JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
Makamu Mwenyeliti wa CHADEMAB(Bara), John Heche amesema kuwa amekutana na Mwenyekiti wa Chama hicho, Tundu Lissu katika Gereza la Ukonga anakoshikiliwa na kiongozi huyo amewataka wanachana wa chama hicho kuendeleza mapambano.
Lissu alikamatwa Aprili 12 wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma na kisha kuletwa Dar es Salaam ambako alifunguliwa kesi ya uhaini katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu.
Hata hivyo, jana April 18, kulikuwa kuna taarifa kuwa kiongozi huyo alihamishwa Gereza la Keko lakini haikujulikana amepelekwa wapi, hadi ilipojulikana leo kuwa yuko Gereza la Ukonga.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akizungumza leo Aprili 19 katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ukonga Mombasa, Heche amesema amekutana na Lissu Gereza la Ukonga.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche akizungumza na Wananchi wa Jimbo la Ukonga, Aprili 19, 2025
"Saa mbili zilizopita nimetoka gerezani na nimeonana na Lissu. Kama mnavyojua Lissu alikamatwa na alifunguliwa kesi kubwa ya uhaini, ambayo hukumu yake ni kifo.
"Mtu ambaye alipigwa risasi 16, Serikali imemfungulia kesi ya uhaini, hajaiba kitu cha mtu, hajamkosea mtu, kosa lake ni kitaka kila mtu achague kwa usawa," amesema.
Soma Pia: Brenda Rupia: Taarifa rasmi Tundu Lissu amehamishiwa gereza la Ukonga, Heche anatarajiwa kufika Ukonga leo kwa ajili ya kumwona
Heche amesema amemkuta Lissu akiwa anaendelea vizuri.
"Amesema mapambano yaendelee na mimi nasema mapambano yaendelee."
Kuhusu kuhamishwa gereza, Heche amekosoa kuhamishwa kwa kiongozi huyo bila kuwajulisha.
"Wamemhamisha kutoka Keko kuja Ukonga bila kutaarifu wanafamilia yake. Nchi hii sio kikundi fulani kinachoamua kila kitu.
"Hata kina Mandela alipofungwa Robben island makaburu Wazungu walijulisha wanafamilia," amesema.
Lissu alikamatwa Aprili 12 wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma na kisha kuletwa Dar es Salaam ambako alifunguliwa kesi ya uhaini katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu.
Hata hivyo, jana April 18, kulikuwa kuna taarifa kuwa kiongozi huyo alihamishwa Gereza la Keko lakini haikujulikana amepelekwa wapi, hadi ilipojulikana leo kuwa yuko Gereza la Ukonga.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akizungumza leo Aprili 19 katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ukonga Mombasa, Heche amesema amekutana na Lissu Gereza la Ukonga.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche akizungumza na Wananchi wa Jimbo la Ukonga, Aprili 19, 2025
"Saa mbili zilizopita nimetoka gerezani na nimeonana na Lissu. Kama mnavyojua Lissu alikamatwa na alifunguliwa kesi kubwa ya uhaini, ambayo hukumu yake ni kifo.
"Mtu ambaye alipigwa risasi 16, Serikali imemfungulia kesi ya uhaini, hajaiba kitu cha mtu, hajamkosea mtu, kosa lake ni kitaka kila mtu achague kwa usawa," amesema.
Soma Pia: Brenda Rupia: Taarifa rasmi Tundu Lissu amehamishiwa gereza la Ukonga, Heche anatarajiwa kufika Ukonga leo kwa ajili ya kumwona
Heche amesema amemkuta Lissu akiwa anaendelea vizuri.
"Amesema mapambano yaendelee na mimi nasema mapambano yaendelee."
Kuhusu kuhamishwa gereza, Heche amekosoa kuhamishwa kwa kiongozi huyo bila kuwajulisha.
"Wamemhamisha kutoka Keko kuja Ukonga bila kutaarifu wanafamilia yake. Nchi hii sio kikundi fulani kinachoamua kila kitu.
"Hata kina Mandela alipofungwa Robben island makaburu Wazungu walijulisha wanafamilia," amesema.