Hekima ya baba huonekana kwa mtoto

Hekima ya baba huonekana kwa mtoto

Mfumo dume in action, VP kwa mtoto single Mather, hekima yake bado inareflect kwa baba?!?!
 
Kwa kifupi tu mboko zisitishwe au siyo? Au ndo yale ya junior stop, junior is not good ya jamaa mmoja

Sent using Jamii Forums mobile app
Haujaelewa bandiko na majibu nnayoyatoa,tumia muda kidogo kufikiri kisha ndio uandike,bandiko langu nimeliweka kwa ujumla nikionyesha umuhimu wa baba kwa mtoto na malezi yake, sijagusia vitu vya kufanya na kuacha,

kumkanya mtoto kwa fimbo iko sehemu zote ukimchapa kwa hekima anajua fimbo ni adhabu ya makosa ila ukimchapa kila saa anaiozea na inakuwa fimbo ndio maisha, hivyo kikubwa ni hekima ya baba ndio inaongoza aidha kwenye kuchapa, kuonya, kufundisha, kuiga nakadhalika.
 
Mfumo dume in action, VP kwa mtoto single Mather, hekima yake bado inareflect kwa baba?!?!
hakuna mfumo dume kwenye malezi na ila ni umuhimu wa baba kwenye malezi ya mwanae,nadhani wewe ndio unashangilia mfumo dume kwa kuona ni sawa mtoto kulelewa bila baba na baba asijali athari za baadae kwa mwanae...single mother hapati hekima ya baba jibu lake nimeliandika uzuri kwenye moja ya swali huko juu kuhusu watoto waliolelewa na mama peke yake.
 
Ukali wa wazazi umetukuza sana, nami pia kifimbo cheza na ukali pia kwa wanangu....

Sent using Jamii Forums mobile app
Safi kabisa hiyo ndio hekima inayoongelewa nadhani kwa sasa unaielewa vizuri dhana ya ukali na kufunza na kufanya kitu kwa mtoto ili atambue amekosea na hujaridhishwa nacho,zamani ulipokuwa mdogo ulikuwa unaona unaonewa sana kwa ukali wao na fimbo zao lakini kwa sasa unasema bila zile huenda usingekuwa huyu tunaekuona sasa,

lakini vivyo hivyo kwa nafasi yako kama baba unatumia ukali kuna muda sio kama umekasirika kwa kiwango unachokionyesha ila unaonyesha hisia kali ili mtoto ajifunze zaidi,unamchapa sio kama kosa ni kubwa sana ila unamkumbusha anatakiwa kutembea kwenye mstari na kuna muda ambapo unakutana na kisanga kikubwa hadi mtoto anajua leo anaenda kuuawa kwa adhabu halafu unamsamehe/ ama unasamehewa ila kwa onyo la adhabu kali kuliko zote ama kwa adhabu ya kawaida hiyo yote ni kumjenga mtoto na hapo ndio hekima ilipo.

Hivyo wachangiaji wengi wanakimbilia kwenye fimbo kama vile bandiko linakataza fimbo hasha,bandiko linagusia hekima ya malezi ya baba.hata fimbo ikiwemo ila matumizi yake lazima yaongozwe na hekima ili kumfundisha mtoto,na jibu lako linaksi vizuri kabisa mada ya kwamba watoto huiga zaidi tunayofanya kuliko tunayosema.
 
Hii theory imekaa kizungu zaidi....japo nakubaliana na wewe kwenye mambo kadhaa ila kwenye bakora hapana😁
 
Hii theory imekaa kizungu zaidi....japo nakubaliana na wewe kwenye mambo kadhaa ila kwenye bakora hapana😁
Rudia tena kusoma naimani utaelewa zaidi ya hapo...na uangalie bakora nimeiandika kwa mlengo upi mkuu.
 
Back
Top Bottom