Hemed PhD: Sitaacha kujipodoa

Hemed PhD: Sitaacha kujipodoa

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,582
Reaction score
28,734
hemedi_suleiman_06-220x300.jpg


MWIGIZAJI wa filamu na msanii wa Bongo Fleva, Hemed Suleiman ‘Hemedy PhD’, amesema kwamba hataacha kutumia vipodozi kwa kuwa humuweka nadhifu na humwongezea mvuto wa mwili wake.

Hemed anayetamba na wimbo wake wa ‘Imebaki stori’, alisema vipodozi anavyotumia zaidi ni poda, lipshine na pafyum na hataacha kujiremba.

“Sitaacha kujiremba kwa sababu kujiremba siyo kwa wasichana tu hata wanaume tunatakiwa tujipake vipodozi, kama poda na lipshine zinasaidia kuongeza mvuto na mwonekano nadhifu zaidi, mimi ni staa natakiwa niishi kistaa hivyo vipodozi ni kitu cha kawaida.

“Mara nyingi vipodozi navitumia nikiwa katika kazi zangu ili nionekane tofauti nyumbani na kazini hivyo nasisitiza kwamba siwezi kuacha kupaka vipodozi kwa kuogopa maneno ya watu,” alimaliza Hemed.

Source: Hemed PhD: Sitaacha kujipodoa kwa hofu ya watu
 
Kujipodoa!! huu msamiati nahisi unawahusu sana wakina Dada,,,anyway jirembe mwana
 
Kujipodoa!! huu msamiati nahisi unawahusu sana wakina Dada,,,anyway jirembe mwana
teh teh teh
wanaume wa siku hizi nao wanajipodoa aiseeee, full kushinda saluni wanafanya ma-scrub , mara sijui kujiangalia angalia kwenye vioo, yaani full mbwembwe
 
Vijana wa Dar sijui wamekumbwa na jinamizi gani....yaani maneno haya yanatoka kwenye kinywa cha mwanamume kabisaa.....???
 
jipaka hilooo..!
lampiga mwizi kwa taulo!
"USHOGA NI PAMOJA NA KUWA NA TABIA ZA UPANDE WA PILI WAKIMAUMBILE.
*KIJIREMBA,N.K.
 
Sipati picha akioa au akiwa na girlfriend huyu jamaa, dressing table itasheheni sana
 
Mmh!!!makubwa dume kabisa eti unajipodoa na lipshine juu.mungu nusuru watoto wetu wa kiume.
 
Back
Top Bottom