Haya yote yanatokea sababu Watanzania tumedharau wosia wa Baba wa Taifa

Zero Hours

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
12,944
18,652
4166fe7bba40bdff33d18bda00a6837d.jpg


Ni ukweli usiopingika kuwa sasa Watanzania tumepuuza mafunzo tulioachiwa na Hyati Baba Wa Taifa, Julius Kambalage Nyerere. Hya yote yanayotutokea sasa ni kwasababu tumepuuza wosia wake na tumejiona tunaweza kufanya tutakavyo kuanzia viongozi hadi Wananchi wake.


065e5c14233d32c3337c1197a3809290.jpg




Tunatengeneza Taifa la vijana Wanafiki na Waoga. Tunavyozidi kuwa waoga ndivyo tunazidi kuwapa viongozi kiburi cha kuwajibisha wale wanao simamia ukweli na kuhoji.

Huwa nawaeleza watu kuwa wanakosea sana wanaposema kuwa serkali ya kikwete ndyo iliongoza kwa ufisadi kila kona. Serkali ya kikwete mpaka sasa ni serkal pekee iliyotengenezea mazingira ya wananchi wake kuhoji. Ndyo maana tukajua madudu yote yaliyotokea hata kwenye serkali ya Mkapa. Watanzania tusipokuwa makini tutarudishwa kulekule. Yani tutaibiwa huku tunaona na tutaogapa kuhoji.

e71cf4d89391656ab853071afa22e255.jpg


Ni aibu kuona kuwa kazi ya kukosa serkali ni kazi ya vyama vya upinzani Tu. Ndyo maana siku hizi mtu akikosoa serkali kama ni mwana CCM anaitwa Msaliti.
a9c78828afa3328b8f59f1d812e5de83.jpg

Watanzania kumbukeni hii ni nchi yetu wote. Hii nchi sio ya Magufuli wala Bashite. Ni jukumu letu kukosoa pale wanapokosea. Maana makosa wafanyayo yanatuumiza sisi sio wao. Wao hawajui hata bei ya unga sokoni inauzwaje. Wanaletewa tu wanakuta chakula mezani kwa kodi zetu.
9893731aa7a1045622e0ec076b5d4936.jpg
 
CCM itatawala Milele

Kwanza taja viongozi wakubwa waliopo Upinzani ambao ni TISS (Usalama)

Watanzania mnachezewa sinema

Watanzania ni wapole na waoga
 
Mimi kwa upande wangu, nimefurahia yaliyomkuta nape.
alihusika Sana Kwenye wizi wa jirani, kumbe walikuwa wanampa nchi mtu wasiyemjua.
Kuhangaika kote wanaishia kuwekwa pembeni na waliokuwa wanakula zao bata Ndio wanaendesha nchi.
Safi Sana.
Nadhani na wengine watajifunza.
 
Kwa uchaguzi ujao Lazima wasukuma wote waingie kupiga kampeni.
Maana hakuna watakakomkubali
 
Back
Top Bottom