Heko TRL kwa usafiri Pugu-Stesheni

Heko TRL kwa usafiri Pugu-Stesheni

kalulukalunde

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2016
Posts
1,056
Reaction score
1,086
WIKI hii Kampuni ya Reli Nchini (TRL) imeanza kutoa huduma ya usafiri wa treni mpya inayotoka Stesheni hadi Pugu jijini Dar es Salaam.

Juzi na jana treni hiyo imeanza kufanya majaribio kwa kutotoza nauli ili kuwawezesha abiria kujifunza jinsi ya kuitumia pia kuwapatia TRL nafasi ya kujua changamoto kwa watumiaji. Hata hivyo leo huduma ya usafiri inaanza rasmi na abiria wataanza kutozwa nauli.

Treni hiyo itakuwa na mabehewa 10 na itapita katika vituo 10 vya Pugu Stesheni, Mwisho wa Lami, Gongo la Mboto, FFU Mombasa, Banana, Njia Panda Segerea Karakata, Vingunguti Mbuzi, Bakhresa, Kamata na Stesheni. Huduma inayotolewa na treni hiyo inasaidia kupunguza tatizo la usafiri kwa wakazi wa maeneo ambayo treni hiyo inapita.

Hakika hatua ya TRL kuanzisha huduma hiyo ya usafiri inapaswa kuungwa mkono na kila mpenda maendeleo kwa kuwa imeondoa kero ya muda mrefu ya tatizo la usafiri. Wananchi wanaotumia treni hiyo sasa wataweza kuwahi maofisini na katika shughuli mbalimbali za maendeleo bila kupoteza muda na kuunga mkono kauli ya Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano ya “Hapa Kazi Tu.”

Wananchi wanaotumia usafiri huo hawapati adha ya foleni. Pia treni hiyo itasaidia kupunguzia gharama za usafiri na kuboresha hali ya maisha katika kaya kwa kuwa awali walilazimika kupanda magari ya watu binafsi kwa Sh 2,000 na wakati mwingine walilazimika kulipa nauli mara mbili.

Napenda kupongeza uongozi mzima wa kampuni hiyo na kuwasihi kufanya tathmini ya watu wanaotumia usafiri hiyo ili kama itabaini watu ni wengi iwezi kuongeza idadi ya mabehewa ili kuepuka msongamano ulioonekana kwa siku hizo mbili. Ni dhahiri kuwa baada ya kufanya majaribio kwa siku mbili wameona mafanikio na changamoto katika njia hizo hivyo kuweza kufanyia kazi wakati wakianza kazi rasmi leo.

Katika baadhi ya mambo ya kufanyia kazi ni pamoja na kuhakikisha kunakuwa na usalama katika milango kwa kuweka wasimamizi kwani kumekuwa na abiria waliokuwa akining’inia milangoni jambo linaloweza kusababisha ajali wakati wa safari hizo.

Katika kuhakikisha usafiri huo unakuwa na tija zaidi ni vyema wananchi kuusimamia na kuwa sehemu ya mradi kuhakikisha kuwa miundombinu ya treni hiyo inalindwa ili huduma hiyo iweze kuwa endelevu.

Mbali na kuhakikisha wanafuata taratibu zote zilizowekwa na kampuni hiyo katika usafiri ni vyema abiria kuzingatia masuala ya usafi kwa kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenziwe kwa kuhakikisha vyombo vya kuhifadhia uchafu vinatumika ipasavyo.

Hakika pongezi ziende kwa menejimenti ya kampuni hiyo iliyoona mateso ya wakazi wa maeneo hayo na kuamua kuanzisha usafiri huo na kutanuka zaidi katika maeneo mengine yenye reli kwani inasaidia kupunguza misongamano barabarani.
 
Ni jambo zuri linafaa kupongezwa lakini kwa train ya kwenda kigoma ile ya kawaida siyo ile mpya ni heli wangeitoa saa nne usiku au saa mbili kuepusha muingiliano na hiyo ya Pugu.. Lakini pongezi kwa Mh Magufuli na Kaimu mkurugenzi Kadogosa kwa kazi nzuriiii
 
Behewa Jana zilikuwa zaidi ya 12 but lilijaa mnazi mmoja na abiria wengine walibaki. Vituo vingine hakupanda mtu maana watu walikaa hadi nje ya milango.
Behewa ni ndogo mno inabidi ziongezwe ikiwezekana zifike 20.
Hii ni sawa unawaalika watu kwenye sherehe na watu wanaondoka bila kula ndivyo ilivyokuwa Jana kwani tulioweza kupanda ni wanaume tena kwa kiwango kikubwa wenye uwezo wa kupita madirishani.
Naomba wahusika waliangalie hilo
 
Behewa Jana zilikuwa zaidi ya 12 but lilijaa mnazi mmoja na abiria wengine walibaki. Vituo vingine hakupanda mtu maana watu walikaa hadi nje ya milango.
Behewa ni ndogo mno inabidi ziongezwe ikiwezekana zifike 20.
Hii ni sawa unawaalika watu kwenye sherehe na watu wanaondoka bila kula ndivyo ilivyokuwa Jana kwani tulioweza kupanda ni wanaume tena kwa kiwango kikubwa wenye uwezo wa kupita madirishani.
Naomba wahusika waliangalie hilo
Mkuu ule utaratibu wa kupanda kwa foleni umeshindikana kutumika hadi muingie kwa dirishani
 
Mkuu ule utaratibu wa kupanda kwa foleni umeshindikana kutumika hadi muingie kwa dirishani
Hilo haliwezekani kwani ni sawa na kuandaa chakula cha watu mia alafu wanakuja watu mianne. Na watanzania kwa ubwabwa lazima kuwe na vurugu.
Mi sasa hivi nipo kwenye daladala mpaka nitakaposikia utaratibu umekaa vizuri.
Maana Jana nilikata saa yangu wakati tunagombania kupita dirishani
 
Behewa Jana zilikuwa zaidi ya 12 but lilijaa mnazi mmoja na abiria wengine walibaki. Vituo vingine hakupanda mtu maana watu walikaa hadi nje ya milango.
Behewa ni ndogo mno inabidi ziongezwe ikiwezekana zifike 20.
Hii ni sawa unawaalika watu kwenye sherehe na watu wanaondoka bila kula ndivyo ilivyokuwa Jana kwani tulioweza kupanda ni wanaume tena kwa kiwango kikubwa wenye uwezo wa kupita madirishani.
Naomba wahusika waliangalie hilo
pia kumbuka ilikua bure kwa siku 2 hizo yaweza ikawa sbabu ya hiyo nyom ya kupindukia.
 
N
pia kumbuka ilikua bure kwa siku 2 hizo yaweza ikawa sbabu ya hiyo nyom ya kupindukia.
Ni Kweli mkuu but haiwezekani behewa 10 zikatosheleza.
Hii reli inawafaidishwa watu wengi kwani haipo mbali na barabara kuu. Watu wa chanika, msongola, pugu, majohe, kivule, kitunda, gongolamboto, ukonga, sehemu kubwa ya segerea na kinyerezi, airport, Vingunguti, buguruni na maeneo mengi zaidi.
Huwezi ukaacha treni ukapanda gari kwani foleni ya gari unaweza kuchukua hadi masaa ma tatu au mawili na nusu kufika mjini kipindi cha asubuhi au jioni kutoka kwenye mihangaiko.
Kuna watu wengi mno
 
Mabehewa hayo hayatoshii ile njia ina watu wengi jamani waongeze ziwe behewa 20+ abiria wa ubungo pia watapanda hiyo treni ili washuke k.koo wapande magari ya mwendo kasi.
Na ile njia ya tazara pia waongeze mabehewa maaana kuna abiria wengi njia ile.
 
Mambo mazuri kweli

Mimi ombi nikuongeza safari zake
Hii ingependeza sana
 
Nihatua nzuri kwakweli hata mwaka mmoja JMPM hajamaliza tunaona mambo mazuri nimeona Jana pia kuna kituo kilisha jengwa kwafedha za Umma BT kilikuwa kimefungwa ameamuru kifunguliwe.

Kuuhusu treni baadae wajipange watoe kadi watu tulipie Kwa kadi
 
Nihatua nzuri kwakweli hata mwaka mmoja JMPM hajamaliza tunaona mambo mazuri nimeona Jana pia kuna kituo kilisha jengwa kwafedha za Umma BT kilikuwa kimefungwa ameamuru kifunguliwe.

Kuuhusu treni baadae wajipange watoe kadi watu tulipie Kwa kadi

Yeah Mkuu hili la kadi umenena. Lkn kabla ya hayo maboresho kadhaa yanatakiwa. Tutafika tu hatimaye!
 
Back
Top Bottom