GE2025 Heche: Kwanini watu wanatekwa na kupotea? Hawa wanaojiita "viongozi" kazi yao ni nini?

GE2025 Heche: Kwanini watu wanatekwa na kupotea? Hawa wanaojiita "viongozi" kazi yao ni nini?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Kupitia ukurasa wake wa X, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche amehoji na kuendelea kuonesba masikitiko yake juu ya vitendo vya utekaje. Heche anaandika;

"Vyombo vyetu vya dola, polisi wetu hawapaswi kuwa chanzo cha hofu kwa watu.

Mwl Nyerere hakuunda Nchi na vyombo vya kujaza watu hofu.

Hivi vilipaswa kuwa vyombo vya kulinda raia, sasa vimegeuka kujaza watu hofu na kuwatisha.

Kwanini watu wanatekwa na kupotea, hawa wanaojiita viongozi kazi yao ni nini?

Mnafikiri mtateka watu wote?

Mnafikiri Watanzania watakaa kimya kwasababu ya ushenzi huu.

Mnazima moto kwa petrol, mnachochea hasira ambayo ikiwaka mtajuta sana"
Screenshot_20250928-131623_X.jpg
 
Kwahiyo Heche anamaanisha wanaoteka ni Polisi?
 
Kwa saa wataendelea kuteka ili kuwachokoza viongozi wa CHADEMA wa-react wapate sababu ya kuwaweka ndani kabla ya siku ya maandamano haijafika.
 
Back
Top Bottom