Serikali imetolea ufafanuzi mara kadhaa kuhusu swala hilo na kusisitiza kuwa, TV zenye tumbo zitaendelea kutumika hata baada ya kuhama kutoka analojia kwenda digitali. Cha msingi,baada ya kuhama technolojia, wenye TV za tumbo watatakiwa kununua ving'amuzi kwa kuwa TV za tumbo hazijajengewa ving'amuzi vya ndani.