Haya yatatokea siku Said Mwema (IGP) atakapokuwa huru

RealMan

JF-Expert Member
Nov 9, 2010
2,367
1,388
Siku Wakuu wa majeshi yetu (polisi, magereza, JW) na vyombo vingine vya usalama watapokuwa huru kifikra na kimaamuzi kutoka ktk minyororo ya Chama Tawala tutashuhudia raia wakilindwa na hawatawindwa.

Tulishuhudia raia wakiuawa Pemba na askari kupandishwa vyeo Polisi wakaua raia Arusha tukaambiwa kosa ni la CDM
Nyamongo na Mbarali wameua kumlinda mwekezaji.

Wafanyakazi walipotaka kugoma Rais akamwambia Mgaya wakithubutu watapambana na risasi za polisi. Kwa kifupi majeshi hayapo kulinda usalama wetu bali usalama wa watawala

Majuzi kule Naivasha raia waliandamana lakini baadhi ya polisi wenye fikra za kiCCM au kiKANU wakatembeza rungu lakini sasa imekula kwao.

Kibarua kimeota magugu maji. Hebu tazama picha kwenye link hii
Caught on camera, on air: Police brutality in Kenya; Administration apologies, Officer involved gets fired! - Wavuti

I have a dream that, One day the CDF, IGP, TISS, TCCB, NEC will walk and work free. I dream of living in new Tanzania with a new pro wananchi constitution. That dream,,,, will come to pass in my life time!!

Amani haiji ila kwa ncha ya "Upanga", tupiganie katiba mpya sasa wakati wa amani tusisubiri machafuko kama ya Kenya 2007/2008.

Mwenye hekima hujifunza kwa makosa ya wenzake....Chukua hatua

RM
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom