Haya yanatokea Zanzbar tu?

Haya yanatokea Zanzbar tu?

Malungwana

Senior Member
Joined
Sep 14, 2013
Posts
187
Reaction score
99
Habari wana jamii.

Haya mambo yanatokea Zanzibar tu, sujawahi kuona.

Juzi kati, kama siku mbili tu hivi zilizopita, pale kwenye "take away restaurant Malindi Zanzibar" palitokea wizi, usiku, basi vijana wakamfukuza yule mwizi, wakamkamata wakampigaaa, then wakajifanya eti wanampeleka police, kumbe wakampeleka sehemu wakaanza kumlawiti huwezi amini wakamlawiti sana, yule kijana kutoka pale akaenda police kushitaki, akaseme kweli mimi nilikua naiba lakini baada ya kunikamata ilikua wanipeleke police, lakini kinyume chake wananilawiti,....... ukichunguza sana unakuta huyo kijana aliyelawitiwa ni kijana wa kibongo (kutoka bara).

Ikitokea fujo Zanzibar, na akiwa anayepigwa ni mbongo, basi watu hawaingilii kabisa, na utasikia kauli, "acha afe, mbongo sio mtu kabisa" dah!

Kuna jamaa (mbongo) kajenga maeneo ya Bububu Kijichi, basi kajenga katikati na amezungukwa na wazanzibari ( hasa wapemba) jamaa ana kijigari, basi yaani wanasema kweli, "ilikuaje mbongo akapata maeneo hapa" jamaa ni muislam, ila tatizo ni mbongo!!!!!

Jamaa mwengine yeye amejenga maeneo ya Kwarara, tene yupo maeneo yale siku nyingi kweli, kabla hata hao jamaa ( wapemba) hawajahamia, wao ndio waazilishi, ila sasa wamejaa na nyumba yake yote imezungukwa, miezi kama mitatu nyuma, aliwekewa bomu la kutengenezwa nyumbani kwake wakitaka wairipue nyumba yake, hadi wakaja wanajeshi ndio wakalitoa hilo bomu, hivi sasa jamaa anauza nyumba yake ahame pale, tatizo wanunuzi ndo wale wale, wanailazia bei nyumba yake ili waichukua kwa bei rahisi, jamaa ni muisilamu safi sana, swala tano tena, ila tatizo ni "mbongo"

Kuna mwengine yeye ni mzaliwa kabisa wa Zanzibar, kasoma na kakulia Zanzibar, ana kazi yake nzuri tu ya ujasiriamali, sasa ameoa Mzanzibari ( sio mpemba), yaani sasa jamaa wanakua wanamshangaa sana, yaani wanasema " eti oooo inakuaje mbongo aoe mzanzibari, si akachukuwe wabomgo wenzake kule Tabora" tatizo ni nini jamani.

Dhambi ya ubaguzi Zanzibar haitaisha kabisa, ila mimi najiuliza je huko Dar, maeneo ya Kariakoo ambapo wamejazana kama njugu hivi wanabagukiwa kama hivi? kila kona sasa ya Tanzania bara wamejaa, je wanabaguliwa?

Naomba majibu jamani.
 
Du hawa jamaa ni wabaguzi hata hapa tz bara hasa tanga wabaguzi kupitiliza.
 
No,maana yangu kwa haya uliyosema sio ajabu.yametokea mengi sana.tunatakiwa tujue kule hatutakiwi.
 
Ila lugha yako nzuri mno,sijui hata kwa wazazi huwa unajibu hivyo,kama hukuelewa kitu mwambie MTU akufafanulie.
 
Ila lugha yako nzuri mno,sijui hata kwa wazazi huwa unajibu hivyo,kama hukuelewa kitu mwambie MTU akufafanulie.

Na wewe unapondika, please andika in a such a way that mtu anaelewa direct
 
Hakuna ajabu kwako kulawitiwa!?? watu wengine wan vichwa kama mfereji wa maji machafu!


kwanza shangaa ya Padri Mushi aliyelawiti mtoto pale changanyikeni karibu na chuo kikuu kabla ya kushangaa ya hao wahuni wa zanzibar!! Kwanza huku bara ndio asingepona kabisa huyo kibaka! wangemlawiti na kumuua kabisa
 
Habari wana jamii.

Haya mambo yanatokea Zanzibar tu, sujawahi kuona.

Juzi kati, kama siku mbili tu hivi zilizopita, pale kwenye "take away restaurant Malindi Zanzibar" palitokea wizi, usiku, basi vijana wakamfukuza yule mwizi, wakamkamata wakampigaaa, then wakajifanya eti wanampeleka police, kumbe wakampeleka sehemu wakaanza kumlawiti huwezi amini wakamlawiti sana, yule kijana kutoka pale akaenda police kushitaki, akaseme kweli mimi nilikua naiba lakini baada ya kunikamata ilikua wanipeleke police, lakini kinyume chake wananilawiti,....... ukichunguza sana unakuta huyo kijana aliyelawitiwa ni kijana wa kibongo (kutoka bara).

Ikitokea fujo Zanzibar, na akiwa anayepigwa ni mbongo, basi watu hawaingilii kabisa, na utasikia kauli, "acha afe, mbongo sio mtu kabisa" dah!

Kuna jamaa (mbongo) kajenga maeneo ya Bububu Kijichi, basi kajenga katikati na amezungukwa na wazanzibari ( hasa wapemba) jamaa ana kijigari, basi yaani wanasema kweli, "ilikuaje mbongo akapata maeneo hapa" jamaa ni muislam, ila tatizo ni mbongo!!!!!

Jamaa mwengine yeye amejenga maeneo ya Kwarara, tene yupo maeneo yale siku nyingi kweli, kabla hata hao jamaa ( wapemba) hawajahamia, wao ndio waazilishi, ila sasa wamejaa na nyumba yake yote imezungukwa, miezi kama mitatu nyuma, aliwekewa bomu la kutengenezwa nyumbani kwake wakitaka wairipue nyumba yake, hadi wakaja wanajeshi ndio wakalitoa hilo bomu, hivi sasa jamaa anauza nyumba yake ahame pale, tatizo wanunuzi ndo wale wale, wanailazia bei nyumba yake ili waichukua kwa bei rahisi, jamaa ni muisilamu safi sana, swala tano tena, ila tatizo ni "mbongo"

Kuna mwengine yeye ni mzaliwa kabisa wa Zanzibar, kasoma na kakulia Zanzibar, ana kazi yake nzuri tu ya ujasiriamali, sasa ameoa Mzanzibari ( sio mpemba), yaani sasa jamaa wanakua wanamshangaa sana, yaani wanasema " eti oooo inakuaje mbongo aoe mzanzibari, si akachukuwe wabomgo wenzake kule Tabora" tatizo ni nini jamani.

Dhambi ya ubaguzi Zanzibar haitaisha kabisa, ila mimi najiuliza je huko Dar, maeneo ya Kariakoo ambapo wamejazana kama njugu hivi wanabagukiwa kama hivi? kila kona sasa ya Tanzania bara wamejaa, je wanabaguliwa?

Naomba majibu jamani.


sasa si bora huko mtu naweza kuoa mpemba na akakupenda hata kama wewe ni mbara!.. sasa jaribu kuoa mchaga kama wewe sio mchaga! huyo mke na familia nzima lazima wakuue na kukomba mali zote! ..bara hali ni mbaya kuliko zanzibar! fanya uchunguzi na huku bara matokeo ya utafiti yatakushangaza sana mzee!
 
sasa si bora huko mtu naweza kuoa mpemba na akakupenda hata kama wewe ni mbara!.. sasa jaribu kuoa mchaga kama wewe sio mchaga! huyo mke na familia nzima lazima wakuue na kukomba mali zote! ..bara hali ni mbaya kuliko zanzibar! fanya uchunguzi na huku bara matokeo ya utafiti yatakushangaza sana mzee!

Ahahaha !
 
Huu haukua ila ni uzushi mkubwa. Watanganyika wapo kitambo tunaishi nao kwa amani hapa zanzibar, kwa sababu ni moja ya mhimili mkubwa wa uchumi wa zanzibar. Mizigo yote mizito hubebwa na watanganyika, mashamba hulimwa na watanganyika, karanga na mahindi huuzwa na watanganyika na sisi hununua kwao, na wao ni marafiki zetu .

Wazanzibari ni kama watu wa aina nyengine, ukiishi wanavotaka wao utasalimika lakini ukienda kinyume lazima watakuchukia. Kumbuka usemi 'when you are in rome do as roman do'
 
Duh kaka kwa tanga usiseme tunapata tabu sana hasa kwa sisi wageni maana wao wamekalia majungu na fitna
 
Mbona hata huku bara waislamu wanabaguliwa na wakristo.......
 
Back
Top Bottom