Mr RoundAbout
Member
- Oct 6, 2023
- 70
- 85
Ndugu zangu watanzania, Taifa letu liko katika kipindi kigumu kuwahi kutokea Kulingana na aina ya uongozi uliopo wa Chama na serikali. Baada ya kushuhudia heka heka nyingi zikiwemo za mikataba ya DP world, kupanda Kwa garama za maisha, matumizi mabaya ya madaraka Kwa walio nayo, ukiukwaji wa sheria Kwa baadhi ya Viongozi na mengine mengi. Bado inaonekana hakuna kiongozi ambaye anawaza na anaweza kulifanya Taifa hili likawa la HAKI na UTULIVU ambao siyo unafiki unaoendelea Sasa. Badala yake wahusika wakuu wameendelea na tabia zile zile za UNYANI pasipo kujali shida na taabu za watanzania maskini ambao wanaunda asilimia 80 ya Taifa letu. Wako bize kufanya mipango na Hila Ili waendelee kukutana katika vikao vikubwa DODOMA, wakilipana posho za walipa Kodi ambao ni maskini pasipo kujali shida zao.
Imefika wahali mtu akisimama Kwa lengo la kukosoa vikundi vya ambavyo vinanufaika na maliasili ya Taifa hili, ataitwa kila aina ya majina Ili mradi tu, aonekane hafai, na baadaye kuondolewa katika nafasi aliyokuwa nayo. Lengo ni kuimarisha mfumo wa kulindani ambao waasisi wake ndiyo kikundi na tabaka la mabwanyenye wa Taifa hili maskini. Mbaya zaidi mamlaka ya juu ya Nchi Iko kimya nayo inatumika Kwa kalamu kuidhinisha upuuzi huu wa wachache kutawala wengi. Ewe QEEN of SHEBA, Je? Utatukuzwa mpaka mbinguni kama mfalume SULEIMANI? Jibu ni HAPANA, Bali utashushwa mpaka KUZIMU ambako alishushwa mfalume JUHA baada ya waliokuwa wanamzunguka kumtengea kiti cha kukaa juu ya shimo ambalo lilikuwa limeandaliwa pasipo yeye mwenyewe kujua kwasababu ya kuendekeza dhuluma, tamaa, majungu, ubaguzi, kujuana, kulindana na taka2 nyingi zinazofanana na hizo.
Zimefika nyakati ambapo hakuna JIWE, litakalo baki juu ya JIWE.......
PASAKA NJEMA!
Imefika wahali mtu akisimama Kwa lengo la kukosoa vikundi vya ambavyo vinanufaika na maliasili ya Taifa hili, ataitwa kila aina ya majina Ili mradi tu, aonekane hafai, na baadaye kuondolewa katika nafasi aliyokuwa nayo. Lengo ni kuimarisha mfumo wa kulindani ambao waasisi wake ndiyo kikundi na tabaka la mabwanyenye wa Taifa hili maskini. Mbaya zaidi mamlaka ya juu ya Nchi Iko kimya nayo inatumika Kwa kalamu kuidhinisha upuuzi huu wa wachache kutawala wengi. Ewe QEEN of SHEBA, Je? Utatukuzwa mpaka mbinguni kama mfalume SULEIMANI? Jibu ni HAPANA, Bali utashushwa mpaka KUZIMU ambako alishushwa mfalume JUHA baada ya waliokuwa wanamzunguka kumtengea kiti cha kukaa juu ya shimo ambalo lilikuwa limeandaliwa pasipo yeye mwenyewe kujua kwasababu ya kuendekeza dhuluma, tamaa, majungu, ubaguzi, kujuana, kulindana na taka2 nyingi zinazofanana na hizo.
Zimefika nyakati ambapo hakuna JIWE, litakalo baki juu ya JIWE.......
PASAKA NJEMA!