adhabu ya kulipa asilimia kumi (10%) ya mkopo wake wote.
(b) Taarifa zake zitawasilishwa kwenye taasisi zinazosimamia taarifa za

wakopaji wanaotaka kukopa kutoka taasisi za fedha zinazotoa mikopo,

ambapo watazuiliwa kukopa kutoka kwenye Taasisi za Fedha.
(c) Atazuiliwa kupata ufadhili wa Serikali kwa ajili ya masomo ya Uzamili au

Uzamivu katika chuo chochote cha Elimu ya Juu ndani na nje ya nchi.
(d) Maelezo yao yatawasilishwa Wizara ya Mambo ya Ndani, Idara ya

Uhamiaji ambapo hawatapewa kibali kwa ajili ya kusafiri nje ya nchi


Swali: Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali(CAG) na kampuni zingine binafsi za ukaguzi wana wajibu gani katika urejeshaji wa mikopo?

· Jukumu la Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG) na makampuni mengine binafsi ya Ukaguzi ni kuhakikisha waajiri wanatekeleza kwa kuwasilisha wahitimu Bodi ya mikopo na makato ya fedha kutoka kwa wadaiwa yanawasilishwa kama ilivyoelekezwa.


Swali: Mnufaika wa mkopo anapaswa kufanya nini ili kulipa deni lake?

· Mara baada ya kuhitimu masomo au kusitisha masomo yake kwa sababu yoyote ile, mnufaika anapaswa aitaarifu Bodi kwa maandishi mahali alipo na hali ya ajira yake ili kukubalina na Bodi juu ya ulipaji wa mkopo wake.


Swali: Makato huwasilishwaje HESLB?

· Kwa wanufaika waajiriwa, hukatwa asilimia nane (8%) ya mshahara wa kila mwezi.

· Mnufaika anaweza kulipa kiwango cha chini cha shilingi 100,000/= kila mwezi kupitia Akaunti zifuatazo:
i. Benki ya Posta Tanzania CCA0240000032
ii. NMB Bank Akaunti 2011100205
iii. Benki ya CRDB Akaunti 01J1028467503

-------------------------
Asante sana ila naomba kujua ile 10% analipa mwajiri au mwajiriwa?
 
10% unalipa wewe kama penalty ya kuchelewa kuanza kuresha mkopo baada ya grace period kumalizika
 
Back
Top Bottom